CHADEMA watoa tamko zito, John Mnyika aanika gharama za fomu za kugombea na kutoa mwongozo

CHADEMA watoa tamko zito, John Mnyika aanika gharama za fomu za kugombea na kutoa mwongozo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika anazungumza na Waandishi wa habari muda huu, Makao Makuu ya Chama hicho, Mikocheni Dar es salaam.

Fuatilia live mazungumzo yake hapa

  • CHADEMA yatoa tamko la Uchaguzi wa Kitaifa kwa mwaka 2024
Katibu Mkuu anatangaza kuwa kutakuwa na uchaguzi wa Chama na Mabaraza kwa ngazi ya Taifa utakaofanyika Januari 2025.

Fomu za kugombea ngazi ya Taifa zinapatikana katika ofisi za makao makuu ya Chama (Mikocheni), makao makuu ya Mabaraza, ofisi za Kanda, ofisi za Chama za mikoa na wilaya kuanzia tarehe 17 Desemba 2024. Mwisho wa kurejesha fomu ni Januari 5, 2025, saa 10 jioni katika ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mikocheni Dar es salaam au katika ofisi za Kanda anayotoka mgombea husika.

Wanachama wanaogombea katika mabaraza ya vijana, wanawake na wazee wanatakiwa kurejesha fomu hizo kwenye ofisi za makao makuu ya mabaraza ya Chama zilizoko mtaa wa Ufipa, Kinondoni, Dar es Salaam, au katika ofisi ya kanda anayotoka mgombea husika.

Gharama ya fomu itategemea nafasi ambayo mwanachama anagombea, na mgombea atatakiwa kuambatanisha risiti ya malipo ya fomu katika fomu yake. Fedha hiyo ilipwe kupitia akaunti ya chama au kwa kila baraza ambako mwanachama anatokea mgombea, na namba za akaunti zimeandikwa kwenye kila fomu ya mgombea.

Pia, Soma:

Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA

Tangazo lote limeambatishwa hapo chini👇👇
 

Attachments

Ni utaratibu kaka wala hakuna ubabaishaji .. Na Lissu ndio chaguo la chama
Utashangaa safari hii na utathibitika kuwa mtabiri fake wa Chadema

Mbowe anashinda mapema tu tena kwa kura nyingi mno

Jiandae kuhama Chadema kwa hasira za Lisu kushindwa uchaguzi
 
Wachaga wanaona ulaji unaenda kupotea, TL ataifufua chagadema iliyotaka kupotelea mikononi mwa makonyagi

Kwa jinsi CCM wanavyompa promo TAL awe mwenyekiti naona kuna shida pahala ,Ukizangiatia Abdul alionana na TAL na Pastor Kinyambe ni mshikaji wake sana TAL na ndiye aliyefinance mkutano.
 
CCM ndiyo wanampenda Lissu awe mwenyekiti ndiyo cha kushangaza ,hata mkutano wa lissu umekuwa financed na Pastor Kinyambe Msigwa na waliohudhuria ni wanasisisemu waliovalia mavazi ya CDM.
lissu akiwa mwenyekiti wa chadema ccm itanufaika vipi, au wanamuingiza kingi kwenye kumi na nane zao waimalize kabisa chadema halafu baadae mama ashinde kwa ulaini bila upinzani mkali wa chadema?
 
Back
Top Bottom