CHADEMA yafanya Uteuzi wa Viongozi wa Kanda ya Kaskazini na Kati

CHADEMA yafanya Uteuzi wa Viongozi wa Kanda ya Kaskazini na Kati

kwani uchaguzi huu si unahusu kanda ya kaskazini kwa hiyo iwapo kama watachaguliwa watu wa huko ni kawaida maana hata kanda ya kusini au kanda nyingine waliochaguliwa ni watu toka kanda husika
Kule kanda ya kati kuna mtu anaitwa Minja nae anagombea uwenyekiti
 
Hebu kwanza mkuu 'Makupa'. Naelewa unacho llamikia, lakini kwani kufikia kwenye ngazi hii pamekuwepo na mchujo wa hao wagombea, au ni hiari ya mtu kujitokeza mbele kugombea?

Hili unalo lilalamikia wewe ni sawa na hili jingine ambalo ni kubwa zaidi,.... Tazama vizuri hayo majina. Unaweza kusema CHADEMA imewabagua watu kwa sababu ya imani zao ndiyo sababu hawaonekani kwenye orodha hizo?

Sijui kama CHADEMA wanyayo sera ya kuwakataa watu kwa misingi ya wanako tokea au imani zao. Ila kama ni lawama, labda tuseme hawajafanya bidii ya kutosha kukifanya chama kiwe na mwonekano wa kitaifa zaidi. Inabidi waongeze bidii katika eneo hilo.
Mko vizuri hadi Minja amekuwa Mnyaturu
 
Natamani kujibu lakini naona wakati fulani kujibizana na watu wanaotoa propaganda za kijinga ni kujishusha.

Samaki ukimkuta majini sio ajabu ila ukimkuta nchi kavu anaogolea kwenye vumbi ndio la kushangaa.

Hivi wachaga wanaishi Kanda gani?
Kaskazini Nkuu
 
Kanda ya kaskazini mwenyekiti angefaa Amani Golugwa na hapo kanda ya kati wangempandisha Aisha Madogga. Anyway naona Team Lissu (David Djumbe) vs Team Mbowe (Devotha Minja) hii itatoa picha muelekeo wa Uchaguzi kama atashinda Devotha basi itakua indicator kuwa Mbowe anabeba tena uenyekiti
Golugwa sio Mangi ujue
 
Kamati Kuu ya CHADEMA, katika kikao chake kilichofanyika tarehe 14 Desemba 2024 jijini Dar es Salaam, ilitangaza uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kwa Kanda ya Kaskazini na Kati.

Uteuzi huo umefanywa kwa mujibu wa Katiba ya chama, ibara ya 7.7.16(s), ambayo inatoa jukumu kwa Kamati Kuu kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za Uenyekiti, Makamu Mwenyekiti, na Mtunza Hazina wa Kanda.
View attachment 3177312View attachment 3177313View attachment 3177314View attachment 3177315
Mungu baba Ibariki CHADEMA❤❤❤
 
kwani uchaguzi huu si unahusu kanda ya kaskazini kwa hiyo iwapo kama watachaguliwa watu wa huko ni kawaida maana hata kanda ya kusini au kanda nyingine waliochaguliwa ni watu toka kanda husika
Minja aneogombea kanda ya kati ni Mnyaturu ehe?
 
Mko vizuri hadi Minja amekuwa Mnyaturu
'Makupa', kwa kawaida huwa sina upumbavu wa kitoto. Nilicho jaribu kueleza kiko wazi. Ni wajibu wako kuelewa.
Sasa unapo niijia kwa njia hiyo unayo taka kunihusisha nayo, hapo itanilazimu nikukabiri kwa njia hiyo hiyo unayo taka wewe.
 
Kanda ya kati mgombea jina la kichaga, ama kweli hiki ni chama Cha wenyewe

..Devotha Minja emezaliwa na kukulia Morogoro.

..Hana tofauti na Mh.Abubakar Asenga Mbunge wa Ccm Kilombero.

..hana tofauti na Patrick Ole Sosopi ambaye amezaliwa na kukulia Iringa.

..kuna Watanzania wengi ambao wamezaliwa na kukulia maeneo tofauti na asili ya wazazi wao.
 
Kamati Kuu ya CHADEMA, katika kikao chake kilichofanyika tarehe 14 Desemba 2024 jijini Dar es Salaam, ilitangaza uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kwa Kanda ya Kaskazini na Kati.

Uteuzi huo umefanywa kwa mujibu wa Katiba ya chama, ibara ya 7.7.16(s), ambayo inatoa jukumu kwa Kamati Kuu kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za Uenyekiti, Makamu Mwenyekiti, na Mtunza Hazina wa Kanda.
View attachment 3177312View attachment 3177313View attachment 3177314View attachment 3177315
Lema kaamua kukaa pembeni, safi
 
Back
Top Bottom