Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 63,730
- 111,542
Mkuu umeongea mengi ya msingi Ila nikukosoe sehemu moja tu, hili taifa halijajigawa. Kama ilivyo mitazamo ya mambo mengine mitandaoni na hili lipo hivyo. Mfano mwaka 2016,2017 nilikuwa nje ya nchi kwa muda wa miezi mingi nilikuwa nikipitia humu naogopa, nilihisi Tanzania watu hawana hata 200 ya kunywa chai asubuhi kwa namna uchumi ulivyokuwa unaongelewa humu. Kila thread ni uchumi unayumba, uchumi unayumba.Wengine njaa,njaa mpaka Lissu naye kuingiza siasa kwenye njaa.Niliporudi nikashangaa mambo tofauti kabisa, mtaani ni picha tofauti na ya humu JF. Hivyo hivyo swala unalolisema la kuligawa Taifa, kwa mtu asiyekuwa nchini angepitia Jamii Forums akaona thread zenu za kuiombea mabaya Taifa Stars na LIKES kibao angesikitika Sana akihisi watanzania wamefikia hapa?, kumbe ni wanafiki wachache tu wa mitandaoni.Nimeenda Taifa huo umati wa watu na foleni za magari, uswahilini ndo usiseme na wachache waliotaka timu ifungwe ni sababu za kubet(Mikeka), wenyewe wanasema nimeiua Taifa Stars point zilikuwa nyingi, wala hawana time na siasa zenu. Nimegundua ndo maana mmejazana humu kudanganyana eti watu wanamchukia JPM na serikali hii, mwakani mtashangazwa Sana msipobadilika. Watu sio wajinga kuzungusha tena mikono.
Kwa taarifa yako hao watu wameenda uwanjani sio kwa hiyo hamasa ambayo unadhani imeletwa na hao wanasiasa. Hata simba na Yanga watu huwa wanajaa nao wamepewa hamasa na mwanasiasa gani? Huwa tunajazana kuangalia mechi za Ulaya na huwa gumzo kila mahali, nayo ni mwanasiasa gani aliwahamasisha?
Huko Sudan leo wanaandamana, unadhani hawana hata hela ya kunywa hiyo chai? Libya walimtoa Gaddafi, unadhani walikosa hela ya chakula? Kwa taarifa yako waliotoa likes sio kwamba hawapendi mpira bali walitoa baada ya kuona nuksi inaingizwa kwenye timu ya taifa na wanasiasa uchwara na ujumbe umefika.
Sio tunejazana humu kusema watu wanamchukia JPM, huku ndio sehemu pekee unayoweza kusema hivyo, jaribu kusemea hayo huko hadharani uone nini kitakukuta. Udhibitisho wa hilo ni juzi wakati wa mjadala wa amani alichosema Mzee Butiku kwamba kwa sasa taifa letu limekuwa la watu minong'ono, je ni kipi kimesababisha watu kuwa wanong'onaji?
Unasema mwakani watu tutashangazwa na ushindi, hakuna atakayeshangazwa kwani tunajua haheshimu box la kura. Zaidi ya nusu ya matokeo yatakuwa ni ya kupika ili kufikia haya unayoyasema. Kikubwa na kutaka kujua watu hawaridhishwi utaona idadi ndogo ya wapiga kura itakayojitokeza kama ushahidi wa kwamba watu hawaridhiki. Nikurahisushie hapendwi bali anaogopwa kutokana na matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya wasiomkubali.