Uchaguzi 2020 CHADEMA yaitaka Tume ya Uchaguzi NEC kutoa Ufafanuzi kuhusu Majina ya Wabunge wa Viti Maalum Wanaodaiwa wamepelekwa Bungeni

Uchaguzi 2020 CHADEMA yaitaka Tume ya Uchaguzi NEC kutoa Ufafanuzi kuhusu Majina ya Wabunge wa Viti Maalum Wanaodaiwa wamepelekwa Bungeni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufafanua kwa umma kupitia vyombo vya habari kuhusu kauli ya upotoshaji iliyotolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dkt. Wilson Mahera kupitia mojawapo ya magazeti ya Jumatatu, Novemba 9, 2020, kwamba majina ya Wabunge wa Viti Maalum wa Chadema yameshatangazwa na kuwasilishwa bungeni, wakati Kamati Kuu ya Chama haijafanya uteuzi wala kuwasilisha majina hayo kwa NEC kama taratibu zinavyoelekeza.

Kupitia barua hiyo ya tarehe 09/11/2020, yenye Kumb. Na. C/HQADM/20/TU/05/140, kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chama, Mhe. John Mnyika, kwenda kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, ikiwa na kichwa cha habari kisemacho, YAH; KAULI POTOFU YA NEC KUWA IMESHATANGAZA NA KUWASILISHA BUNGENI MAJINA 19 YA WABUNGE WA VITI MAALUM KUPITIA CHADEMA, Chadema imeitaka NEC kuheshimu na kuzingatia mamlaka ya uteuzi wa Wabunge na Madiwani wa Viti Maalum kwa mujibu wa Katiba ya Chadema Ibara ya 7.7.16(q) na (z) yako kwa Kamati Kuu ya Chama ambayo hadi sasa haijafanya uteuzi wowote wa nafasi hizo wala kuwasilisha majina kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

“Kauli hii ni potofu kwa kuwa Chadema (kupitia Katibu Mkuu ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kuwasilisha orodha ya majina ya wanaopendekezwa kuteuliwa kuwa wabunge), haijawasilisha orodha yoyote,” imesema sehemu ya barua hiyo ambayo pia nakala yake imepelekwa kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi.

Kupitia Gazeti la Nipashe, Toleo la Jumatatu, Novemba 9, 2020, ISSN 0856. Na. 0580394, katika habari iliyopewa uzito ukurasa wa kwanza, ikiwa na kichwa cha habari “NEC yatangaza viti maalum, Chadema yaambulia 19,” imeiandikwa kuwa NEC imeweka wazi idadi ya Wabunge wa Viti Maalum huku, Mkurugenzi wa Uchaguzi Dkt. Mahera akinukuliwa akitoa kauli ya upotoshaji kuwa waandishi wa habari wakiyataka majina hayo watayapata bungeni.

Imetolewa leo Jumatatu, Novemba 9, 2020 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Chadema
1604937145596.png

 
Kupeleka Wabunge Wa Viti maalum ni kuchochea mgogoro ndani ya Chama na kuipaisha CCM ili bunge lionekane kuwa ni la vyama vingi wakati walisema kuwa Wapinzani ni wasaliti na wanachelewesha maendeleo ya nchi. Sisi wananchi tumetaka CCM iwe peke yake kama ilivyoomba kupitia mgombea wake wa Urais na Spika wa Bunge kuwa bunge lijalo hakuna mpinzani ndani ya bunge hilo . Sasa wanataka nini tena kama sio kuchochea hasira na vurugu ili wapate sababu ya kuua watu.?

Wabunge wa upinzani watasababisha nchi ikose maendeleo. Hao Wabunge wapinzani watakua ni Chambo cha kuhakikisha maeneo wanayotoka hayapatiwi maendeleo ili baadae Mwenye Funguo za Benki kuu aseme ni kwa sababu mliniletea Wabunge wa upinzani wanaopinga maendeleo kumbe bajeti yake haitishi kuhudumia wizara zote zaidi ya miundo mbinu tuu.

Nitawashangaa sana wapinzani watakaotumika kuzuia maendeleo ya baadhi ya maeneo. Tunataka maendeleo nchi nzima kwa usawa.

Na Kilimanjaro ambao mwanzo waliambiwa kuwa wasubiri kwanza ,awamu hii wameambiwa wataketewa maendeleo kwa masharti ya kuichagua CCM sasa msije mkawapelekea viti vyenu maalumu wakajikuta wananyimwa maendeleo waliyoahidiwa ikiwemo kupewa Jiji.

Mnyika na Mbowe Tafadhalini sana msije mkawanyima watanzania maendeleo kwa kuwateua Wabunge toka sehemu yoyote.

Wananchi wanataka maendeleo ndio maana wakawachagua Wabunge wa CCM nchi nzima.
Maendeleo yanahitaji Chama cha mapinduzi.
Hamkuelewa maana ya nenoa MAENDELEO HAYANA VYAMA.!!
Maana yake maendeleo hayahitaji vyama vingi.
Hakusema kuwa maendeleo hayana Chama ( Bali hayana vyama(wingi)).
Tafarini kwa kina kauli hiyo msije mkapeleka Wabunge wenu wa kuteuliwa mkawakosesha wananchi maendeleo.
 
Ba
Bado najiuliza kama wengi wanavyohoji humu, inakuwaje inakuwaje kukifuata fuata chadema wakati tayari mna wabunge wa kutosha kuongoza bunge pasi hofu?
Bawacha akina Mdee na Bulaya wamepeleka sasa mashabiki mnachezeshwa kama mazezetu!! Hahahahahahaha.
 
Back
Top Bottom