CHADEMA yashauri Katiba ifuatwe kuunda Serikali, Waziri Mkuu na Mawaziri waliopo hawakuapa mbele ya Rais wa sasa

Mkuu CHADEMA wapo kikatiba?
 
Yani hawa chadema wametumia vifungu vya sheria ambavyo Raisi akimaliza uchaguzi aapishwe hlf waziri mkuu, mawaziri na manaibu wajiuzuru ili kutengeneza serikali na baraza jipya na wamekwepesha vifungu halisi vya baada ya kifo cha Raisi / ugonjwa au utimamu wa akili unaopelekea Makamu wa raisi kuteuliwa ikiwa uchaguzi umepita .

Vifungu ambavyo havilazishi kuvunja baraza na kuunda baraza jipya.

Hii nchi kuendelea ni kazi sana.
 
Mkuu CHADEMA wapo kikatiba?
 
Mkuu CHADEMA wapo kikatiba?
 
Hili tukio la kufiwa na kiongozi mkuu (Rais) wa nchi ni jipya na geni kabisa na ukichanganya na namna au style lilivyotukia ndiyo inakuwa utata mtupu..

Inasemaekana kwa kuwa ni tukio ambalo katiba haijaliwekea utaratibu mahususi wa kulishughulikia, ilipelekea VP Samia Suluhu Hassani kubabaika kwa kiasi kikubwa...

Inasememekana aliogopa hata kutangaza kifo cha Rais. Hata alipopata ujasiri wa kutangaza akakosea kutangaza siku rasmi za maombolezo ya kitaifa kwa mujibu wa sheria. Badala ya 21 yeye akatangaza siku 14. Tunashukuru baada ya kupata utulivu alirekebisha...

Vivyo katika hili. Inawezekana bado ni ile hali ya kuweweseka tu inayowakabili...

Hili liko wazi sana. Ni lazima Rais mpya aunde serikali/baraza la mawaziri jipya litakalowajibika kwake moja kwa moja baada kula kiapo kwake. Hili lililopo limekufa pamoja na Rais wake...

Na kama Rais Samia Suluhu Hassani anataka kufanya kazi na kuwapenda hawahawa, basi atamke hivyo na kisha wafanye jambo moja tu muhimu, KULA KIAPO KIPYA KWA RAIS MPYA..

Na nchi hii inashangaza sana, maana ni kana kwamba haina Mwanasheria mkuu wa serikali ili kumshauri Rais vyema mambo yq kisheria na kikatiba...
 
Ni kweli katiba ifuatwe na kama samia anataka hao hao waendelee basi avunje baraza la mawaziri awateu tena wale wale na waape mbele yake...Hatuna shida na mtu sisi tuna shida na katiba maana akivunja katiba wazi wazi ni hatari.
 

Mbona unaficha hivyo vya juu? Au na ww umekaririshwa? Hayo masharti ni pale Rais kama kaenda nje ya nchi,anaumwa au kuna sababu nyingine ambazo zinapelekea kiti chake kulaliwa na mwingine kama VP kwa muda, hivyo atakayekalia icho kiti ndiye hawezi kufanya hayo, ila Huyu kashaapishwa ni Rais, halafu unasema hawezi badilisha waziri mkuu!, mnachekesha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…