Chalamila: Huwezi kukwepa kelele Dar es Salaam

Chalamila: Huwezi kukwepa kelele Dar es Salaam

Kama kasema hivyo kakosea sana kwa sababu inakuwaje starehe yake na walevi wenzake iwe kero kwa watu wengine wanaoishi maeneo jirani bila kujali kama kuna wagonjwa,watoto,wazee na hata wakati mwingine hutokea dharura ya misiba lakini wote hao wateseke eti tu kwa vile kuna washenzi wachache wanakunywa pombe!
Halafu kama yeye anapenda sana kulewa ndio anatakiwa arudi kwao huko akanywe ulanzi atakavyo sio kuwaambia wenye mji wao eti wahame,halafu nilikuwa namsapoti sana Rais lakini tayari ameanza kunitoka kabisa naona kile kilevi kiitwacho madaraka kimemzidi kwa sababu hata kilichomshawishi kumleta Dar sijui ni kipi au sijui kuja kuhamasisha ulevi na mikelele!
Kwani kelele za misikitini na makanisani hazikeri wengine?

Kumbuka walevi ndio wanaendesha nchi, unakerwa na mlipa kodi[emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sema viongozi wetu bana Sheria wanapitisha wenyewe zikianza kutekelezwa wanakuja mbio mbio kuzuia. Tukichekea huu uhuni wa viongozi kugomea Sheria/ kanuni ipo siku li mtu litakatalia madarakani na hamtakua na chakulifanya.

Hata akina kagame, museveni, Mugabe n.k msifikiri waliruka tu mpaka kubadili katiba/sheria no!
Kama alivyokuwa anataka jpm awe madarakani mpaka kifo chake tu.
 
Kasema leo, Dar ni jiji la biashara, wasiopenda kelele waende Dodoma, watu watafute pesa, wale bia, mziki mnene. Maana wanachangia maendeleo ya jiji.

==========

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewaomba Wakazi wa Mkoa wa Dar es salaam kufanya starehe ambazo hazitokuwa na makwazo huku akiongezeka kuwa Jiji la Dar es Salaam haliwezi kukwepa kelele wala kukwepa starehe.

Akiongea wakati wa Swahili Comedy Show iliyofanyika Swahili Exprience, Coco Beach Dar es salaam, amesema “Kikubwa Mimi kama RC naahidi kutoa ushirikiano wa kiulinzi lakini zaidi kufanya starehe ambazo hazitokuwa na makwazo kwasababu maana na tafsiri ya kelele bado ni jambo ambalo ni gumu kidogo, adhana ikipiga asubuhi asiye Muislamu atasema hizo ni kelele"

"Vyombo vya Kanisani vikipiga kwa nguvu asiye Mkristo atasema ni kelele, miziki ya Baa ikipigwa Mtu ambaye sio mnywa pombe atasema ni kelele, kwahiyo kuna mahali panahitaji busara kuhusu tafsiri sahihi ya kelele ili Muislamu, Mkristo wapate haki zao, mnywa pombe apate haki yake na asiye imani apate haki yake, kikubwa Dar es salaam huwezi kukwepa kilele, huwezi kwepa starehe"

View attachment 2638831
Sauti yoyote iwe muziki, mayowe au mtetemo unaozidi mawimbi mrudio (decibel) yasiyoathiri kiwambo cha sikio na mapigo ya moyo au utulivu wa akili kwa kutafakari mambo mengine ya maana yanayohitaji utulivu ni dB 80 na isizidi dB 85.
Kwa sheria ya Tanzania kelele inahesabika kama uchafuzi wa mazingira (environmental pollution). Inatakiwa wale wanaozalisha kelele ili kuwakinga wengine na madhara yake kiafya wanatakiwa kuweka vipoza mawimbi sauti ambavyo vinanunuliwa. Sheria zizingatiwe badala ya kuendekeza siasa kwa nia ya kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa wapiga kura wasiwachukie. ZINGATIENI SHERIA zilizopo au mzirejeree kwa marekebisho ili watawala waue wananchi wengi kwa kusababisha afya mgogoro.
 

Attachments

"Vyombo vya Kanisani vikipiga kwa nguvu asiye Mkristo atasema ni kelele, miziki ya Baa ikipigwa Mtu ambaye sio mnywa pombe atasema ni kelele, kwahiyo kuna mahali panahitaji busara kuhusu tafsiri sahihi ya kelele ili Muislamu, Mkristo wapate haki zao, mnywa pombe apate haki yake na asiye imani apate haki yake, kikubwa Dar es salaam huwezi kukwepa kilele, huwezi kwepa starehe"
Mpumbavu huyu, anapingana na sheria za nchi, hajitambui kuwa alikula kiapo
 
Ningemshauri ahamishie familia yake pemben ya kitambaa cheupe,boardroom n.k halafu ndio aje aongee hayo anayoongea ndio ataeleweka.
Zaid ya apo ni pumba tu na kutojali wengine.
 
Hii ndio Kauli aliyoitoa leo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dr. Chalamila kwa watu wote, kwamba Kunywa bia kimya kimya ni sawa na kunywa Juice.

Aliyeelewa atusaidie kufafanua ili tuanze kuchangia.
Aisee..
 
Ni Chalamila aliyezuia BUKOBA CLUB na Lake Hotel kuendesha shughuli za harusi kwa sababu zinampigia kelele akiwa kwenye kasri lake jirani na kumbi hizo.
Lakini baada ya kuamia Dar ameibuka na maoni tofauti.
Wanasiasa ni vigumu kuwaelewa.
Ndio maana anaweza kukwambia kwamba atakujengea daraja hata mahali ambapo hakuna mto,ukimwambia mbona hakuna mto anakwambia na mto nitauleta!.
Chalamila ni mtu wa porojo tu usimsikilize, kumbuka alivyosema ameongea na Jiwe kuwa yupo anachapa kazi.
Kumbe mtu keshatangulia mbele ya haki,
 
Hii ndio Kauli aliyoitoa leo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dr. Chalamila kwa watu wote, kwamba Kunywa bia kimya kimya ni sawa na kunywa Juice.

Aliyeelewa atusaidie kufafanua ili tuanze kuchangia.
Kwenye baa, kila mtu anapenda kuongea kwa sauti kubwa ili asikike. Na mara nyingi kadri idadi ya bia inavyozidi kuongezeka ndiyo sauti inavyozidi kupanda juu kwani karibu kila mnywaji hupenda kuongea na wengine wamsikie, matokeo yake kelele huwa nyingi sana sehemu hizo. Juice haina kilevi hivyo wanywaji sehemu hizo hawapaazi sauti zao kadri muda unavyokwenda. Kwa mantiki hiyo basi mara nyingi huwa pana ukimya maeneo yao.
 
Kasema leo, Dar ni jiji la biashara, wasiopenda kelele waende Dodoma, watu watafute pesa, wale bia, mziki mnene. Maana wanachangia maendeleo ya jiji.

==========

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewaomba Wakazi wa Mkoa wa Dar es salaam kufanya starehe ambazo hazitokuwa na makwazo huku akiongezeka kuwa Jiji la Dar es Salaam haliwezi kukwepa kelele wala kukwepa starehe.

Akiongea wakati wa Swahili Comedy Show iliyofanyika Swahili Exprience, Coco Beach Dar es salaam, amesema “Kikubwa Mimi kama RC naahidi kutoa ushirikiano wa kiulinzi lakini zaidi kufanya starehe ambazo hazitokuwa na makwazo kwasababu maana na tafsiri ya kelele bado ni jambo ambalo ni gumu kidogo, adhana ikipiga asubuhi asiye Muislamu atasema hizo ni kelele"

"Vyombo vya Kanisani vikipiga kwa nguvu asiye Mkristo atasema ni kelele, miziki ya Baa ikipigwa Mtu ambaye sio mnywa pombe atasema ni kelele, kwahiyo kuna mahali panahitaji busara kuhusu tafsiri sahihi ya kelele ili Muislamu, Mkristo wapate haki zao, mnywa pombe apate haki yake na asiye imani apate haki yake, kikubwa Dar es salaam huwezi kukwepa kilele, huwezi kwepa starehe"

View attachment 2638831
Kelele huwa zinapimwa kwa kutumia kiwango cha usikivu wa sikio la mtu ambacho "units" zake zinaitwa decibles (dB); zero dB ikiwa ndiyo kiwango cha juu kabisa cha sauti ambayo hata kiziwi anaweza ngalau akai-feel kwenye sikio lake. Bado Mh Mkuu wa Mkoa anahitaji ashauriwe katika hilo, tusimwache tu hewani.
 
Back
Top Bottom