Chalamila: Vibaka wafanywe 'skeleton' za maabara iwe fundisho kwa wengine

Chalamila: Vibaka wafanywe 'skeleton' za maabara iwe fundisho kwa wengine

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Ni Chalamila tena katika matamko yake kama vile amekatwa kichwa! Mchengerwa OR TAMISEMI tunasubiri neno lako hapo, huyu bwana hajui kama kuna sheria za kufuata?

====


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ameliagiza Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua kali watu wote wanaojihusisha na uporaji 'vibaka' katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo hususani vibaka wa Daraja la Selenda, ili iwe fundisho kwa wale wote wanaohatarisha amani na usalama jijini.

Chalamila amesema hayo mwishoni mwa juma alipoongoza zoezi la usafi kama maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam ikiwemo Daraja la Selenda, Soko la Kimataifa la Salamaki la Feri na maeneo mengine ikiwa ni maandalizi kuelekea Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika 'Mission 300' unaotarajiwa kufanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kuanzia Januari 27-28 mwaka huu.

Chalamila amesema, "Sasa, naagiza kibaka takayekamatwa, asipigwe wala kuuliwa, apelekwe maabara awe 'skeleton' mifupa ya kufundishia wengine ambao wataiga mfano kwamba wizi haustahili katika jiji la Dar, kwahiyo hilo ndio agizo langu, wakale kielelezo kizuri kwa watu wengine." amesisitiza RC huyo.
 
Siku kibaka akikuchoma bisi bisi shingo au kisu cha tumbo kisa tu kukuibia sim ndio utamuelewa Mkuu wa Mkoa. Jamaa yangu pale Sinza alipigwa nondo ya uso jamaa wakaondoka na sim na wallet japo amepona lakini paji la uso limebonyea mpaka leo.
Kuna namna ya kufikisha ujumbe bila kuonesha unahamasisha kuvunja sheria. Mfano yule aliesema POLISI WAWANYANG'ANYE SILAHA MAJAMBAZI. Hapo utajua silaha wananyang'anywa vipi.
 
Kwenye hili namuunga mkono RC vibaka wamekuwa makatili sana sasa kwanini wao wafanyiwe uungwana?
Huku uswahilini kwetu walimpiga mtu nondo ya kichwa lakini walipomsachi wamemkuta na shilingi 3,000 na kiberiti! Sasa kweli watu kama hao ni wa kuwaonea huruma?
 
Vibaka na majambazi ni watu wabaya sana inahitaji ukatili wa hali ya juu ku deal nao, tatizo watu wengine ambao hata sio vibaka wanaweza kupata madhara makubwa pia pale njia za ukatili zinapotumika.
 
Kwenye hili namuunga mkono RC vibaka wamekuwa makatili sana sasa kwanini wao wafanyiwe uungwana?
Huku uswahilini kwetu walimpiga mtu nondo ya kichwa lakini walipomsachi wamemkuta na shilingi 3,000 na kiberiti! Sasa kweli watu kama hao ni wa kuwaonea huruma?
Buku 3 na kiberiti tu mtu kapigwa nondo?
 
Back
Top Bottom