Chalamila yupo sahihi; kuna Bima ya elfu 40. Unajua Mkeo ni mjamzito, huna Pesa. Kata hata hiyo

Chalamila yupo sahihi; kuna Bima ya elfu 40. Unajua Mkeo ni mjamzito, huna Pesa. Kata hata hiyo

Wazeee wetu waliokua na uchumi average sana mama akiwa mjamzito wanakua na maandalizi mengi sana kuanzia fedha, usafiri, vyakula siku za awali za uzazi( ndizi, nyama mara nyingi wanachinja kuku kadhaaa baadae mbuzi) na wamama nao wanakua washajua ataenda na nani hospital na nani atamhudumia akishajifunguua

Hivyo ndivyo inavyotakiwa.
 
Kwema Wakuu!

Chalamila hapa nitamtaja kama Mhusika bila kuhusisha cheo chake. Ni aina ha watu ambao hawana breki za kuongea na watu wa aina hii mara nyingi huongeaga UKWELI mchungu ambao wakati mwingine huweza kuwaacha watu mdomo wazi.

Chalamila kadiri unavyompa nafasi na Muda WA kuongea ndivyo anavyoweza Kuropoka mambo ambayo ni magumu. Kwa Sisi tunaojua watu aina yake hatuwapagi nafasi Sana ya kuongea au kuwauliza maswali Tata ambayo yatamfanya ajichie.

Chalamila ni kama Kina Tundu Lisu. Tofauti Yao ni Moja. Mmoja anajua kujenga hoja wakati mwingine hawezi kujenga hoja ila wote wanaweza kuwa wanasema ukweli uleule wa Jambo lilelile.

Wasema ukweli mara nyingi hawanaga Staha. Hiyo huwafanya kuitwa roporopo.

Tukirudi kwenye hoja ya Chalamila kuhusu Wajawazito. Yupo sahihi Kabisa

Serikali sio kama imeweza Kabisa lakini angalau inajaribu kujitahidi Kusaidia watu hasa watu wa chini ingawaje zipo changamoto za kiutendaji na kifedha.

Kuna Bima ya CHF kama sijakosea ambayo kwa mwaka ni elfu 40,
Mambo inayotibu Bima hii ni Magonjwa ya kawaida yote.
Ujauzito
Ultrasound
X-ray
Kujifungua na Upasuaji mdogo
N.k.

Hivi mtu unajua Kabisa unaenda kuzaa mtoto au umembebesha Mimba Binti au Mkeo. Kwa nini usiweke angalau kwa siku elfu Moja Miatano kwa siku kisha mwisho wa mwezi wa Kwanza wa Ile Mimba ukate Bima ya elfu 40 kwaajili ya kumsaidia Mkeo au huyo uliyempa Mimba

Au kama umetelekezwa, sio sababu ya kukosa Bima ya elfu 40 kwa Sababusiku hizi Fursa za uzalishaji na kujipatia kipato ni Haki Sawa baina ya Mwanaume na mwanamke. Nikimaanisha huna haja ya kumtegemea Mumeo au mwanaume wakati Fursa zimetolewa Sawa.

Kata Bima ya elfu 40 kwaajili yako kama mwanamke mjamzito.

Na sio kulialia kumtafutia mtu Lawama kwa Jambo linalokuhusu mwenyewe ambalo umerahisishiwa.

Mambo ya huruma huruma, burebure ndio yanaharibu jamii.

Tunajua nchi yetu ni Maskini na jamii zetu nyingi ni Maskini ndio maana serikali kwa sehemu nayo imerahisisha kwa upande wao. Sasa mwaka mzima ushindwe Kutafuta elfu 40 ulipie Bima ati utake serikali ikuhudumie. Huo kama sio Ukengemaji ni nini?

Chukua Bima ya 40 Kisha andaa pesa ya kujifungulia ya dharura na ya uzazi
Hayo ndio majukumu yenyewe. Pumbavu.

Tupo kwa ajili ya wengi wenye kuhitaji msaada wanaoustahili

Tupo hapa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Ww na yy wote wapuuzi, inamana vifaa vipo? Au hyo bima ingeteremsha vifaa kutoka peponi?
 
Ulitaka aseme Kwa namna ipi kwa mtu ambaye hataki kuchangia pesa kwa Mtoto wake aliyetumboni ili azaliwe?
Au mwanamke ambaye hataki kuchangia mtoto wake azaliwe anataka azaliwe burebure
Namna nyingine inayofaa
kauli za "kama huwezi....fanya..." eg. mtu akwambie kama hutaki kupokea maoni anzisha JF yako, kama huna elfu10 ya hela ya twisheni kafungue shule yako umfundishe mwenyewe
elfu50 sawa ichangiwe tatizo RC kawasilisha hoja kwa maneno yasiyofaa
 
Mkuu ndio maana serikali imeweka elfu 40.
Hiyo gharama ni reasonable kwa Tanzania yetu lakini kuiondoa iwe bure Kabisa huo utakuwa Wehu.

Unajua kulima kibarua heka Moja Kwa sasa kijijini ni elfu 30-40

Mtu kuwa Maskini haimaanishi asiwajibike.

Kutowajibika kunaondoa UTU wa binadamu.

Na Sisi Watibeli Moja ya mambo tunayoyalinda ni Hilo la UTU. Kuwajibika, kufanya kazi, ili kuchangia, kuonyesha mchango wako kwenye jamii inayokuzunguka
Kwamba huduma bure ni wehu, hapana tunakuwa na ujinga fulani, ni kwamba haiwezekani ama shida nini

Heka moja elfu 30 mpaka 40, sawa tufanye 40, heka moja mtu mmoja anailima kwa siku ngapi, jiulize kwa siku kaingiza sh ngapi? Jiulize hiyo pesa inamtosha kwa chakula, mavazi na vitu vingine, serikali haijitambui, viongozi wabinafsi, kuna mataifa yanaweza sisi kwanini tushimdwe, kwa tanzania hii inawezekana, kifupi tu viongozi wetu ndio wabaya wetu, nimetembea nimeona kuna watanzania hawajimudu hata kwa hiyo 40 ya pamoja.
 
Kwamba huduma bure ni wehu, hapana tunakuwa na ujinga fulani, ni kwamba haiwezekani ama shida nini
Sisi wapenda Haki. Bure ni dhambi. Kitu chochote lazima ugharamike. Hiyo ni Moja.
Ndio maana Mungu Mkuu tunayemuabudu licha ya kuwa sio mhitaji lakini anatutaka tukienda kwake tusiende Mikono mitupu.
Kwa Sisi Watibeli, huo ni Wehu

Heka moja elfu 30 mpaka 40, sawa tufanye 40, heka moja mtu mmoja anailima kwa siku ngapi, jiulize kwa siku kaingiza sh ngapi? Jiulize hiyo pesa inamtosha kwa chakula, mavazi na vitu vingine, serikali haijitambui, viongozi wabinafsi, kuna mataifa yanaweza sisi kwanini tushimdwe, kwa tanzania hii inawezekana, kifupi tu viongozi wetu ndio wabaya wetu, nimetembea nimeona kuna watanzania hawajimudu hata kwa hiyo 40 ya pamoja.

Ubaya wa viongozi wetu unatokana na kushindwa kuwajenga watu wawe na minute ya kujitegemea(falsafa ya Nyerere)

Ingawaje Sera ya Elimu inataka watu wakimaliza shule waweze kuwa na uwezo wa kujitegemea. Ukishakuwa na uwezo wa kujitegemea huwezipendelea mambo ya burebure
 
Jamii yenyewe imefundishwa na serikali kuombaomba
Hakuna wa kulaumiwa hapa ila serikali
Wanapokea mpaka misaada ya vyoo na hata hivyo havidumu au havipo tu
Kila leo nchi masikini zinaomba misaada na wengi wanasema ooh watoto wanakufa mara magonjwa mengi yaani ni kulia lia tu
Ila mkipewa na kuhurumiwa hela zinapigwa na wachache
Tuache utani yaani leo hospital inakosa gloves?
Hiyo misaada inafanya nini?
Kuropoka kwake ni kawaida maana tunawajua wengi wa hivyo ila tunawapiga stop lakini huyu wa kumpiga stop ndio anaemdekeza
 
Shida watanzania wengi hawajui kitu kinaitwa savings yaani kuweka akiba ya pesa yako. Mfano mzuri watu wengi wanalalamika January ni ngumu ukiuliza sababu watakwambia ada ina maana kuanzia mwezi wa kumi hawakujua kama wanatakiwa walipe ada January? Laiti wangekuwa wanasave pesa zao kila mwezi pengine wangelipa ada kiurahisi na kukabiliana na matatizo madogomadogo.
Acheni kutoa majibu ya jumla. Kuna kipindi cha Radio Free Africa kinaitwa "Je Wajua" hurushwa kila J'pili saa nne. Jaribuni kusikiliza halafu mje hapa kutoa maoni yenu.
 
Namna nyingine inayofaa
kauli za "kama huwezi....fanya..." eg. mtu akwambie kama hutaki kupokea maoni anzisha JF yako, kama huna elfu10 ya hela ya twisheni kafungue shule yako umfundishe mwenyewe
elfu50 sawa ichangiwe tatizo RC kawasilisha hoja kwa maneno yasiyofaa

😂😂😂

Hiyo ndio Lugha inayogusa Mtima nyongo na kumfanya mtu aelewe kwa urahisi.
Huoni hapa tunajadili
Angesema unavyoshauri wewe Wala isingekuwa habari Wala tusingekuwa haa tunajadili
 
Jamii yenyewe imefundishwa na serikali kuombaomba
Hakuna wa kulaumiwa hapa ila serikali
Wanapokea mpaka misaada ya vyoo na hata hivyo havidumu au havipo tu
Kila leo nchi masikini zinaomba misaada na wengi wanasema ooh watoto wanakufa mara magonjwa mengi yaani ni kulia lia tu
Ila mkipewa na kuhurumiwa hela zinapigwa na wachache
Tuache utani yaani leo hospital inakosa gloves?
Hiyo misaada inafanya nini?
Kuropoka kwake ni kawaida maana tunawajua wengi wa hivyo ila tunawapiga stop lakini huyu wa kumpiga stop ndio anaemdekeza

Umeongea Jambo kubwa na muhimu

Kila mtu ombaomba
 
Acheni kutoa majibu ya jumla. Kuna kipindi cha Radio Free Africa kinaitwa "Je Wajua" hurushwa kila J'pili saa nne. Jaribuni kusikiliza halafu mje hapa kutoa maoni yenu.
Acha kuadvertise radio na vipindi vya watu. Toa hoja yako ueleweke.
 
Acheni kutoa majibu ya jumla. Kuna kipindi cha Radio Free Africa kinaitwa "Je Wajua" hurushwa kila J'pili saa nne. Jaribuni kusikiliza halafu mje hapa kutoa maoni yenu.

Mkuu wewe si umesikiliza. Jenga hoja zako
 
Kwa akili hizi tutapelekeshwa sana na watawala.

Ukipenda bure lazima upelekeshwe na wanasiasa

Wanasiasa hawapelekeshi watu wanaogharamia mambo Yao.

Niliwahi kusema hii nchi tukilipa Kodi Watanzania angalau asilimia 50 wananchi watakuwa na nguvu zaidi ya viongozi
 
Anaweza akawa sahihi lakini lugha aliyoitumia kama kiongozi sio sahihi......

Lakini pia watu tumetofautiana vipato kwa wengine buku ni hela ya sigara na kwa wengine buku ni hela ya mboga......

Kiongozi ni wa watu wote.... masikini na matajiri.....kauli zake ziwe kwenye kujenga na sio kuzua taharuki
 
Watu wanataka bure tu kila kitu!
Yani hata wakipeana mimba kwa starehe zao wanataka serikali iwahudumie bure!
Tatizo sisi tunaoishi uswahilini hakuna mtu anatuelimisha kuhusu bima hiyo. Ni kweli bima hiyo IPO na inafanyakazi hosp zote za serikali nchi nchi mzima kasoro national referral hosp kama muhimbili.

Mimi nimeona faida ya hiyo bima hawana tatizo nayo popote penye government hosp au kituo cha afya.

Tunaomba kuwepo na juhudi za makisudi za serikali kutoa elimu umuhimu wa bima hii.

Temeke wakiwaweka watu wao ambao w alikuwa wanafuatilia na kukatia watu lakini sikuizi sijui nini kimetokea hawaonekani pale mpaka uende ofisi za manispaa
 
Kwema Wakuu!

Chalamila hapa nitamtaja kama Mhusika bila kuhusisha cheo chake. Ni aina ha watu ambao hawana breki za kuongea na watu wa aina hii mara nyingi huongeaga UKWELI mchungu ambao wakati mwingine huweza kuwaacha watu mdomo wazi.

Chalamila kadiri unavyompa nafasi na Muda WA kuongea ndivyo anavyoweza Kuropoka mambo ambayo ni magumu. Kwa Sisi tunaojua watu aina yake hatuwapagi nafasi Sana ya kuongea au kuwauliza maswali Tata ambayo yatamfanya ajichie.

Chalamila ni kama Kina Tundu Lisu. Tofauti Yao ni Moja. Mmoja anajua kujenga hoja wakati mwingine hawezi kujenga hoja ila wote wanaweza kuwa wanasema ukweli uleule wa Jambo lilelile.

Wasema ukweli mara nyingi hawanaga Staha. Hiyo huwafanya kuitwa roporopo.

Tukirudi kwenye hoja ya Chalamila kuhusu Wajawazito. Yupo sahihi Kabisa

Serikali sio kama imeweza Kabisa lakini angalau inajaribu kujitahidi Kusaidia watu hasa watu wa chini ingawaje zipo changamoto za kiutendaji na kifedha.

Kuna Bima ya CHF kama sijakosea ambayo kwa mwaka ni elfu 40,
Mambo inayotibu Bima hii ni Magonjwa ya kawaida yote.
Ujauzito
Ultrasound
X-ray
Kujifungua na Upasuaji mdogo
N.k.

Hivi mtu unajua Kabisa unaenda kuzaa mtoto au umembebesha Mimba Binti au Mkeo. Kwa nini usiweke angalau kwa siku elfu Moja Miatano kwa siku kisha mwisho wa mwezi wa Kwanza wa Ile Mimba ukate Bima ya elfu 40 kwaajili ya kumsaidia Mkeo au huyo uliyempa Mimba

Au kama umetelekezwa, sio sababu ya kukosa Bima ya elfu 40 kwa Sababusiku hizi Fursa za uzalishaji na kujipatia kipato ni Haki Sawa baina ya Mwanaume na mwanamke. Nikimaanisha huna haja ya kumtegemea Mumeo au mwanaume wakati Fursa zimetolewa Sawa.

Kata Bima ya elfu 40 kwaajili yako kama mwanamke mjamzito.

Na sio kulialia kumtafutia mtu Lawama kwa Jambo linalokuhusu mwenyewe ambalo umerahisishiwa.

Mambo ya huruma huruma, burebure ndio yanaharibu jamii.

Tunajua nchi yetu ni Maskini na jamii zetu nyingi ni Maskini ndio maana serikali kwa sehemu nayo imerahisisha kwa upande wao. Sasa mwaka mzima ushindwe Kutafuta elfu 40 ulipie Bima ati utake serikali ikuhudumie. Huo kama sio Ukengemaji ni nini?

Chukua Bima ya 40 Kisha andaa pesa ya kujifungulia ya dharura na ya uzazi
Hayo ndio majukumu yenyewe. Pumbavu.

Tupo kwa ajili ya wengi wenye kuhitaji msaada wanaoustahili

Tupo hapa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Haupo sawa kichwani hata kidogo. Na kama ndiyo watanzania baadhi mpo hivi basi ni laana kwa nchi. Hivi kweli wewe kwa akili Yako unaona ni sawa mtu anayehitaji huduma ya kiafya kuambiwa hatuna gloves? Hospital tena ya umma ambayo mwananchi anakatwa Kodi na kabebeshwa mzigo wa tozo. Tukisema chalamanda yupo sawa tunatoa taswira Gani katika sekta ya afya? Juzi kuna mama kafa kwa kung'atwa na nyoka wamekataa kumtibu Hadi atoe 150.000. wewe unaona ni sawa tu. Bila shaka wewe utakuwa ni baba yake shetani. Utakufa vibaya wewe.😭
 
Anaweza akawa sahihi lakini lugha aliyoitumia kama kiongozi sio sahihi......

Lakini pia watu tumetofautiana vipato kwa wengine buku ni hela ya sigara na kwa wengine buku ni hela ya mboga......

Kiongozi ni wa watu wote.... masikini na matajiri.....kauli zake ziwe kwenye kujenga na sio kuzua taharuki

Unaweza kuwa Sawa kabisa
Moja ya faida ya kauli za namna hiyo ni kufanya Jambo Fulani kuwa habari na kujadiliwa Jambo ambalo linaongeza uelewa, watu kujua nini chakufanya

Angeongea kawaida wala isingekuwa habari na tusingekuwa hapa.
 
Says a privileged keyboard warrior.
Ukipenda kuandikandika kwenye majukwaa, lazima ujue unahitajika kuwa mtafiti.

Ungelikuwa unajua umasikini uliopo kwa Watanzania wenzako, usingeizungumzia elfu arobaini kama jero.

Wewe na aliyeongea nyote mko sawa kwa sababu hamjui kina cha ufahamu wenu ni kifupi sana.
 
Hiyo ndio Lugha inayogusa Mtima nyongo na kumfanya mtu aelewe kwa urahisi.
Huoni hapa tunajadili
Angesema unavyoshauri wewe Wala isingekuwa habari Wala tusingekuwa haa tunajadili
hata hivo mentality ya BURE imeharibu wengi badala ya kutumia neno GHARAMA NAFUU wanatumia BURE sasa wakiambia watu changia inakuwa kelele, si unaona POTUS kajitoa kusaidia Africa imekua kilio kwasababu tumezoea bure/msaada badala ya kuchangia japo kidogo imagine leo waseme net za malaria ziuzwe elfu5 utasikia vilio wakati malaria anatuadhiri sisi wenyewe, kuchangia tunaona ni kuteswa. Why tumezoeshwa BURE!
 
Says a privileged keyboard warrior.
Ukipenda kuandikandika kwenye majukwaa, lazima ujue unahitajika kuwa mtafiti.

Ungelikuwa unajua umasikini uliopo kwa Watanzania wenzako, usingeizungumzia elfu arobaini kama jero.

Wewe na aliyeongea nyote mko sawa kwa sababu hamjui kina cha ufahamu wenu ni kifupi sana.
Mkuu sawa ni haki yenu kulalamika kwa kile alichokiongea RC ila usiniambie ya kuwa ndani ya miezi tisa umeshindwa kudunduliza hadi ifike 50,000 hata kama ni umasikini ila hii imezidi.
Mimba inakuja na vikwazo vingi kuweka pesa kidogo kidogo ni muhimu.
 
Back
Top Bottom