Chalamila yupo sahihi; kuna Bima ya elfu 40. Unajua Mkeo ni mjamzito, huna Pesa. Kata hata hiyo

Chalamila yupo sahihi; kuna Bima ya elfu 40. Unajua Mkeo ni mjamzito, huna Pesa. Kata hata hiyo

Kuna watu wanafanya kazi DSM mshahara wa siku ni elfu sita. Hata akijibana vipi lazima matumizi yawe makubwa kuliko kipato. Pia, kuna kundi la watu wasio na ajira. Wanaishi kwa kudura tu, wakipata wanakula wakikosa wanalala.
Mkuu hiyo 6000.kwa siku ukijibana vizuri kuna akiba inabaki labda uendekeza milo mitatu na soda. Na hao ambao hawana ajira wameshindwa kupata hata mtaji wa kufanya biashara au ndo hela za boom walikuwa wanazila zote?
Wanafahamu kuwa maisha yao ni magumu na watoto watateseka lakini hawawezi kuacha kuzaliana.

Kwanza, wana imani kuwa kila mtoto huja na sahani yake.
Pili, raha pekee ya masikini ni ngono.
Tatu, kuzaliana ni ASILI. Haijalishi kiumbe hai yuko katika mazingira gani, akipata nafasi ya kuzaa atazaa tu. Ndiyo maana licha ya mabomu ya Gaza lakini watoto wanazaliwa kila leo.
Mkuu sasa huku ni kuendekeza ngono. Sawa tuseme ndo starehe yao wameshindwa kutumia hata kondomu.ambazo ni bure?
 
Ndiyo maana nimekuambia inaonyesha wewe umekulia kwenye rough environment. Hakuna ustaarabu bali mmezoea kupayukiana!

Mimi nimezoea kumjibu mtu vile atakavyokuja.

Kum-treat mtu vile anavyojilengesha kwangu.

Sasa mtu akikuuliza swali la kijinga unataka utumie Busara kumjibu?
 
Kuwa na bima haikufanyi hizo gloves ziwepo hospital kwenye hospital za serikali 90% dawa ni kununua hata uwe na bima kiasi Gani Kuna muda unaenda unaambiwa hata kipimo Cha maralia hakipo vimeisha😭😭

Nadhani Huwa huendi government wewe
 
1737089115728.jpg
 
Kwema Wakuu!

Chalamila hapa nitamtaja kama Mhusika bila kuhusisha cheo chake. Ni aina ha watu ambao hawana breki za kuongea na watu wa aina hii mara nyingi huongeaga UKWELI mchungu ambao wakati mwingine huweza kuwaacha watu mdomo wazi.

Chalamila kadiri unavyompa nafasi na Muda WA kuongea ndivyo anavyoweza Kuropoka mambo ambayo ni magumu. Kwa Sisi tunaojua watu aina yake hatuwapagi nafasi Sana ya kuongea au kuwauliza maswali Tata ambayo yatamfanya ajichie.

Chalamila ni kama Kina Tundu Lisu. Tofauti Yao ni Moja. Mmoja anajua kujenga hoja wakati mwingine hawezi kujenga hoja ila wote wanaweza kuwa wanasema ukweli uleule wa Jambo lilelile.

Wasema ukweli mara nyingi hawanaga Staha. Hiyo huwafanya kuitwa roporopo.

Tukirudi kwenye hoja ya Chalamila kuhusu Wajawazito. Yupo sahihi Kabisa

Serikali sio kama imeweza Kabisa lakini angalau inajaribu kujitahidi Kusaidia watu hasa watu wa chini ingawaje zipo changamoto za kiutendaji na kifedha.

Kuna Bima ya CHF kama sijakosea ambayo kwa mwaka ni elfu 40,
Mambo inayotibu Bima hii ni Magonjwa ya kawaida yote.
Ujauzito
Ultrasound
X-ray
Kujifungua na Upasuaji mdogo
N.k.

Hivi mtu unajua Kabisa unaenda kuzaa mtoto au umembebesha Mimba Binti au Mkeo. Kwa nini usiweke angalau kwa siku elfu Moja Miatano kwa siku kisha mwisho wa mwezi wa Kwanza wa Ile Mimba ukate Bima ya elfu 40 kwaajili ya kumsaidia Mkeo au huyo uliyempa Mimba

Au kama umetelekezwa, sio sababu ya kukosa Bima ya elfu 40 kwa Sababusiku hizi Fursa za uzalishaji na kujipatia kipato ni Haki Sawa baina ya Mwanaume na mwanamke. Nikimaanisha huna haja ya kumtegemea Mumeo au mwanaume wakati Fursa zimetolewa Sawa.

Kata Bima ya elfu 40 kwaajili yako kama mwanamke mjamzito.

Na sio kulialia kumtafutia mtu Lawama kwa Jambo linalokuhusu mwenyewe ambalo umerahisishiwa.

Mambo ya huruma huruma, burebure ndio yanaharibu jamii.

Tunajua nchi yetu ni Maskini na jamii zetu nyingi ni Maskini ndio maana serikali kwa sehemu nayo imerahisisha kwa upande wao. Sasa mwaka mzima ushindwe Kutafuta elfu 40 ulipie Bima ati utake serikali ikuhudumie. Huo kama sio Ukengemaji ni nini?

Chukua Bima ya 40 Kisha andaa pesa ya kujifungulia ya dharura na ya uzazi
Hayo ndio majukumu yenyewe. Pumbavu.

Tupo kwa ajili ya wengi wenye kuhitaji msaada wanaoustahili

Tupo hapa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Maskini wa tanzania wanajifariji kwa kuzaa watoto wengi ambao hawana uwezo wa kuwahudumia
 
Kata Bima ya elfu 40 kwaajili yako kama mwanamke mjamzito.
Kuna huduma ukienda na hako kabima kako hupati ng'o ni kabima kasicho na thamani hospitalini ni kabima ka kupata get pass ya kumuona daktari na kuandikiwa dawa za bei rahisi mno na kukiwa na vipimo vikubwa utaambiwa ulipie tu maana bima yako hairuhusu wewe kupata hio huduma dawa za bei juu huwezi kupata kwa hio bima mfano dawa za kuanzia 100,000/= na kuendelea hupati kwa hio bima lazima uambiwe ulipie tu
 
Mkuu hiyo 6000.kwa siku ukijibana vizuri kuna akiba inabaki labda uendekeza milo mitatu na soda. Na hao ambao hawana ajira wameshindwa kupata hata mtaji wa kufanya biashara au ndo hela za boom walikuwa wanazila zote?
Mkuu sasa huku ni kuendekeza ngono. Sawa tuseme ndo starehe yao wameshindwa kutumia hata kondomu.ambazo ni bure?
Kama ilivyo kwa kondomu kuwa bure, ndivyo na gloves ziwe bure.
Watu hawajaomba chakula, wameomba gloves za bure!
___
Kuhusu ujira wa 6,000 kwa siku, hebu jaribu kufanya uchanganuzi.
Nauli, chakula, familia, kodi, mavazi, dharura na kila kitu halafu niambie kwa siku una-save ngapi.
 
Ndio maana kuna Bima Mkuu.
Kata Bima ili kujihami na hizo circumstances
Bob, kuna kaya hawawezi kupata Tsh. 30,000 ya pamoja ili kupata hizo bima za CHF.
Ili kupata hicho kiasi kwa pamoja, itawabidi wasile ama wasinunue hata mafuta ya taa kwa mwezi mzima.

Nenda Singida, Dodoma na mikoa mingine mikame ambako chakula walichovuna huisha mwezi Septemba kisha miezi mingi wanaishi kwa kubaingaza ndipo utajua 30,000 ni fedha nyingi sana kwa baadhi ya Watanzania.
 
Kuna huduma ukienda na hako kabima kako hupati ng'o ni kabima kasicho na thamani hospitalini ni kabima ka kupata get pass ya kumuona daktari na kuandikiwa dawa za bei rahisi mno na kukiwa na vipimo vikubwa utaambiwa ulipie tu maana bima yako hairuhusu wewe kupata hio huduma dawa za bei juu huwezi kupata kwa hio bima mfano dawa za kuanzia 100,000/= na kuendelea hupati kwa hio bima lazima uambiwe ulipie tu

Ndio maana nikaorodhesha utanufaika na nini kwenye hiyo Bima.

Ultrasound bila Bima serikali ni Tsh 15,000 - 25,000 kutegemeana na hospital.
Lakini ukiwa na Bima ya Tsh 40k hutoi Pesa.

Kujifungua kwa OP serikali ni Tsh 150,000 - 300,000 serikalini ukiwa huna bima.
Ila ukiwa na Bima ya 40k hutoi Pesa yoyote.

Kulala usiku Mmoja kwenye vitanda vya hospital za serikali ukiwa huna bima, Tsh 10,000 to 20,000. Lakini ukiwa na Bima ya 40k hutoi hata Buku.

Hiyo Bima ya 40k ni ya watu wa kipato cha chini Sana ili nao Wapate matibabu.

Imesaidia wengi.

Hiyo Bima ya 40k
Unapima Magonjwa yafuatayo;
UTI
Malaria
Taifodi
Na Magonjwa yote ya bacteria.

Kama haitoshi, unaweza kucheki full blood picture

Sasa wewe unataka nini zaidi?

Magonjwa makubwa hata hizo Bima za Milioni Moja hayatibu.
 
Bob, kuna kaya hawawezi kupata Tsh. 30,000 ya pamoja ili kupata hizo bima za CHF.
Ili kupata hicho kiasi kwa pamoja, itawabidi wasile ama wasinunue hata mafuta ya taa kwa mwezi mzima.

Nenda Singida, Dodoma na mikoa mingine mikame ambako chakula walichovuna huisha mwezi Septemba kisha miezi mingi wanaishi kwa kubaingaza ndipo utajua 30,000 ni fedha nyingi sana kwa baadhi ya Watanzania.

Nakuhakikishia hizohizo Kaya zinapeleka zaidi ya Laki kwa waganga wa kienyeji. Ushahidi huo ninao.

Mtu hospitalini anasema gharama. Ni kweli kwa sababu si Hana Bima.
Lakini mtu huyohuyo anaenda kwa sangoma anaambiwa atoe Laki tatu na anatoa.
 
Nakuhakikishia hizohizo Kaya zinapeleka zaidi ya Laki kwa waganga wa kienyeji. Ushahidi huo ninao.

Mtu hospitalini anasema gharama. Ni kweli kwa sababu si Hana Bima.
Lakini mtu huyohuyo anaenda kwa sangoma anaambiwa atoe Laki tatu na anatoa.
Hizo familia zipo, na zipo ambazo haziendi kwa waganga na hazina kitu.
 
Kama ilivyo kwa kondomu kuwa bure, ndivyo na gloves ziwe bure.
Watu hawajaomba chakula, wameomba gloves za bure!
___
Kuhusu ujira wa 6,000 kwa siku, hebu jaribu kufanya uchanganuzi.
Nauli, chakula, familia, kodi, mavazi, dharura na kila kitu halafu niambie kwa siku una-save ngapi.
Mkuu kwenye hiyo 6000 ningetumia 2000 kwaajili ya chakula kila siku. Hapo kwa siku nasave 4000. Mwezi unasiku 30 hivyo basi 4000×30=120,000. Mkuu hiyo 120,000 inatosha kwakodi(let's say kwa mwezi unalipa 60,000) hapo inabaki 60,000 ambayo inatosha kwa mavazi na nauli kama ukiitumia kwa makini na akiba inabaki.
 
Mkuu kwenye hiyo 6000 ningetumia 2000 kwaajili ya chakula kila siku. Hapo kwa siku nasave 4000. Mwezi unasiku 30 hivyo basi 4000×30=120,000. Mkuu hiyo 120,000 inatosha kwakodi(let's say kwa mwezi unalipa 60,000) hapo inabaki 60,000 ambayo inatosha kwa mavazi na nauli kama ukiitumia kwa makini na akiba inabaki.
Nimefurahi kusoma maoni yako, mdogo wangu.
Nikutakie usiku mwema.
 
Back
Top Bottom