Chalinze: Mtoto ajinyonga baada ya kukatazwa na mama yake asiende kwenye Kigodoro

Chalinze: Mtoto ajinyonga baada ya kukatazwa na mama yake asiende kwenye Kigodoro

Mtoto aliyejulikana kwa jina la Dotto mwenye miaka 10 mkazi wa kijiji cha Chalinze Mzee wilaya ya Chalinze amekutwa amejinyonga usiku wa kuamkia leo.

Imeelezwa kuwa amejinyonga baada ya kukatazwa na mama yake mzazi asiende kwenye muziki (kigodoro).

Copied from EATV
 
Hii ni moja ya sababu watu wa pwani tunapigwa sana gap la kielimu na watu wa bara, vigodoro ,midundiko, vanga tunaiabudu sana aisee.

Zamani ilikuw mtoto haonekani shule miezi minne kumbe kawekwa mwali ndani....

Watoto kama hawa wanaishi na mentality hiyohiyo ya kuabudu vigodoro mpaka ukubwani
 
Chalinze Mzee! Ni hapo ukitoka Chalinze center just a few meters towards Segera.
 
IMG_20230304_231210.jpg
IMG_20230304_231210.jpg
Si ndiyo hawa!!!, ukute na yeye alitaka shuhudia haya.
 
VITU VINAVYOATHIRI MALEZI NA TABIA MBOVU ZA WATOTO KULIKO UMRI WAO.

❌ Tamaduni na ngoma za hovyo zisizo na maadili kama vigodoro na singili.

❌ Nyimbo za Taarabu zinachangia asilimia kubwa kujaribu maadili ya watoto wa pwani , na ukimuona mwanao wa kiume anapenda kuimba au kwenda kwenye matamasha ya nyimbo hizo, Anza kumtilia mashaka

❌ Nyumba yenye vyumba vichache ambapo watoto husikia faragha za wazazi .

❌ Baadhi ya wazazi / wakubwa hasa wa kike kupenda kuweka vikao vya majungu, kuongea mbo mazito ya mahusiano, michepuko Yao na mbinu za kumbana/ kumchuna mwanaume bila kujali kuwa watoto wapo na wanakariri neno kwa neno.

❌ Tamthilia zinazoonyeshwa kwenye Tv masaa 24 wanawake wenye nyumba/ wadada wa kazi na wanawake in general wanaziangalia masaa 24, tena wapo na watoto wanaofurahia na kuchangiwa kinachoendelea. Tamthilia hizo Zina theme nyingi za mapenzi na mahusiano.

❌ Mahubiri kwenye nyumba za ibada wale ambao hawatengi ibada za watoto Bali wote huchanganyikana. Sasa, asilimia kubwa ya mahubiri Yao ni mapenzi na mahusiano. Wanaongea mambo mazito ama wanapo kemea tabia Fulani au wanapomasisha mahusiano, wakati wanaongea hayo watoto wadogo wapo.

❌ Wakitoka hapo wanaokwenda kufanyia utafiti waliyoyasikia na hapo wanakwenda kuwa influence wenzao ambao hawajui chochote na hivyo kujaribu maadili ya jamii nzima
 
Hii ni moja ya sababu watu wa pwani tunapigwa sana gap la kielimu na watu wa bara, vigodoro ,midundiko, vanga tunaiabudu sana aisee.

Zamani ilikuw mtoto haonekani shule miezi minne kumbe kawekwa mwali ndani....

Watoto kama hawa wanaishi na mentality hiyohiyo ya kuabudu vigodoro mpaka ukubwani
Kila Jamii ina udhaifu wake

kuna Jamii huko kwenu imani za kishirikina zimewakaa hadi wakiwa wakubwa kila failures kwny maisha wanasingizia mabibi wenye macho mekundu

huko maporini kwenu nyie si ndio mnashawishi watoto wajifelishe mitihani ili wasiende Sekondari ?
 
Back
Top Bottom