Chama cha wasio waislam wala wakristo kinahitajika

Naunga mkono hoja namimi ntakua mjumbe
 


  1. Surah Al-Imran (3:19):
    • "Hakika Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu..."
    • Aya hii inaeleza kwamba dini inayokubalika mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.
  2. Surah Al-Imran (3:85):
    • "Na anayefuata dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake, na huko Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara."
    • Hii inaonyesha kwamba kufuata dini nyingine kando na Uislamu hakutakubaliwa na mtu huyo atakuwa miongoni mwa wenye hasara katika Akhera.
  3. Surah Al-Ma'idah (5:3):
    • "...Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekupendeleeni Uislamu uwe Dini yenu..."
    • Hii inaeleza kuwa Uislamu ni dini iliyokamilishwa na Mwenyezi Mungu na kupendekezwa kwa watu kama njia yao ya kuishi.
  4. Surah Al-Baqarah (2:256):
    • "Hapana kulazimisha katika Dini. Uongofu umekwisha pambanuka na upotovu..."
    • Aya hii inaonyesha kwamba hakuna kulazimisha mtu kuingia katika Uislamu, lakini uongofu (dini ya haki) imekuwa wazi na dhahiri.
  5. Surah Al-Hujurat (49:13):
    • "Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanaume na mwanamke, na tumekufanyeni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika ahishimikae zaidi kati yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni huyo amchaye Mwenyezi Mungu zaidi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye khabari."
    • Aya hii inaeleza umoja wa wanadamu na kwamba heshima ya kweli mbele ya Mungu inatokana na uchamungu na siyo dini, ingawa kwa Waislamu uchamungu unamaanisha kufuata Uislamu.
 
Ashampoo...
Nakuomba ruhusa uniruhusu mimi Muislam nichangie.

Pili uzoefu unaonyesha kuwa wengi wanaojiita Wapagani kabla walikuwa Wakristo.

Huwezi kumpata Muislam aliyemwamini Mungu akakengeuka na kumkana Allah.

Hakuna.
Salman Rushdie
Ayaan Hirsi Ali
Abu Bakr al-Razi
Abu al-Alaa al-Maarri
 
Nakushauri mada kama hizi uwe unakaa kimya,nenda kawarubuni wapumbafu na wajinga wenzio katika imani yao.

Kwa taarifa yako hakuna musilamu kamail tz wengi ji wapangani tu na makafiri wanaoenda kusali ilkwa sababau ya hofu ya kifo na uongo mwingi malio wajaza vichwani mwao kuhusu dhabu ya kaburi,kitu ambacho ni uongo mtupu,

Dini zote ni utumwa wa kifikra kama ulivyo wewe.

Dini imekua chanzo cha utengano baina ya jamii,kama ambavyo unajitahidi kufanya kazi hii ya kuwatenga watanzania kwa minajili ya dini zao.

Kaa kimya mzee huna hoja katika hili.
 
ofcourse ni ruksa na ni jambo jema nyie mnaoamini / wenye mawazo yanayofanana kukutana na kubadilishana mawazo ingawa nadhani umeweka kwenye jukwaa la siasa kimakosa sababu hiki chama chenu kitakuwa sio cha kisiasa sababu mkiwa ni chama cha kisiasa mkapata uongozi mtakinzana na dhana ya kwamba Serikali yetu haina dini wala haitengi dini wala haiitaji kujua imani zenu..

 
Sio kweli....

Pagan ni neno lililotumiwa na wakristo wa mwanzoni mwa karne ya 4, lilitumika kuwaita Warumi ambao walikuwa wanaabudu Mungu zaidi ya mmoja (polytheism)

Nilikuwa nafikiria tu kama kitu kidogo kama hiki umeshindwa kukielewa, vipi kuhusu maswala complex kama uhuru wa Tanganyika?

Tunaweza vipi kujihakikishia kuhusu uhalali wa makala zako za historia ya uhuru kuwa ni reliable na sio kwamba ni mwendelezo ule ule wa tatizo lako la kutokuelewa vizuri mambo?
 
Acha kumtisha wafua dini hii nchi wachachd sana wengi ni wapumbafu tu waliojaa double standards
Usiwaponze wenzako, Wafia dini ndio wameishikilia na kuiongoza nchi hii kila sekta, suala la double standards ni mjadala mwingine.
 
Scars...
Mimi sipendi kubishana.
Hupenda kufanya mjadala ili nami nijifunze kwa wengine.

Si lazima uamini niandikayo.
Wewe ni mtu mmoja.

Nimeandika vitabu na paper nyingi.

Watu wengi wananisoma na kuniamini.
 
Kwanza kabisa, wasioamini Mungu si wapagani. Kuna wapagani wengi wanaamini Mungu.

Neno wapagani ni la kikoloni la kuwabagaza watu walioamini miungu tofauti na walioamini au kuijua wao, hususan Ukristo na Uislamu.

Hili neno ukilisema katika ulimwengu wa leo kwa kumuita atheist, mtu asiyeamini Mungu, unaonesha kutokuwa na elimu kwenye maneno ya mada hizi, pengine kwa sababu hazijaelezwa sana kwa Kiswahili.

Watu wanaoamini miungu ya dini za asili ni wapagani, na wanaamini Mungu. Atheist hawaamini Mungu kabisa, kwa hivyo, kuna tofauti kati ya atheists na wapagani.

Pili, habari yako kwamba wengi wa atheist ni waliokuwa Wakristo ni potofu. Hii Tanzania Atheist Society ipo tayari na kuna waliokuwa Waislamu wengi tu.

Nimekuwekea video ya mtu aliyekuwa Muislamu wa Zanzibar na baadaye kuwa atheist ametoa video wazi akiukataa Uislamu

Tatu, dini ikiwa na ujinga, watu wana haki ya kusema dini ina ujinga. Pinga hoja kwa hoja, si kwa logical fallacy ya "argument from authority" kwamba dini haiwezi kuwa na ujinga kwa sababu tu ni dini.

Cc Ashampoo burning
Your browser is not able to display this video.
 
Kuna Tanzania Atheist Society. Ila haijapata formal registration. Kuna umuhimu wa kuwa wawazi, angalau hiyo registratiin na intent iwe wazi, secret society haitasaidia sana na itaongeza persecution.
 
Kuna Tanzania Atheist Society. Ila haijapata formal registration. Kuna umuhimu wa kuwa wawazi, angalau hiyo registratiin na intent iwe wazi, secret society haitasaidia sana na itaongeza persecution.
Ipo wapi hiyo tuunge mkono
 
Scars...
Mimi sipendi kubishana.
Hupenda kufanya mjadala ili nami nijifunze kwa wengine.

Si lazima uamini niandikayo.
Wewe ni mtu mmoja.

Nimeandika vitabu na paper nyingi.

Watu wengi wananisoma na kuniamini.
Ukitaka kuepuka kubishiwa basi hakikisha kile ulichoandika kinakuwa ni cha kweli.

Na mtu mwenye busara akikosea hawezi kuita mabishano zile hoja zinazomsahihisha.

Mara nyingi watu wenye busara huchukua hiyo kama somo kwa kukiri makosa yao ili waongeze maarifa mapya.

Kwenye mjadala huwezi kuandika kitu ambacho ni cha uongo halafu ukazuia ukosoaji kwa kusema hutaki mabishano.

Ni kama tu wewe ulipomjibu mtoa mada kuwa hawezi kuzuia wasiokuwa na Atheist wachangie uzi wake, basi hivyo hivyo na wewe huwezi kuzuia wakosoaji wasikosoe pale unapokosea kwasababu tu hutaki mabishano.
 
Nikukumbushe kanisa limejenga shule nyingi kabla hata ya uhuru hata leo wana-shule nyingi
Unavyoouponda ukristo ukumbuke na hili
 
TANU chama cha waislamu
 
Mkuu kuna tofauti kubwa kati ya upagani na watu wasio amini uwepo wa Mungu na shetani.
 
Wasicho jua watu wengi nikwamba watazame vizuri watu wanao jiita wenye dini.
Matendo yao na maisha yao kwaujumla..ndipo utaamini kwamba nichui alie vaa ngozi ya kondoo..kwani matendo yao hayaendani namisingi mikuu ya dini zao.
Ipo,ipo,ipo,ipo siku mwanga utalishangaza giza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…