Chama changu CCM mkitaka tusiwe wapinzani groom Vijana wengi ila kwa sasa macho yenu yaweke kwa Vijana hawa

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
16,295
Reaction score
33,994
Chama changu cha Mapinduzi
Tukitaka kuendelea kuongoza nchi tubadili mbinu

Hakikisha hatuweki mtu anayetumia nguvu kubwa kijibrand badala ya kazi kumbrand, kuna Vijana ambao kwakweli tuwe wakweli wanapiga kazi na wanakubali wanapokosea, wako humble Kwa wananchi , na ni wasafi Narudia ni wasafi nataka mjue hivyo ni wasafi hawana harufu ya ufisadi

1. Innocent Bashungwa
Kijana mmoja smart Mtanashati asiye na makuu Mtenda haki dhidi ya wengine ambaye akipata nafasi za juu ndani ya serekali tutapata jembe moja zuri , is so humble na anakiri anapokosea, anafuatiliwa sana Jamaa hata juzi kwenye ajali ya ndege bukoba hotuba yake imejaa hekima kuliko siasa na ni mtu pekee alokiri makosa ya serikali.


2. Hussein Bashe
Mwamba wa AMKOS ameiwezesha wizara yake ya kilimo kufika mbali hata Kama bado kuna changamoto kadhaa ila tunaelewa shughuli yake CCM Hawa ndo watu wa kuwashika sana.



3. Anthony Mtaka
Nani asiyeelewa kazi ya mwamba huyu Jamaa anaweza kazi sana ni msafi hana Makubdi and he is so intelligent Kabisa na anajali sana kazi yake kuliko jambo lolote.



4. Steven Masele
Ana msimamo kwenye mambo ya msingi hayumbishwi hata kidogo na anatetea anachokiamini, ni mtendaji mzuri wa kazi tena sana.



5. Togolan Mavura
Kwa ambao hamjui Jamaa ndo masta plan wa shughuli nyingi serikali zinazoonekana kukwama na akihusishwa zinaenda huyu Balozi jembe sana na Kwa taarifa nilizopenyezewa yeye na mzee wa nzega,Mkata na Bashungwa ndo mama anawaangalia Kama watu wa kuwapa Majukumu mazito sana anaposhindwa.



6. Joanfaith Kataraihya (DED sehemu)
Haka kadada bwana kuna mtu alikataka kakakataa na ni mtu mzito tuachane na hayo twende kwenye kazi kamepiga kazi kuzidi Mkurugenzi yeyote wa Almashauri kuwai kutokea eneo alipo, tokea kaenda kuna mabadiriko makubwa sana sehemu anapoongoza, si mla rushwa ni mtiifu Kwa wananchi na anaelewa kazi




7.Steven Byabato
Kwa taarifa wengi hawajui bwana Makamba anazingua wizara hii hata hicho kidogo ni Kwa sababu ya mipango ya Bwana Mdogo huyu




Ombi Kwa CCM hizi ni hazina zitunzwe Lakin pili tunaomba tuwapate wengine wa aina hii ambao hata hatuwajui kuweza kuwa na timu ya kutosha hapo baadae

Kidumu Chama cha Mapinduzi

Britanicca
 
Sku bashe akichukua fomu ya kugombea uraisi mnistue
 
Kuwepo na uwanja sawa wa ushindani wa kisiasa ndio muweze kuwapima hao vijana wa CCM. Lakini katika mazingira ya mbeleko, wahuni ndio watajifanya wanafanya vizuri.
 
Kwa Mtaka sahihi kabisa. Ila kwa mnyambo chapa Inyambo no. Afadhali
1. Mtaka
2. Masele
3. Biteko japo ni bahima
4. Byabato.
 
Chawa mkuu kazini , yaani mtu anavuta hela kwa watu zaidi ya 10 kwa kazi ya uchawa tu ! Maisha kama ya Chuma ulete yaani !!
 
Nipe namba yake huyu mdada nimpongeze
 
Mbona hujawashauri waboreshe mbinu za kuiba kura?

CCM bila TumeCCM na PoliCCM mchana kweupe wanafutwa kwenye uso wa siasa za Tanzania.

CCM kinachofanya iendelee kuwepo ni hivyo bila kusahau mfumo mbovu wa elimu unaoaminisha watu kuhusu mafanikio ya vyeti na sio kujitambua.
 
Mavura alikua muandika hotuba wa JK nothing special zaidi ya hiko!!

Huyo Byabato kapita kwa kuiba kura hana hata mandate ya wananchi wake kivipi Tena ni asset?

Huyo DED naye anafanya branding kubwa Ili tu 2025 agombee ubunge maana ana nyuzi nyingi humu za kusifiwa kuliko kueleza utendaji kazi wake!!

Hapo Assets kidogo ni Bashe na Mtaka (Ingawa naye yupo exaggerated sana) wakati alipopelekwa jiji la Dodoma ame under perform badly.

CCM hakuna assets no wonder vijana wa upinzani wakihamia huko wanapewa top seats!!
 
Muongeze na SUPHIANI kwenye hiyo listi jamaa ni noma sana.
 
swadakta
 
Uzi wako wa kijinga kuliko ujinga wako nani kakuambia hao ndio wasafi??? Ccm wote kwa sasa hakuna wasafi wote hovyo na nani amekuambia hiii ni inchi ya Ccm tu?
 
Mkuuu Bashe ni mtu wa hovyo na u hovyo wake wa kiwango cha SGR
 
Ombi Kwa CCM hizi ni hazina zitunzwe Lakin pili tunaomba tuwapate wengine wa aina hii ambao hata hatuwajui kuweza kuwa na timu ya kutosha hapo baadae
Kwa bahati nzuri au mbaya hujawahi kusikia mtu aitwae 'Tax', au pengine vigezo vyako ni hafifu. Mtaka naunga mkono, hao wengine unajua mwenyewe.
 
Kuna kichwa kingine Balozi Mberwa Kairuki wa China.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…