Champions League last 16: Real Madrid kuivaa PSG; Chelsea kukipiga na Barcelona

Kumbe huwajui Liverpool...!
 
Hivi Barca huwa mnawaonaje.? Mbona kipindi ndio walikua moto na Messi ndio alikua balaa na tuliwapiga darajani tukaja kudraw Nou Camp tukaenda kuchukua mbele ya Bayern Munich.

Msitubeze bhana. Huu ni mpira
Kipindi kile kuna drogba bhana ,terry na Lampard na mlikuwa basi mnajua kuliweka kisawa sawa hadi Camp Nou hawajapata goli.Chelsea ya saivi inaenda kula nyingi huko UEFA.
 
kwa wapenzi wa epl chelsea anatoboa hapo naamini kabisa barca wenyewe hawawataki hao blues mpaka kesho mara mia wangepangiwa spurs
 
Haswaaa!!! 2012 tulibezwa sana kuanzia quarter final first leg tulivyoliwa 3-1 na Napoli, hadi 19/05 pale Allianz Arena tunafanya wonders watu hawakuamini
[emoji23] [emoji23]
Tena ile siku pale Alliaz Arena ilinifanya nikalala na viatu.
 
Chelsea wanagongewa nje kabisa asubuhi na mapema. Kwa kiwango chao kibovu watagongwa mpaka refa nae atashangaa.
 
Bila shaka msimu huu wahenga wa England naweza nikasema ni wakati wao. Timu zimeingia kwenye droo bila shaka mmojawapo ataambulia kuingia fainali na hatimaye kutwaa ubingwa kabisa. Ni historia nyingne ambapo ktk misimu kadhaa iliyopita waengland hao hawajawai kutamba mbele ya wababe Barcelona pamoja na real Madrid ambao ndo mabingwa wa msimu uliopita. Ni tabiri yangu kuwa the blues from Etihad chini ya kocha mwenye mbinu mingi watafanikiwa kutawaza mabingwa wa UEFA msimu huu. Katika michezo yote waliyocheza katika hatua ya mtoano wameonekana bora Mbele ya wapinzani wao waliokuwa wakicheza nao. Japokuwa mchezo wa mwisho waliangukia pua mbali kwamba wao haikuwaathiri chochote. Ni dua zangu kwa blues hao kutinga mnako fainali na hatimaye kutwaa kombe ktk msimu huu wa 2017/2018
 
Kocha mwenye mbinu mingi ambaye aliikuta bayern katika ubora wa hali ya juu na akashindwa kucheza fainali hata moja kwa muda wa miaka mitatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…