Changamoto ya Tofauti ya Umri Katika Mahusiano

Changamoto ya Tofauti ya Umri Katika Mahusiano

cold water

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2021
Posts
238
Reaction score
954
Naomba nianze kwa kujieleza,

Nitaelezea changamoto katika mahusiano ninayoyapitia, hasa upande wa tofauti ya umri. Mimi ni mwanamke, nimezaliwa mwaka 1993.

Mahusiano yangu ya kwanza yalikuwa na mwanaume aliyezaliwa mwaka 1992. Kama nilivyoeleza mwanzo, tulipishana mwaka mmoja tu, yeye akiwa mkubwa kwangu kwa mwaka mmoja. Hata hivyo, hatukudumu kwenye mahusiano yetu kutokana na tabia zetu kutowiana.

Sasa, baada ya kuachana naye, wanaume ninaowapata ni wale waliozaliwa mwaka 1998. Ninapata changamoto kubwa kuhusiana na suala la umri. Nashindwa hata kufikiria kubeba mimba kwa sababu nawaona wadogo kwangu, na pia ninaogopa kuchekwa na jamii inayonizunguka.

Hata hivyo, utakuta tunapendana vizuri, na tatizo pekee linakuwa umri. Naomba ushauri kwa sababu nina mtoto mmoja wa miaka kumi, na ninatamani kuanzisha familia nyingine. Umri unazidi kwenda, lakini wanaume ninaowapata naowapenda ni wadogo kwangu.

Sijabahatika kupata mwanaume wa umri mkubwa ambaye nitampenda. Si kwamba hawapo, lakini hawanivutii kabisa!
 
C Kwa ubaya lakii...
FB_IMG_1732536905823.jpg
 
1993 mpaka 2024 ni miaka 31 na hapo hujasema ukweli wako kwamba umezaliwa 1985.

Tuchukulie una miaka 31. Kwa umri huo unadhani Kuna mwanaume wa Miaka kuanzia 32 na kuendelea atakuwa anakuhitaji?

Usiseme unawapenda hao wa 98, sema ulikuwa unajishebedua sana.

Kubali matokeo
 
Upe furaha moyo wako, maneno husemwa na yataendelea kusemwa bila kujali your perfection kwa jamii unayoiogopa so as long as hauvunji sheria ya jamuhuri we endelea kufurahia maisha...
 
Dada yangu pole kwa changamoto kikubwa focus na mtu ambaye unajua utajenga naye future achana na mambo ya kuchekwa na jamii. Kuna umri ukifika rika moja mnakuwa sawa mfano mtu aliyezaliwa 1990 mpaka 1998 kwa Sasa ni rika moja maana hawapishani more than 10 years.

NB. 1 unaposema Kila unayempata unashindwa kubeba mimba kwa maana ni mdogo kwako unamaanisha Nini?
NB. 2 acha kuruhusu miwili wako kuwa sehemu ya majaribio kwa wanaume maana miwili wako ni hekalu la Mungu.
 
Dada yangu pole kwa changamoto kikubwa focus na mtu ambaye unajua utajenga naye future achana na mambo ya kuchekwa na jamii. Kuna umri ukifika rika moja mnakuwa sawa mfano mtu aliyezaliwa 1990 mpaka 1998 kwa Sasa ni rika moja maana hawapishani more than 10 years.

NB. 1 unaposema Kila unayempata unashindwa kubeba mimba kwa maana ni mdogo kwako unamaanisha Nini?
NB. 2 acha kuruhusu miwili wako kuwa sehemu ya majaribio kwa wanaume maana miwili wako ni hekalu la Mungu.
Kila anayempata ina maana ni wengi,yani huyu mpk aje kuolewa kashapitiwa na zaidi ya wanaume 100,halafu hiyo ndoa isipodumu atasema ana bahati mbaya kumbe anajitia mikosi ya kujitakia...
 
Hao unaowapata ni kwamba hawaendani na wewe au hawakupi pesa? Yule dereva malori alikuwa anakupa elfu 2 za vocha. Yule muarabu chotara kama saso alikuwa hakupi kabisa ila ulimpenda kisa rangi/handsome.
 
Miaka 31 halafu bado una mawenge na una mtoto!

Tatizo ni ubongo wako bado hujachangamka.

Hebu achana na maisha ya Instagram jitambua achana na maisha ya picha picha ndo maana unaona wazee Kama watakuharibia post zako.

Kumbuka una mtoto ambae babake hajakuoa sijui Kama unanielewa ..
 
Hii kusema madingilai wapo wanaokutaka ila huvutiwi nao unavutiwa na serengeti boy ni ngumu kumeza ila sio mbaya komaa na haohao wa 97 japo mtasumbuana sana huko mbele.

Kuna mdgo wangu wa buku mbili alikua na mke lika kama lako, wakaja kuachana kwa kutofautiana mitazamo. Umri kama wa mleta uzi wanataka familia na kutulia na kulea familia ya baba, mama na watoto. Na dogo yeye ni mchakalikaji, hakai sehemu moja full mishe mishe na ndoto kibao.

Mke anataka attention, anahisi dogo anacheat na madogo dgo wengine, lawama haziishi. Anataka mume alokua anamuota kua anaenda kazini, jioni anarudi kujumuika na familia 😆😆.
 
Naomba nianze kwa kujieleza,

Nitaelezea changamoto katika mahusiano ninayoyapitia, hasa upande wa tofauti ya umri. Mimi ni mwanamke, nimezaliwa mwaka 1993.

Mahusiano yangu ya kwanza yalikuwa na mwanaume aliyezaliwa mwaka 1992. Kama nilivyoeleza mwanzo, tulipishana mwaka mmoja tu, yeye akiwa mkubwa kwangu kwa mwaka mmoja. Hata hivyo, hatukudumu kwenye mahusiano yetu kutokana na tabia zetu kutowiana.

Sasa, baada ya kuachana naye, wanaume ninaowapata ni wale waliozaliwa mwaka 1998. Ninapata changamoto kubwa kuhusiana na suala la umri. Nashindwa hata kufikiria kubeba mimba kwa sababu nawaona wadogo kwangu, na pia ninaogopa kuchekwa na jamii inayonizunguka.

Hata hivyo, utakuta tunapendana vizuri, na tatizo pekee linakuwa umri. Naomba ushauri kwa sababu nina mtoto mmoja wa miaka kumi, na ninatamani kuanzisha familia nyingine. Umri unazidi kwenda, lakini wanaume ninaowapata naowapenda ni wadogo kwangu.

Sijabahatika kupata mwanaume wa umri mkubwa ambaye nitampenda. Si kwamba hawapo, lakini hawanivutii kabisa!
Single maza wa miaka 31 havutiwi na wanaume wakubwa. Duniani kuna vituko.
 
Back
Top Bottom