Changamoto za kupata mtoto mchanga ukiwa umri wa kustaafu, unakuwa ni Baba Babu. Dawa ni kujipanga kabla, vinginevyo ni kubebesha watu mizigo yako

Changamoto za kupata mtoto mchanga ukiwa umri wa kustaafu, unakuwa ni Baba Babu. Dawa ni kujipanga kabla, vinginevyo ni kubebesha watu mizigo yako

I wish ungemuona utatupilia mbali hizo fikra potofu.
Kumuona sura au akili huyo mtoto wa Pascal Mayala? Sura aweza kuwa vizuri shughuli kwenye akili .Toto la baba mzee na Mama mzee changamoto hata akizaliwa mzima iko kwenye akili mbele utaliona performance shule kuwa kuna walakini hata ulipeleke shule nzuri
 
Hongera sana; Kwa sie watu wa poti kuzaa kwenye umri mkubwa ni kawaida sana.Kuzaa kwenye 50 - 60 ukanda wa ziwa wala haishtui hio ni moja ya mila na desturi za u poti! Happy birthday Mayalla Snr na Happy born day Mayalla Jnr. Nguvu ya mamba kumai.
Kwa mwanaume it is ok.

Huyo mzaaji mwanamke ana umri gani awe hawara au mke whatever .Shida iko hapo

Pascal atueleze huyo mwanamke mzaaji ana umri Gani? Issue sio kumwita Pascal Mayala Junior
 
Pasco, umezaa na mkeo? Watoto 8 ni wengi sana. Wanatumia financial, physical and emotional resources nyingi sana kuwahudumia na kuwalea. I think it wasn’t the wisest decision for you to have a baby at this point in your life. Hapo umefulia mzee. Big time.
Wanasema huwezi kua bingwa milele...if it's true amefulia inakuhusu nini...? Au wewe una uhakika wa kudumu ulivyo milele?
 
Happy birthday brother, Mungu akupe maisha marefu kaka. Wewe ni moja ya watu mnastahili kuwa na kitabu cha kuelezea maisha yako ya uandishi/utangazaji.

Guru wa mahojiano, Respect brother!
 
Kumuona sura au akili huyo mtoto wa Pascal Mayala? Sura aweza kuwa vizuri shughuli kwenye akili .Toto la baba mzee na Mama mzee changamoto hata akizaliwa mzima iko kwenye akili mbele utaliona performance shule kuwa kuna walakini hata ulipeleke shule nzuri
Wengine wanakua bright sana wazaz wakiwa na umri mkubwa. Usikariri
 
Mungu kampa mwanadamu kuishi miaka 70, mingine bonus, yangu ni hayo Tu!
Hongera kwa kuitikia wito wa kuijaza dunia!
Umepokea zawadi nzuri, Una watoto na wajukuu, hawa wajukuu watamuitaje bamdogo junior?! Wamemzidi umri!
 
Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.

Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.

Asante kwa elimu ya uwekezaji (investment). Tatizo linakuja, tukistaafu, ndio tunategemea mafao hayo tukajengee nyumba, je, huo uwekezaji tutauweza? Tunategemea hela hiyo tufanye mambo yote tuliyoshindwa kufanya tukiwa kwenye ajira; kujenga nyumba ya kuishi, kununua gari, shamba, nk, hapo hela ya uwekezaji itabaki? Sio kwamba hatutaki kuwekeza, la hasha, ila uhalisia wa maisha unatupeleka uelekeo mwingine!
Mbona mnasahau withholding tax?
 
Leo Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa tayari ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa mbinu za changamoto za ulezi katika umri mkubwa kwa huku unajiandaa kustaafu, huku vichanga vinaendelea kuzaliwa!.

Naomba kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, mgeni huyu mpya, amebisha hodi Duniani Leo, 8 April, 2022 majira ya saa 4:00 asubuhi, katika hospital ya Aga Khan, na kwa vile mgeni mwenyewe ni kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pascal, hivyo ataitwa Pascal Mayalla, Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pascal Mayalla Snr baada ya ujio wa Pascal Mayalla Jnr.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa tayari wana watoto, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kiume, huyu Pascal Mayalla Jnr ni baba yao mdogo na wajukuu wa mabinti huyu ni mjomba wao, baba mdogo na mjomba kuwa ni mdogo kuliko wajukuu, haupendezei kivile!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida sana, watu wanajenga familia wakiwa vijana, ukifika miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na sio tena kuanza kulea na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus ni kawaida sana, tuna mfano mingi tuu, ukitafuta umri wa Chief Burito wakati Julius Kambarage Nyerere anazaliwa, hutashangaa!. Hata Nabii Ibrahim alipomzaa Isaka alikuwa na miaka 90!. Mfano mzuri wa karibu ni yule Mzee wetu fulani, Al maarufu na mashuhuri, alipata watoto twins at 74 years!, hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus, mimi ni bado sana!, ila huyu ni last born!.

lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50 +, hiyo peke yake tayari ni stress tosha, kwasababu mtoto anatakiwa kutimiza the age of majority, akiwa total dependant. Pesa za mstaafu, haziwezi kumlipia shule nzuri mtoto, unless nikubali akasome St. Kayumba!. Kama hao wenzake 8, hakuna aliyesoma St. Kayumba, hivyo huyu kitinda mimba wa Baba Babu, needs a little bit kujipanga zaidi. Hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wale wote wenye umri mkubwa, huku wakikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitega uchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa hata kupokea simu ya dingi ukidhani ni mzinga!, kumbe simu nyingine wala sio mizinga, ni dingi amekukumbuka tuu na anakupigia ili kukusalimia tuu.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matoi yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.

Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 16 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,300,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
All the best brother Pascal. Mungu akufanyie wepesi kwenye malezi ya Pascal jnr, na afanye njia pale panapoonekana kama hapana njia.
 
Leo Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa tayari ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa mbinu za changamoto za ulezi katika umri mkubwa kwa huku unajiandaa kustaafu, huku vichanga vinaendelea kuzaliwa!.

Naomba kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, mgeni huyu mpya, amebisha hodi Duniani Leo, 8 April, 2022 majira ya saa 4:00 asubuhi, katika hospital ya Aga Khan, na kwa vile mgeni mwenyewe ni kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pascal, hivyo ataitwa Pascal Mayalla, Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pascal Mayalla Snr baada ya ujio wa Pascal Mayalla Jnr.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa tayari wana watoto, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kiume, huyu Pascal Mayalla Jnr ni baba yao mdogo na wajukuu wa mabinti huyu ni mjomba wao, baba mdogo na mjomba kuwa ni mdogo kuliko wajukuu, haupendezei kivile!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida sana, watu wanajenga familia wakiwa vijana, ukifika miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na sio tena kuanza kulea na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus ni kawaida sana, tuna mfano mingi tuu, ukitafuta umri wa Chief Burito wakati Julius Kambarage Nyerere anazaliwa, hutashangaa!. Hata Nabii Ibrahim alipomzaa Isaka alikuwa na miaka 90!. Mfano mzuri wa karibu ni yule Mzee wetu fulani, Al maarufu na mashuhuri, alipata watoto twins at 74 years!, hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus, mimi ni bado sana!, ila huyu ni last born!.

lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50 +, hiyo peke yake tayari ni stress tosha, kwasababu mtoto anatakiwa kutimiza the age of majority, akiwa total dependant. Pesa za mstaafu, haziwezi kumlipia shule nzuri mtoto, unless nikubali akasome St. Kayumba!. Kama hao wenzake 8, hakuna aliyesoma St. Kayumba, hivyo huyu kitinda mimba wa Baba Babu, needs a little bit kujipanga zaidi. Hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wale wote wenye umri mkubwa, huku wakikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitega uchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa hata kupokea simu ya dingi ukidhani ni mzinga!, kumbe simu nyingine wala sio mizinga, ni dingi amekukumbuka tuu na anakupigia ili kukusalimia tuu.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matoi yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.

Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 16 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,300,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
Bandiko refu lakini linakutia stress mwenyewe!

Hofu hii ya kuogopa watoto wa kustaafia huwapata wastaafu watarajiwa walio wengi bila kuwa wamefanya utafiti wa kina.

Lakini acha nikupe angalizo la upande mwingine wa shilingi ambao wewe haujauangazia!

Kuna point moja tu hapo inayokusaga roho, ni ile hofu ya kushindwa kumsomesha shule ghali mwanao baada ya kustaafu!

Nitakuuliza kwa nini uhofie jambo dogo kiasi hicho wakati mchanganuo wako wa kutumia mafao yako upo vizuri, kama kweli umejipanga katika uwekezaji wa namna hiyo?

Mtoto wa kustaafia wala asikuhofishe bure, ni faraja aliyokuletea Mwenyezi Mungu unapoyakaribia maisha rasmi ya upweke!

Ukiisha kustaafu, urafiki wa maofisini hukoma rasmi, mke naye ashakuwa mbibi kachoka, inabidi umsaidie majukumu yake mengine!

Umri huo uliofikia na kwa kukiri mwenyewe, ushasomesha watoto zako hao na pengine washajitegemea kimaisha, hauishi nao hapo nyumbani.

Utakapostaafu, utabakia hapo wewe na "shemeji" tu jumba lote bila kitegemezi wa kuwafariji!

Ukiwa kazini, ulikuwa boss kuanzia ofisini hadi nyumbani ambapo ulikuwa umezungukwa na familia kubwa ya mke na watoto, sasa mmebakia wawili, uboss haupo tena mkuu kuanzia ofisini hadi nyumbani.

Kupata zawadi ya huyo mtoto sasa, mshukuru sana Mungu kwa kuwa umepata "pakushika" na mfariji wako mkubwa.

Cheo na hadhi ya mwanao huyo mchanga iko pale pale, ni "bwana mdogo", "ba'mdogo", "babu mdogo" nk nk, heshima yake haina mjadala na kwako ni utajiri wa familia, ambapo hautakosa kabisa watoto vyumbani mpaka mwisho wako.

Umepata faraja itakayokulinda mpaka ukikongwe wako ama mpaka kudaja!

60 kwa 20 utakuwa na 80 Mungu akikupa uhai.

Na shemeji anaonekana bado ni kijana kwa kukuletea hiyo faraja uzeeni isee!

Kumlisha mtoto mmoja, kumsomesha utakavyo na mahitaji mengine hayatakushinda maana vyanzo vya mapato rasmi unavyo.

Nimeitamani sana baraka hiyo uliyoipata wewe kama ingelikuja kwangu singelijuta, ningelishukuru sana Mungu.

Nimeandika nikiwa na uzoefu wa adha ya kuishi bila mtoto nyumbani baada ya kustaafu.

Pokea hongera za dhati kabisa na hofu ondoa, mtoto atakua kama kawaida na mahitaji umtakiayo atapata , Mungu ni mkubwa omba tu uhai.
 
Back
Top Bottom