Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.
Ndugu zangu Watanzania eti;
Ukigundua kuwa umemkosea mtoto wako mdogo huwa unafanya nini ili kuweza kupooza machungu yake na wewe kujipunguzia hatia nafsini mwako?
Unamnunulia anachokipenda (chips), unamuomba msamaha au unapotezea tu?
(1) Just imagine umemchapa mtoto kwa kumhisi anang'ata buttons za remote controller ya TV kumbe sio yeye bali ni panya ndio wanaharibu? Au;
(2) Mwanao umemkosea ulipomgombeza kumbe siyo yeye aliyemwaga maziwa...!!!!!
Ukigundua kuwa umemkosea mtoto unafanya nini?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Baadhi ya maoni ya wadau
=========