Changamoto za uke wenza

Changamoto za uke wenza

kwaio mwanaume huyo akioa wawili au watatu huwa si chochote, lakini akitoka na makahaba mia ndio unamuona ana nguvu?
Umeshasema makahaba tofautisha mahitaji ya mke na kahaba hata siku moja hayawezi kuwa sawa. Na kuridhika sio ngono pekee ili mke aridhike kuna vitu vingi.
 
Sifa Moja wapo ya kuoa Wake wawili ni kuwa na Uwezo!

Sasa Kama huna Sifa ya 'Uwezo' Kihelehele cha nini?
 
Eeeh ndio

Nani anataka dushe la foleni? Mambo ya zamu.????

Wakati wewe unaliwazwa na yeye analiwazwa.....unadhani kuna mwanamke anapenda ukewenza????


Ila wanaume viumbe wa ajabu sana....

Kumridhisha mwanamke 1 tu kazi sasa unapowapanga 11 unategemea nini???


Mswati tu na ufalme wake amechapiwa....


(
 
Nilishawai muuliza Dada mmoja ambaye alikuwa ameolewa mke wa pili na jamaa flani ;
Hivi kwanini unachipuka wakati umeolewa ?
jibu alonijibu wallah niliishiwa nguvu,
Yule Dada alisema hivi; Tatizo Dushelele la foleni yeye hawezi,
Dah niliishiwa nguvu sasa mpaka nikajiuliza kwanini akubali kama alikuwa hawezi kulisubiria mpaka litoke uko kwenye mzunguko.


Ukiachana na mfano huo hapo juu upo mwingine ambao nao pia ni dada ambaye najua makuzi na malezi yake ,alikulia katika dini na alikuwa na msimamo thabiti katika dini,Aliolewa na jamaa flani ,ambaye waliishi vizuri wakafanikiwa kujenga na kuwa na maisha mazuri,

Baada ya kuwa na maisha mazuri jamaa aliowa mke wa pili na hapa ndipo timbwili lilipoanza ,maana mwisho wa siku yule dada naye alitafta mtu wa pembeni kwa ajili ya kumtoa mawazo.

Jambo hili limekuwa likinichanganya sana ,maana nikitazama wengi walokuwa na mahusiano na mke zaidi ya mmoja ,wengi wanasaidiwa wake zao awe mkubwa au mdogo.

Nimejikuta naogopa hata ikifikia kuja kuowa wake wawili ,maana wengi wanachapiwa na hawajui wanachapiwa .

Nasababu kubwa nimeiyona wanayoijenga wanawake ni kuwa bwana wakuchangia hawawezi ,

Sina lengo na kupingana naafundisho alokuja nayo bwana mtume ,(Rehma na Amani zimshukie),ila nikitazama wanawake wa zama hizi ni mtihaani kwakweli ,maana kila napozungunga kwa hawa watu hali ni hiyo hiyo ,yaan kumi kwa mmoja ukute ndo mwenye kujiheshimu,
maana haya mambo yanafanywa mpaka na wamama wa makamo yaani ukiwaangalia huwezi amini,


Angalizo kwa waloowa wake wawili;
1;Jamani msijisahau sana iwe nyumba kubwa au ndogo basi kule ambapo utakuacha basi ujuwe watu wanakusaidia.

2;Pia ziara za kustukiza muhimu sana,maana wengi akiwa zamu ya bi mkubwa ,huku kwa bi mdogo anamuacha free tu usiku kucha hata kupitia pita hakuna mpaka ifike zamu ya mchana,au kama atapita basi mchana,
Jamani kuweni makini mkitoa tu miguuu watu usiku wanakuja kulala na uzuri ratiba zenu wanazijua fika siku ambazo hampo




Ebu wadau mkuje Hapa tupeane maarifa maana mpaka nimekuwa muoga sana wakumiliki majiko mawili japo natamani sana hapo baadae, maana kwa sasa Hali tete


Kwa hiyo akichepuka nje anakuwa hachangii huo mkia? Wewe sema umetunga stori tu.
 
Umeshasema makahaba tofautisha mahitaji ya mke na kahaba hata siku moja hayawezi kuwa sawa. Na kuridhika sio ngono pekee ili mke aridhike kuna vitu vingi.
kama umeolewa alafu unachepuka kwanini usiwe kahaba? yaani we kwako kuchepuka ni kawaida sio? Kama mumeo anakupatia kila kitu na mapenzi anakuonesha kwa nini tena uchepuka kisa eti ana mke wa pili? we umeona jibu la huyo mwanamke kusema hawez dushe ya foleni ni jibu sahihi?
 
Kwani wanapooa wake wengi wanategemea nini?

Maisha yenyewe ya sasa hivi wanaume wenye nguvu ni wa kuhesabu ikiwa mwanamke mmoja mtu anashindwa kumridhisha unadhani ukiwa na zaidi ya mmoja nini kitatokea.
si ndo hapo sasa. na inakua hadi mapenzi yanaishia kwa mmoja tu ukiachilia mbali mambo ya 6 kwa 6. kwanini nisitafute kafaraja na mimi? hahahaha.
 
Mkuu tunarudi pale pale ziara za kustukiza ni muhimu iwe mchana au usiku,
maana huwa wakijuwa ratiba yako basi andika umeumia ,
kama mchana hunatabia ya kurudi basi atautumia muda huo huo wa mchana na kama usiku basi ni vile vile,

Unajua wapo wanaume wanatabia huwa hawarudi nyumbani kwao mpaka watoe taarifa ,sasa hiyo watoto wa kike huwa wanachukuwa point na kuanza kufanya yao mpaka utaporudi
Sasa mwanamke kama huyo ndio tunasema hana maadili. Mana kumtaarifu mkeo muda unaorudi ni jambo jema tu, pengine ukifika home unakuta full mahanjumati umeandliwa na masurprise. Kwa mke ambae ana maadili hasa, na anaejielewa hawezi kuchepuka hata kama utakaa mwez hujarudi. Haya yote ni matokeo ya ugrilfriend na uboyfriend, vijana wakiwa na mambo izi ndoa zao hazitulii. Ndoa ni kuaminiana, lakini amani lazima itoweke tu ikiwa mwenzako umempata kwa njia za haramu. Mfano mkeo mwanzo alikuwa na boyfriend wake, na wewe ukijua ukaenda kumtongoza akakubalia, akamuachia bf wake akaja kwako, we unafikiria hawezi kukuacha na wewe akenda kwa mwengine? Au kabla ya kuoana mlifanya zinaa, na kuna njia mlikuwa mnatumia kukutana kisiri, mwanamke kama huyu tayari wewe mwenyeo ushamfundisha jinsi gani agegedwe kisiri tena asigegedwe kama ww hupo?


Ishu kuu hapa ni MAADILI ya MME na MKE ndio yatakyotunza ndoa. Sio kujua ratiba za mwenza, wala sio dushe la foleni. kama haitegemei maadili, basi pole sana madereva wanaokwama congo, mapilot na mabaharia mana kama concept yako ni kuwa wanagongewa tu.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia sie madereva wa Magari makubwa ambao sometimes tunakwama Congo mwezi mzima tunachapiwa? Vipi wife wa rubani nae atakuwa anachapiwa tu maana hawezi kurudi nyumbani kila siku. Mwanamke kuigawa nje ni tabia tu wala si kusema hawezi kuvumilia siku mbili mpaka zamu yake ifike.
madereva wa magari si ndo mnaongoza kwa nyumba ndogo kila mkoa? hahahaha acha mchapiwe tu.
 
Umeshakuwa katika ndoa za mitala?!


Ukweli ni kuwa hamna mwanamke anayetaka mumewe aoe mke mwingine


Kama unampenda mumeo siku akikwambia anataka kuoa mke mwingine mapenzi yatapungua kwa asilimia kubwa kama sio kwisha
swadaktaa
 
si ndo hapo sasa. na inakua hadi mapenzi yanaishia kwa mmoja tu ukiachilia mbali mambo ya 6 kwa 6. kwanini nisitafute kafaraja na mimi? hahahaha.
Mbona wapo wenzenu wanaishi na mume mmoja wao wako wanne na hakuna anaechepuka? na wanaishi kwa furaha tu. Mapenzi hayaishii kwa mmoja tu ukiwa unatimiza majukumu yako katika ndoa kwa mumeo. mapenzi yanaanza kuisha pale unapojenga dharau kwa mumeo. wanawake wa siku izi bana.... eti na yeye akatafute kafaraja.... yaani akili zenu zimekuwa kingonongono tu. Ndo maana mtaendelea kutumiwa vizuri....mkiona fahari eti...
 
Ukiwa umeolewa kwa lengo la kujenga maisha na kujenga familia, basi hutoona sababu ya kuchepuka. Ila ukiwa umeolewa kisa mgegedo, basi utachepuka tu hata kama mumeo hana wa pili... mana umefata mapenzi ya mgegedo..... Tunaona humu mada watu wanalalamika wake/wachumba zao wanachepuka, na mtu hajaongeza mke. mwisho juzi nimesoma story moja jamaa mkewe kagegedwa na ndugu yake..... Hii yote inaonesha kuchepuka ni Ukahaba......
 
kama umeolewa alafu unachepuka kwanini usiwe kahaba? yaani we kwako kuchepuka ni kawaida sio? Kama mumeo anakupatia kila kitu na mapenzi anakuonesha kwa nini tena uchepuka kisa eti ana mke wa pili? we umeona jibu la huyo mwanamke kusema hawez dushe ya foleni ni jibu sahihi?
Kwa mwenye mke zaidi ya mmoja sio rahisi kuwaridhisha wote kama unavyofikiria.
 
si ndo hapo sasa. na inakua hadi mapenzi yanaishia kwa mmoja tu ukiachilia mbali mambo ya 6 kwa 6. kwanini nisitafute kafaraja na mimi? hahahaha.
Eti! Ni wachache watakao kukubali lakini ukweli ndio huo haiwezekani wote wakaridhika.
 
Eeeh ndio

Nani anataka dushe la foleni? Mambo ya zamu.????

Wakati wewe unaliwazwa na yeye analiwazwa.....unadhani kuna mwanamke anapenda ukewenza????


Ila wanaume viumbe wa ajabu sana....

Kumridhisha mwanamke 1 tu kazi sasa unapowapanga 11 unategemea nini???


Mswati tu na ufalme wake amechapiwa....


(
Ujuwe wanawake ni wengi jaman kila mtu na dushe lake haiwezekani inabidi tu msubiri ivo ivo la foleni ili mgawane[emoji87] [emoji87] [emoji87]
 
Kwa hiyo akichepuka nje anakuwa hachangii huo mkia? Wewe sema umetunga stori tu.
Mkuu usiwe na dhana potofu si kila stor inayoletwa umu ni yakutunga ,
kwani kipi cha ajabu unachokiona hapo hakiwezi kutokea kwenye maisha halisi?

Jaribu kuishi mazingira tofauti ndo utajua mtaani kuna mambo.
 
Back
Top Bottom