#COVID19 Chanjo ya Corona iwe lazima kwa baadhi ya makundi yanayotoa huduma za kijamii

#COVID19 Chanjo ya Corona iwe lazima kwa baadhi ya makundi yanayotoa huduma za kijamii

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Chanjo ya Korona inaweza kuwa hiari, lakini usiseme hutaki chanjo halafu uendelee kuwa konda wa basi au nesi hospitali, tafuta kazi nyingine.

Katika hali ya haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufanya analotaka ili mradi asivunje sheria au kuingilia au kuathiri haki za watu wengine katika kuwa kwao huru na kutofanyiwa bugudha za kimaisha.

Sasa wapo wanaotaka kwamba suala la chanjo za Korona liwe la utashi wa mtu, watu kama kina Aunt Fatma Karume. Na wapo wanaotaka chanjo za Korona liwe lazima, watu kama kina Mbowe. Wote hawa wapo sawa, lakini kuwa kwao sawa kuna mipaka.

Nikianza na kina Fatma Karume, ni sawa watu kuwa huru kuamua kuchanja au kutochanja dhidi ya Korona. Lakini sasa, wewe unapoamua hutaki kuchanja basi msimamo wako usiathiri au kuhatarisha maisha ya wengine.

Kama utakataa kuchanja na ukaamua kujifungia nyumbani kwako hilo ni hiari yako. Lakini usikatae kuchanja halafu uje unipumulie virusi vya korona sugu mimi ambaye nimekubali kuchanja, au hata watoto ambao wako chini ya umri wa kuchanja, au watu ambao wameambiwa wasichanje kwa sasa kwa sababu mbalimbali kama ujauzito.

Na kwa kina Mbowe, kinyume cha hili la kina Fatma kinatumika kwako. Ikiwa sitaki kuchanja na hata niko tayari kuacha kazi yangu ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya wengine kwa sababu sijachanja, basi usiniingilie, niache nijifungie nyumbani kwangu, kwa kuwa sina haja ya kujichanganya na watu wengine.

Tukielewana katika haya basi tutakuwa sawa.
 
Katika hali ya haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufanya analotaka ili mradi asivunje sheria au kuingilia au kuathiri haki za watu wengine katika kuwa kwao huru na kutofanyiwa bugudha za kimaisha.

Sasa wapo wanaotaka kwamba suala la chanjo za Korona liwe la utashi wa mtu, watu kama kina Aunt Fatuma Karume. Na wapo wanaotaka chanjo za Korona liwe lazima, watu kama kina Mbowe. Wote hawa wapo sawa, lakini kuwa kwao sawa kuna mipaka.

Nikianza na kina Fatuma Karume, ni sawa watu kuwa huru kuamua kuchanja au kutochanja dhidi ya Korona. Lakini sasa, wewe unapoamua hutaki kuchanja basi msimamo wako usiathiri au kuhatarisha maisha ya wengine. Kama utakataa kuchanja na ukaamua kujifungia nyumbani kwako hilo ni hiari yako. Lakini usikatae kuchanja halafu uje unipumulie virusi vya korona sugu mimi ambaye nimekubali kuchanja, au hata watoto ambao wako chini ya umri wa kuchanja, au watu ambao wameambiwa wasichanje kwa sasa kwa sababu mbalimbali kama ujauzito.

Na kwa kina Mbowe, kinyume cha hili la kina Fatuma kinatumika kwako. Ikiwa sitaki kuchanja na hata niko tayari kuacha kazi yangu ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya wengine kwa sababu sijachanja, basi usiniingilie, niache nijifungie nyumbani kwangu, kwa kuwa sina haja ya kujichanganya na watu wengine.

Tukielewana katika haya basi tutakuwa sawa.
Labda kuweka sawa taarifa yako.Hata kama umechanja kuambukizwa kuko pale pale sema mwenye chanjo anayo chance kubwa kutokupata yale madhara yanayosababishwa na virusi vya corona.Ila kama huja chanja na kinga zako ni za wasiwasi,hii kitu ikikupata madhara yake ni makubwa sana.Yaani itakushughulisha sana vilivyo.

So tusidanganye watu eti kuchanjwa huambukizwi,no huo ni uongo.

Narudia,ukichanjwa unanafasi kubwa sana ya kuhimili madhara ya corona pindi unapoambukizwa.Ila haimanishi ukichanja basi hutakiwi kuvaa barakoa na kuacha zile taratibu zote za kujikinga,na hii kwa sababu ya kuwakinga ambao hawajachanja bado.

Ndiyo maana hili ni jambo binafsi sana,ni wewe mwenyewe kujitathimini hali yako na exposure yako kwenye maeneo hatarishi.
 
Mkuu, hivi unajua tangu uzaliwe umeshafanyiwa chanjo ngapi? Na kitu gani kilikufanya uwe na imani na hizo chanjo lakini sio hii ya Korona, hadi kuwapeleka watoto wako wanapozaliwa kuchanjwa?

Kuna watu kama Magufuli kwa mfano, walidai wazungu wanaweza kuwa na ajenda ya siri katika hizi chanjo. Lakini ni chanjo na dawa za wazungu ngapi unaingiza mwilini mwako ambazo wameshindwa kuzitumia kama nia yao ni kukudhuru? Hivi ni akili kudhani kama wazungu wangetaka kutudhuru watu weusi wangetumia chanjo ya ugonjwa ambayo hata wao unawaua? Huoni kama wangetumia chanjo za tropical diseases ambazo kwao hazipo?

Hiyo yellow card tunayolazimishwa kuwa nayo ikiwa na chanjo za kipindupindu, yellow fever, dengue sijui nk, unafikiri wazungu wanachanja hayo madude? Vidonge vya uzazi wa mpango sijui, mbegu za mahindi nk, kwa nini wasivitumie wakijua athari upande wao zitakuwa kidogo sana kwa sababu hawatumii ugali kama Wasukuma wa Mwanza?

Vitu vingine unapaswa kutumia akili kidogo tu kuelewa
Why unademka?
Choma chanjo ujilinde dhidi ya wasiochanjwa
 
Why unademka?
Choma chanjo ujilinde dhidi ya wasiochanjwa
Ni suala la kuelewa sio kusema tu chanja ujilinde dhidi ya wasiochanja. Tatizo ni kwamba, watu wasiochanjwa wanasababisha virusi kuendelea kusambaa na kubadilika, kwa kuwa kunakuwa na watu ambao wanavi-host. Sasa kadiri ambavyo watu hao wanaendelea kuwapo, na virusi vinaendelea kuwatumia kujibadilisha, hata nyie mliochanja itafikia mahali vile virusi wanavyosambaza vimebadilika na chanjo mliyofanya haiwazuii tena.

Na kama nilivyosema, kuna watu kama watoto chini ya miaka 12 na wajawazito, wenye BP kali nk, hawaruhusiwi kuchanja. Kwa hiyo kuchanja ni kulilinda hili kundi pia.
 
Ni suala la kuelewa sio kusema tu chanja ujilinde dhidi ya wasiochanja. Tatizo ni kwamba, watu wasiochanjwa wanasababisha virusi kuendelea kusambaa na kubadilika, kwa kuwa kunakuwa na watu ambao wanavi-host. Sasa kadiri ambavyo watu hao wanaendelea kuwapo...
Its impossible kulazimisha watu chanjo
Ukikubali hilo hutapata shida
 
Mkuu me nahisi kuna watu wanalipwa kwa kazi ya kuhamasisha huu upuuzi walio uita chanjo.
Haiwezekani me na familia yangu tukatae kudungwa chanjo, alafu anatokea kenge analazimisha tuchanjwe kisa yeye na familia yake wamechanjwa.
Ndo hapo sasa ushangae
 
Jamani wilaya niliopo sijashudia kisa chochote cha Covid 19, sio wimbi la kwanza, lapili wala hili la tatu, kwahiyo huwa na jiuliza hiyo Corona inatuogopa watu wa maeneo haya niliyopo?
 
Mkuu me nahisi kuna watu wanalipwa kwa kazi ya kuhamasisha huu upuuzi walio uita chanjo.
Haiwezekani me na familia yangu tukatae kudungwa chanjo, alafu anatokea kenge analazimisha tuchanjwe kisa yeye na familia yake wamechanjwa.
Na kuna watu wanalipwa kusema chanjo zinaua na kutengeneza video hadi kuonyesha ukichanja ukibandika balbu mwilini itawaka.

Haiwezekani mimi na familia yangu tukubali kudungwa chanjo halafu anatokea kenge analazimisha kutupumulia usoni na virusi vyake sugu vya korona kisa yeye na familia yake wamekataa kuchanja
 
Sasa kama mtu aliyepata chanjo anaweza kupata maambukizi kwa mtu ambaye hajachanjwa kuna haja gani ya kupata hiyo chanjo..........
Swali lako nilijibu hapo juu

Tatizo ni kwamba, watu wasiochanjwa wanasababisha virusi kuendelea kusambaa na kubadilika (mutate), kwa kuwa kunakuwa na watu ambao wanavi-host. Sasa kadiri ambavyo watu hao wanaendelea kuwapo, na virusi vinaendelea kuwatumia kujibadilisha, hata nyie mliochanja itafikia mahali vile virusi wanavyosambaza vimebadilika na chanjo mliyofanya haiwazuii tena.

Na kama nilivyosema, kuna watu kama watoto chini ya miaka 12 na wajawazito, wenye BP kali nk, hawaruhusiwi kuchanja. Kwa hiyo kuchanja ni kulilinda hili kundi pia.
 
Unajuaje kama huna? Unaleta yale yale ya kuwapima watu HIV kwa macho. Kuwa na Korona sio lazima uumwe na kushindwa kupumua
Sasa kama umepata chanjo kwanini una mashaka na mimi ambaye sijachanjwa hali ya mimi siwezi kukuambukiza wewe ambaye humechanjwa......??
Swali lako nilijibu hapo juu

Tatizo ni kwamba, watu wasiochanjwa wanasababisha virusi kuendelea kusambaa na kubadilika (mutate), kwa kuwa kunakuwa na watu ambao wanavi-host. Sasa kadiri ambavyo watu hao wanaendelea kuwapo, na virusi vinaendelea kuwatumia kujibadilisha, hata nyie mliochanja itafikia mahali vile virusi wanavyosambaza vimebadilika na chanjo mliyofanya haiwazuii tena.

Na kama nilivyosema, kuna watu kama watoto chini ya miaka 12 na wajawazito, wenye BP kali nk, hawaruhusiwi kuchanja. Kwa hiyo kuchanja ni kulilinda hili kundi pia.
Nyie mnaotaka kuchanjwa endeleeni kwa kadri virusi vinavyo badilika........
 
Back
Top Bottom