Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Chanjo ya Korona inaweza kuwa hiari, lakini usiseme hutaki chanjo halafu uendelee kuwa konda wa basi au nesi hospitali, tafuta kazi nyingine.
Katika hali ya haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufanya analotaka ili mradi asivunje sheria au kuingilia au kuathiri haki za watu wengine katika kuwa kwao huru na kutofanyiwa bugudha za kimaisha.
Sasa wapo wanaotaka kwamba suala la chanjo za Korona liwe la utashi wa mtu, watu kama kina Aunt Fatma Karume. Na wapo wanaotaka chanjo za Korona liwe lazima, watu kama kina Mbowe. Wote hawa wapo sawa, lakini kuwa kwao sawa kuna mipaka.
Nikianza na kina Fatma Karume, ni sawa watu kuwa huru kuamua kuchanja au kutochanja dhidi ya Korona. Lakini sasa, wewe unapoamua hutaki kuchanja basi msimamo wako usiathiri au kuhatarisha maisha ya wengine.
Kama utakataa kuchanja na ukaamua kujifungia nyumbani kwako hilo ni hiari yako. Lakini usikatae kuchanja halafu uje unipumulie virusi vya korona sugu mimi ambaye nimekubali kuchanja, au hata watoto ambao wako chini ya umri wa kuchanja, au watu ambao wameambiwa wasichanje kwa sasa kwa sababu mbalimbali kama ujauzito.
Na kwa kina Mbowe, kinyume cha hili la kina Fatma kinatumika kwako. Ikiwa sitaki kuchanja na hata niko tayari kuacha kazi yangu ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya wengine kwa sababu sijachanja, basi usiniingilie, niache nijifungie nyumbani kwangu, kwa kuwa sina haja ya kujichanganya na watu wengine.
Tukielewana katika haya basi tutakuwa sawa.
Katika hali ya haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufanya analotaka ili mradi asivunje sheria au kuingilia au kuathiri haki za watu wengine katika kuwa kwao huru na kutofanyiwa bugudha za kimaisha.
Sasa wapo wanaotaka kwamba suala la chanjo za Korona liwe la utashi wa mtu, watu kama kina Aunt Fatma Karume. Na wapo wanaotaka chanjo za Korona liwe lazima, watu kama kina Mbowe. Wote hawa wapo sawa, lakini kuwa kwao sawa kuna mipaka.
Nikianza na kina Fatma Karume, ni sawa watu kuwa huru kuamua kuchanja au kutochanja dhidi ya Korona. Lakini sasa, wewe unapoamua hutaki kuchanja basi msimamo wako usiathiri au kuhatarisha maisha ya wengine.
Kama utakataa kuchanja na ukaamua kujifungia nyumbani kwako hilo ni hiari yako. Lakini usikatae kuchanja halafu uje unipumulie virusi vya korona sugu mimi ambaye nimekubali kuchanja, au hata watoto ambao wako chini ya umri wa kuchanja, au watu ambao wameambiwa wasichanje kwa sasa kwa sababu mbalimbali kama ujauzito.
Na kwa kina Mbowe, kinyume cha hili la kina Fatma kinatumika kwako. Ikiwa sitaki kuchanja na hata niko tayari kuacha kazi yangu ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya wengine kwa sababu sijachanja, basi usiniingilie, niache nijifungie nyumbani kwangu, kwa kuwa sina haja ya kujichanganya na watu wengine.
Tukielewana katika haya basi tutakuwa sawa.