Chanzo cha umasikini Afrika sio viongozi ila ukosefu wa ujuzi wa sayansi na teknolojia


Ubunifu ni utamaduni wetu sio wazungu. Tuna wasomi ambao hawabuni chochote cha kusaidia jamii na hata wakibuni hawasifiwi. Tunathamini wanasiasa ambao ni walaji badala ya wabunifu na wafanyabiashara. Korea, Japan zimeendelezwa kwa ubunifu na biashara
 
Ubunifu ni utamaduni wetu sio wazungu. Tuna wasomi ambao hawabuni chochote cha kusaidia jamii na hata wakibuni hawasifiwi. Tunathamini wanasiasa ambao ni walaji badala ya wabunifu na wafanyabiashara. Korea, Japan zimeendelezwa kwa ubunifu na biashara
Tunasoma ili tuajiriwe, masomo yetu ni ya kuajiriwa tu, hata tukienda Ulaya bado hatuwezi kujenga engine za magari au meli hata ndege.
 
Tunasoma ili tuajiriwe, masomo yetu ni ya kuajiriwa tu, hata tukienda Ulaya bado hatuwezi kujenga engine za magari au meli hata ndege.

Sio kusoma tu ni utamaduni. Mfano Bill gates na wengine wengi hawajamaliza hata vyuo lakini walikuwa na ubunifu kuliko watu wenye PHD's
 
Viongozi wetu na msimamo mibaya ya kisiasa inachangia. Nakumbuka kipindi cha Kikwete ilianzishwa mpango wa Elimu bure, Matokeo yake wanafunzi wakawa wengi kiasi ambacho madarasa, maabara, matundu ya vyoo n.k vikawa havitoshi.
Serikali kupitia wakuu wa mikoa, wilaya, wabunge na viongozi wengine wakawa wanahamasisha wananchi wachangie na serikali ita ongeza nguvu ili kila kata iwena shule yenye maabara, madarasa n.k.
Chakushangaza mheshimiwa Tundu Lisu akawa hataki/ anashawishi wananchi wa jimboni Kwake wasi changie. Wakati huo yeye watoto wake wanasoma shule nzuri tena wanachangia michango katika shule na hakatai Kuchanga. Sasa unaweza kupata picha jinsi baadhi ya wanasiasa wetu walivyo.
Baadhi ya wanasiasa walisema ni aibu kwa nchi kubwa kama Tanzania kutokua na ndege, Ndege zikanunuliwa Zitto akasema ndege zenyewe ni used, baadae akasema kipaumbele sio ndege.Chakushangaza Zitto akienda kwao kigoma anapanda ndege izoizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Andiko langu ni zuri sana. Ila huwezi kupata technology bure lazima ununue.

Kwa nchi kama Tanzania ni watu wachache ambao wanaweza kumudu kununua technology ya kuchakata malighafi ili kupata consumable product.

Taarifa ya 2016, TanTrade kupitia DG wake nd. Edwin Rutageruka iliweka wazi kuwa Lindi naMtwara pekee zili export tani za ufuta tani 440,925/mwaka. Wastania wa bei ya ufuta kama ilikuwa sh. 5,000 kwa kg maana yake nchi ilipata wastani wa 2.2Tril.

Mathalani kama leo nigenipa dhamana ya kibenki toka TIB, Bank ya maendeleo ya Kilimo au BoT kununua machine au mtu mwingine mwenye vision ya agro-processing ili kuunza mafuta kwenye global consumable standard. Tungeweza kuuza tani zaidi ya tani laki moja za mafuta na nchi ingeingiza walau 5.5 Tril badala ya 2.2 Tril.


Kwa kwa 65% inatoa mafuta Ukiuza na mashudu ambayo ni sawa na zaidi ya tani 150,000 kwa ajili ya chakula cha wanyama, more money gets in Tanzania domestic circulation.
hapo ni kama zaidi ya bil 70




Soko la mafuta ya ufuta Singapore
Tumia www.xe.com kupata exchange rate to TZS

Organic Sesame Oil, Kevala, 1/2 Gallon | Buy Products Online with Ubuy Singapore in Affordable Prices. B00A82MFYE

Soko la mafuta ya ufuta Bondeni ndani ya SADC
Tumia xe.com kupata exchange rate to TZS

Dabur Sesame Oil 250 Ml | Buy Products Online with Ubuy South Africa in Affordable Prices. B00FEQPSKW
Ubuy South Africa Online Shopping For sesame cooking oil in Affordable Prices.

Machine ya kuchakata mafuta na kujenga warehouse haizidi bil 15; baada ya hapo uwekezaji unatoa ajira,
uwekezaji unaleta more forex
uwekaji unachochea wakuli kulima zaidi maana soko la ndani lipo kununua mazao ghafi,
Tax base ya TRA inaongezeka.

Rais pale juu, super ndiyo maana anataka kuona industry inachochea kukuza uchumi. Iko haja uongozi wa kisekta wizara kuwa more innovative na creative ili utoa agri-industrial investment financing. Mtu/kampuni hapewi hela mkonini.

Wanakopeshwa machinery kwa benki kumlipa muuzaji wa machine au kuewa guarantee ya BOT kukopa fedha ambayo straight inanunua machine, warehouse inaengwa na right away uzalishaji unanza.

Honestly, nchi hii ni sleeping giant. Ila namna ya kuratibu mambo haya yatokee lazima Farao awepo wa kum-facilitate Yusuf kuwekeza kwa muktadha wetu na atarejesha mkopo kufuatia mauzo ya consumable products za ufuta, korosho, kahawa, pamba, chai the list goes on.
Sio vigumu kuwekeza kama kuna utayari wa kufanya kwa pamoja kupitia Public Private Partnership
Economic freedom should come today and not tomorrow
 
Tatizo la umaskini wa nchi za ki afrika no uelewa duni wa viongozi,na uroho wa madaraka.

Rejea uamuzi wa JPM kununua korosho,bila shaka ulikuwa ni uamuzi wa hovyo.
Kuhusu corona ndiyo useme,jamaa wanapima hadi matunda?

Kuhusu umeme,kulikuwa na shida gani kumalizia miradi ya gesi aliyokuwa ameifanya J. Kikwete kama siyo kutaka sifa?

Ukija kwenye madini,ukianza na Mkapa,JK Hadi JPM wote ni hovyo.

Ujenzi wa uwanja wa ndege huko Chato...na mengine...orodha ni ndefu kwa kweli.

Umaskini wa wa Afrika inaletwa ni viongozi wa hovyo na wadogo wa madaraka wa Africa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru kwamba umekili hali ya uchumi hapa nchini kwa sasa chini ya uongozi wa JPM ni mbaya, bali unaona si haki kuitumia Tanzania kwa sasa kama mfano wa hizo nchi maskini kwavile uongozi wa Rais Magufuli hauna muda mrefu kupima ufanisi wake.

Sasa hebu niambie, kama kweli unaamini kwa dhati kwamba umasikini wa nchi za Afrika ni kutokana na ukosefu wa maarifa ya sayansi na teknolojia, je uongozi wa JPM unafanya nini cha maana kuijengea nchi uwezo huo ili kuhakikisha nchi inaondokana na umasikini? Au unataka kuniambia hao marafiki zako wanaosomea uchumi Uingereza walikuhakikishia kwamba uwekezaji wa matrilioni ya shilingi kwenye miradi mikibwa ya ujenzi (structures) kama SGR, madaraja marefu, bwawa kubwa la umeme (JNHPP) na mahospitali kila wilaya unaofanyika chini ya uongozi wa JPM ndo njia sahihi ya kuondoa umasikini wa nchi?
 
Sio kusoma tu ni utamaduni. Mfano Bill gates na wengine wengi hawajamaliza hata vyuo lakini walikuwa na ubunifu kuliko watu wenye PHD's
Mafunzo yoyote ni masomo, Bill Gates hakuzaliwa anajua computer, alijifunza na kusoma nje ya shule.
 
Inakubidi kujifunza kwa nini China ni tajiri sasa wakati ilikuwa masikini, hakuna kiongozi yeyote mwenye ujuzi wa kutengeneza na kuunda bidhaa kama za Ulaya, tunatakiwa sisi kujifunza hayo siyo kutegemea siasa. Kwa sababu unavyotaka vifanywe na viongozi havina mtaji wa kutosha, na hilo ni kwa sababu sie ni masikini. Mradi wa gas hauzalishi umeme ila mradi wa kufua umeme unaojengwa na Magufuli, mkubwa kuliko yote east Africa.

Una mengi ya kujifunza la sivyo unachojua ni yale unayoambiwa na mabeberu ili wachafue nchi yetu, lakini kama umesoma vizurio post yangu ya uzi huu na kutumia akili, usingekwama kujua kwa nini sisi ni masikini. Hivi unajua utajiri wa Ulaya unatokana na nini? Jibu hilo kwanza fanya utafiti maana humu sio shule bali sehemu ya kujifunza kama Chuo, unafanya utafiti wako baada ya kupata mada.
 
Post yangu ina majibu yote kama ukitumia akili kuisoma, haijasema chochote kuhusu miradi ya nchi yeyote, kwa sababu hilo linaangukia kwenye mada kuu ya ukosefu wa sayansi na teknolojia kulazimika kuomba wazungu na wachina kujenga nchi yetu na kuongeza madeni na kudumisha umasikini.

Poat yangu ni pana for a big picture of Africa, sio kuhusu nchi moja moja kiundani, hilo hutaki kuelewa au you just don't get it. Tunaongelea sababu kuu ya umasikini Afrika nzima, common major mega reason only. Labda misamiati ytangu michache kufafanua hili, lakini naongea kama naongea na watu wanaotumia akili, wengi wameelewa ila wachache mpaka sasa wawili tu hawajaelewa, mmoja wapo ni wewe.
 
Viongozi hawaweki mambo wazi tutaendeleaje, mikataba siri, corona ni issue ya kiusalama badala ya kuwa issue ya kiafya hao wanasayansi wa tanzania watatafiti vp, bunge ni kuvutana tu na chadema mambo ya msingi watajadili saa ngapi. Hatuendelei kwa sababu za kiuongozi hata technolojia ikiwepo itatumika saa ngapi watu wanawaza uchadema na uccm!
 
Sawa mzee, ila mie nazungumzia mashine za viwanda, engine za magari, ndege, meli, Drones, hata mashine za kutengenezea nguo, dawa hata za mashambani. Pia uwezo wa kutengeneza barabara, madaraja, reli n.k.
 
Viongozi wetu sio wakutufundisha kutengeneza mashine hata za kusagia nafaka, engine za magari, meli, ndege, drones, mashine za kutengeneza barabara, madaraja hata kujenga madaraja hata majumba ya kisasa ya maghorofa makubwa. Wewe ndiyo wa kuisaka elimu hiyo toka ukiwa mtoto, badilisha miono na fikira utaona, hasa kama ulisoma post yangu vizuri as intellectual sio mwana siasa.
 
Sio viongozi wa kujua kutengeneza mashine na engine mbalimbali hata madawa ya hospital, ni siye wananchi, wao ni wanasiasa siye wazalishaji wanaohitaji uongozi. Jibu rahisi kuwalaumu viongozi na kufungia pazia ukosefu wa teknolojia kwa sababu ni ngume kwetu kutumia akili zote na kubaki na ujinga na umasikini wetu. Natumaini jibu langu linakupa mwanga.
 
Mi nadhani umaskini wa Afrika unaanzia kwenye uumbaji. Mungu alitunyima maarifa kidogo na akatubariki na resources nyingi sana alijua tu kwa akili zetu hizi resources haziwezi kutusadia ila zitawasidia wale aliowapa maarifa. Ni sawa na alivyofanya kwa nyumbu alijua nyumbu akiwa mwerevu simba atakosa chakula.haimake sense mpk sasa kuna watu wanakufa na njaa Afrika yaani hata kujilisha tumeshindwa.
Halafu always tunatafuta mchawi mara mabeberu mara viongozi? Mbona nchi za Asia zilitawaliwa na zine piga hatua? Hao viongozi wabovu wametoka kwenye jamii zetu ambazo ni mbovu pia.
 
Kwa kuwalaumu viongozi wetu badala ya kuutazama ukweli wa ukosefu wa ujuzi wa kiteknolojia, hakuta tufikisha popote ila kubaki kwenye umasikini na ujinga wetu. Sio siasa zinazojenga nchi bali UZALISHAJI, na lazima uwe wa kushindana duniani, sio kuzalisha malighafi pekee. Kwa undani zaidi jifunze politic economy kidato cha pili.
 
Si kweli kumlaumu mungu, hiyo pia ni moja ya kukataa lawama za wazi, ni siye wenyewe wala sio viongozi, sisi wote tunakosea.
Kwa kuwalaumu viongozi wetu badala ya kuutazama ukweli wa ukosefu wa ujuzi wa kiteknolojia, hakuta tufikisha popote ila kubaki kwenye umasikini na ujinga wetu. Sio siasa zinazojenga nchi bali UZALISHAJI, na lazima uwe wa kushindana duniani, sio kuzalisha malighafi pekee. Kwa undani zaidi jifunze politic economy kidato cha pili.
 
tatizo la Africa ni waafirica usisingizie teknolojia. Hakuna viongozi wapumbavu kama wa afrika,hukaribia kujipachika uungu waabudiwe
 
Kwa taarifa yako maswali ninayouliza haimaanishi nakulazimisha uyajibu. Hii ni mitego ya kujenga hoja ambazo huwezi kuzijibu na ukijaribu kujibu lazima utapotea.

Kiufupi tu ni kwamba nilitaka kukuonesha lwamba haihitaji kutoa muda zaidi kwa uongozi wa JPM ili tuhukumu kama hali ya uchumi itatengemaa au umasikini utaendelea kutamalaki kwasababu tayari anawekeza kwenye ujenzi unaoteketeza matrilioni ya shilingi badala ya kujikita kwenye maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Lakini ni muhimu kukumbuka kwamba hadi sasa ambapo muhula wake wa kwanza unaelekea ukingoni, hakuna hata mradi mmoja uliokamilika ua hata nusu. Hii maana yake ni kwamba miradi hii itaendelea kuteketeza fedha hadi muhula wake wa mwisho na hakuna kitakachokamilika. Kwamaana hii nikisema JPM amechemsha na kwamba hataweza kuvunja rekodi ya kikwete ya kukuza uchumi kwa zaidi ya 8%.

Zaidi nataka nirekebeshe pale uliposema uimara wa thamani ya sarafu ndo kigezo cha hali nzuri ya chumi na eti kwavile kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi chini ya uongozi wa JPM ni ndogo ukilinganisha na enzi za JK maana yake uchumi umeimarika, si kweli.

Kwa taarifa yako tu ni kwamba sarafu (Dinar) za Kuwait, Bahrain na Oman zinaongoza kwa kuwa na kuwa na thamani kubwa duniani na zinashika nafasi tatu za kwanza katika orodha ya sarafu 10 zinazoongoza kwa thamani hapa duniani. Je, unatakata uchumi wa nchi hizi uko juu kuliko Marekani, China na Japani, Ujerumani na Uingereza nchi ambazo ni nambari moja kwa uwezo wa sayansi na teknolojia?

Naomba uwasiliane tena na rafiki zako wanaosomea uchumi Uingereza wakuelekeze vizuri kuhusu uchumi.
 
tatizo la Africa ni waafirica usisingizie teknolojia. Hakuna viongozi wapumbavu kama wa afrika,hukaribia kujipachika uungu waabudiwe
Usiukimbie huo upumbavu wa kutojua kutengeneza hata dawa za magonjwa yote lazima tuagize toka nje, wa kutojua kutengeneza hata cherehani usijali mashine za viwanda hata madaraja yetu.

Kwani ni viongozi wetu wa kufanya hivyo au siyo sie wote? Unakimbia kuutazama ukweli kwamba sie ni wajinga kwa sababu ni jibu rahisi kwa wale wasio na fikira, na wanao tafuta kisingizio cha ujinga wao kutojua kutengeneza chochote? Unaujuzi wa kutengeneza chochote?

Tunazungumzia magari, ndege, meli, ndege za kivita, drones, computer, simu, hata nguo zetu karibu zote zinatoka China au Ulaya, barbara zetu na madaraja makubwa hate reli zinajengwa na wachina, wewe utafanya hivyo lini kuisaidia nchi yako? Kuwa mmojawapo wa wabunifu, engineer wa kuunda na kutengeneza ndege, magari etc, engineer wa computer etc?

Kwa wenye mawazo na muono mdogo watasma ni viongozi kwa sababu hawajui hata ni nini cha kufanya kupambana na umasikini, kama ungesoma vizuri post yangu ya kwanza na kuelewa usingejibu hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…