Charles Hilary ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu - Zanzibar

Tunasubiri uteuzi wa Baba levo awe waziri wa Sanaa utamaduni na michezo
 
Siyo kweli Charles Hilary ni Mpogoro wa Morogoro, kwa hiyo hata wewe ni chaka na umetaka kumuingiza mwenzio chaka.Mmekutana vipofu watupu, hakuna wa kumuonyesha mwenzake njia.
Asili yake ndiyo, lakini kwa kukua na kusoma ni Zanzibar. Sikiliza lafudhi yake vizuri uone kama ni ya kipogoro. Baba yake Mzee Hilary amestaafu polisi akiwa Zanzibar na alifungua 'business' yake maeneo ya Mpendae baada ya kustaafu.

Zanzibar wako wengi wenye asili ya bara ambao baadhi ni wazawa wa kule, mfano akina Mwakanjuki ambao baadhi wamezaliwa kule na wamekuwa wakiishi Zanzibar miaka yote.
 
Kweli yajayo yanafurahisha kama alivyosema Mwinyi.

Hii ya Mkristo kuteuliwa siyo record kweli kule Zanzibar? au Charles ni jina tu ila ni Ustadhi.
Augustino ramadhani alikuwa mkristo na amefanya Sana kazi serikali ya mapinduzi
 
Sasa hii ya wakristo kuitwa makafiri na chogo kule zanzibar inatokea wapi?
 
Sasa umekuja sawa kabisa ongezea na
Edington Kisasi alikuwa Askari Mzanzibar kutoka Kilimanjaro
Adam Mwakanjuki alikuwa askari CO Makutupora asili Mbeya Mzanzibar
Ally Hassan Mwinyi kwao ni Kisarawe akamzaa Dr Hussein Mwinyi Mzenj Rais wa sasa wa Zanzibar aliyemchagua Charles H. Mkangwa Mpogoro baba yake Mzee Hillary Mzanzibar
Charles kasomea Kinondoni
mikorogo yote ni Watanzania, linapokuja suala la maslahi au Cheo tunaanza kujitenga Upemba na Uzenj na Ubara
 
duh, kafir na Znz wapi na wapi
Na nyie mko bara mnakula maisha mnatuona mapimbi sio, sijapenda kabisa hiyo kauli ya kibaguzi sana, hamna Cha kututisha, dini ni mapokeo na mrengo tu kisikufanye kumnyanyapaa mtu kiasi hicho
 
Lilia bahati siku zote ndani ya hii dunia. Congrats mzee wa macharanga.
 
Shule ya sekondari alisoma Kinondoni Sec tukamaliza naye 1979 na mwaka 1980 akajiunga na RTD. Baba yake Mzee Hilary Nkwanga alikwenda pia kuzikwa Malinyi. Zanzibar baba yake alikuwa kikazi polisi na akaja kustaafia huku Tanzania Bara. Nakupa hiyo kama ulikuwa ubajua juu juu.
 
Hao kina Mwakanjuki n tofauti na Charles, hao kina Mwakanjuki babu zao walenda huko miaka ya utumwa. Charles tumesoma wote Kinondoni sec. Primary tu alisoma Zanzibar na hakumalizia kule alikuja malizia huku bara na ndiyo hapo alipomaliza Form four akaingia Redio Tanzania Dar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…