Charles Kimei: Serikali iwekeze kwenye Elimu ya ujuzi ambayo inaakisi maisha yetu ya kila siku

Nina uza duka.ila napenda kuwa na fani nyingi.
Umeme naujua.kufunga madishi najua.na hizo fani nataka niongezee
 
Mimi wasomi na viongozi wa nchi hii wakati mwingine hataga huwa siwaelewagi.
Kuna mamiswada na mashasheria yanapitishwa hapa,utadhani anayeona wala anayeguswa.
1:Hivi masomo yaliyofutwa mwaka 2003/4 Yale watu hamkwepoo? Unafuaje kilimo,unafutaje biashara,unafutaje uchoraji,unafutaji upishi?, unafutaje ufundi? Leo hii ukitaka mtu hata wa kuandika kibao cha shule ni shida.
2:Like Sheria la LoarnBoard kandamizi kabisa watu hawa hawa hakuna alihoji,yatapowafika utasikia kelele zake
3: Halafu hayo aliyo sema kimei watu wanawaona na kuyasikia,lakini ndiyo limepita hivyo.
4: Rais kusisitiza somo la Historia liwe la lazima ili watu wajue uzalendo,lakini nalo watalibumba vyumba tu.
Mie kwa Mtazamo wangu nilifikiria Wizara wakeomba maoni ya wadau jinsi gani hilo linatekelezwa.
Mfano, Tangu shule ya msingi kuandaliwe mtaala wa History ambao mpka mtu wa Phd atasoma.Hiyo inawezekana,mbona Somo la siasa liliwezekana?
Mfano:Somo hilo liitwe: Historia ya Tanzania kabla na baada ya uhuru.(The history of Tanzania before and after Independence.
Wakati huo huo history Ile ya kawaida pia itafundishwa kama ilivyo..
Sasa cha ajabu hapa mtaambiwa eti Kuwe na midahalo ya kuhudhuria mashuleni ndiyo imeisha hapo,watoto siku hizi hawapendi midahalo,hata hivyo walimu wetu hawawezi simamia hilo.
 
Nina uza duka.ila napenda kuwa na fani nyingi.
Umeme naujua.kufunga madishi najua.na hizo fani nataka niongezee
Hongera uko vizuri hiyo inaitwa multi skill mfano katibu mkuu wa CCM Dk Bashiru Ally Mbali na kuwa katibu mkuu wa CCM ni mwalimu mahiri wa chuo kikuu lakini pia ni mvuvi hodari mpiga makasia mitumbwi ya uvuvi,mchuuzi wa samaki ,dalali na dereva wa malori makubwa na fundi makenika wa malori makubwa na mkulima na fundi ujenzi wa nyumba

Hiyo multi skills muhimu kwenye maisha hufi njaa ongeza fani zingine ukiweza
 
Sina hakika kama umeelewa nilichoandika

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kuna wachina nafanya nao kazi naambiwa vyuo vile academics vingi sana wamebadilisha kwenda veta system. Na anayetokea mfumo wa veta ndiye anayelipwa Hela nyingi sana kuliko kama huyu wa udsm aliyejaa theory na ilhali hata redio fuse ikiungua hawezi kubadilisha
 
UJUZI HAUOZI.
Leo nikifukuzwa kazi naingia mitaani nafunga madishi na kazi za umeme
 
Tuliyosoma VETA naona sahv wenyewe mnatutambua [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] zamani tulikuwa tunadharaulika

Ova
Sawa, ila tuambie unafanya nini
 
Kazi Nyingi sasa hivi sio za white color jobs za kulamba suti na tai muambiane huko Chadema kuwa kazi za kulamba suti na tai hazipo ukiwemo ugombea uraisi , ubunge na udiwani kupitia Chadema
Tatizo upo kiuanachama kwa kila mada
 
Mkuu, asante kwa uzi wako.
====
Mkuu, kama haitakuwa shida. Naomba kujua skills ulizojifunza/soma lakini hujui unaziapply vipi (VP) kwenye maisha ya kawaida.

Karibu.

 
Moja ya sababu ya kuwa economic depression huko ulaya na Marekani zama hizo ni uneven distribution of income .

Hata watu wakiwa na ujuzi lakini wananchi uchumi ni mbovu hakuna tija hata kidogo maana fundi gari anasubiria mtu aje kutengeneza gari je mwenye gari asipokuwa na fedha ya kupeleka gari ufundi je

Haya umetengeneza kitanda mtu hana hela ya kuja kulipia huo ujuzi utakula wewe ?

Tujenge nchi.
 
yuko sahihi mzee Kimei, vyuo vikuu karibu vyote vinafundisha elimu ili tuajiriwe serikalini au ktk sekta binafsi na sio kujiajiri,

Waziri wa elimu na jopo lake lote wakae chini waangalie namana bora ya mitaala yetu ya elimu. kuanzia sekondari mfumo wa elimu ulenge kujiajiri zadi ndipo taifa letu litafikia uchumi wa juu wa kati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Stable systems duniani zinazalisha ajira ili kuwa na waajiriwa.
Outcome yake ni kuwa na mzunguko wa fedha kwenye sekta za kibenki, pension funds, insurance funds, real estate development na vingina kama legal, suppliers chain management na logistics.

Ili tukifikie hapo, lazima tuwe system thinking approach and system execution approach.
Sio hii ya kila mmoja kujiajiri na kupambana na hali yake.

Maana hata daktari Janabi na utaalam wake pale JKCI, ukimtoa awe peke yake, he is destined to fail. Ila kuwa kwenye organised system, success is inevitable.

We should be honest, Elimu ya vyuo vikuu na ma-prof waliopo hawana DNA na entrepreneurship ili kuzalisha waajiri.

Tunakwama kama taifa pale ambapo hata waziri ambae portfolio ya ajira iko chini yake hajui nini afanye.

To every problem in a given community Tanzania being inclusive, kuna watu wenye IQ na DNA ya kuja na sustainable solutions.
Ngoma ipo kwenye kuwang'amua. Ni mama madini; huwa yamefichwa chini kwenye ardhi au yako exposed juu y ardhi.

Kuweza kung'amua namna ya kubadili kilicho chini ya ardhi na kukigeuza kuwa hela nayo ni akili. Si kila mmoja anayo ila wapo ambao wanayo.

It's just needed a recognition ili hao watu wapewe nafasi ya kuonesha nini kifanyike ili wao wafaidike, serikali and the general public.

Napata tabu kwa namna ambayo out of box thinking haipo; kwa kuwa sheria na policy zilizo in place zimetungwa early 90 na kwa sasa hazifanyi kazi tena.

Innovation in most cases inavunja barriers kwa kuja na vitu vipya.

Kujiajiri kunazalisha tija kiasi kidogo sana unlike mfumo wa kuajiri/kuajiriwa.

Hapa Taifa lije na call ya search for brains which each individual or companies can create sa 100-500 fulltime employments kwa kutumia fursa za ndani na nje.

Kuna sehemu tutafika.
 
Wazo zuri, shida ipio kwenye kulitekeleza.
 
Mimi naomba sana wa-tanzania wapate nafasi ya kuwa wanamsikiliza huyu mtu kila anapokuwa anongea Bungeni.
 
Siyo wazo baya ila practically kuwambia vijana wajiajiri wakati anayeongea hayo aliajiriwa miaka nenda hadi kastaafu na badala ya kujiajiri kaingia bungeni inastajabisha kidogo. Kujiajiri siyo mchezo. Inataka dedication na uvumilivu wa hali ya juu. mtu mpaka utoboe uwe tayari kusota miaka mingi. Siyo kazi rahisi kujiajiri. na wengi wanaopiga kelele vijana wajiajiri wao wameajiriwa. Narudia siyo wzo baya ila ni vigumu sana kuliappy practically.
 
Ndio hii spirit tuwajengee watoto tangu Siku wanakanyaga shuleni usome ila kuna option mbili uajiriwe au ujiajiri..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…