Tetesi: Chato kuwa Mkoa au Magufuli Day kutangazwa rasmi na Rais Samia

Tetesi: Chato kuwa Mkoa au Magufuli Day kutangazwa rasmi na Rais Samia

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna tetesi kadhaa zimeanza kusambaa mitaa ya Chato tangu leo asubuhi kuwa, ujio wa Rais Samia katika Wilaya ya Chato katika kuadhimisha kumbukizi ya mwaka mmoja tangu kufariki dunia kwa rais Magufuli huenda kukaenda sambamba na mojawapo kati ya mambo mawili kama sio yote mawili, yaani Chato kupewa hadhi ya kuwa mkoa au tarehe 17/Machi kuwa siku ya mapumziko kitaifa (Magufuli day).

Lengo haswa ni kuenzi mema yaliyowahi kufanywa na Magufuli (kulinda legacy ya Magufuli) japokuwa wadadisi wanasema ni mbinu za Rais Samia kutafuta uungwaji mkono kutoka kanda ya ziwa baada ya kupata ukosoaji mkubwa kutoka kwa wakazi na wazawa wa mikoa ya kanda ya ziwa tangu aingie madarakani.

Kuhusu hoja kuwa ingepaswa kwanza kuwepo kwa Mkapa Day kabla ya kufikiria kuwepo Magufuli day, wapigia debe wa kuwepo Magufuli day wanasema kuwa, Magufuli alifariki akiwa madarakani jambo ambalo linajenga hoja ya upekee na msukumo wa kutaka uwepo wa siku maalum ya kumkumbuka Magufuli kwa kuwa kifo kilimkuta katikati ya jukumu la kuwatumikia watanzania.
 
Ikija kutokea kwa Hangaya tutakuwa tena Hangaya day kwakuwa ni Rais Mwanamke.
Haya mambo yakumbukizi yabaki kwa Nyerere tu.wanaofuata familia ziwe zinapewa hela kidogo kusafishia makaburi.Tukio la kesho linakula hela mingi sana
 
Kuna tetesi kadhaa zimeanza kusambaa mitaa ya Chato tangu leo asubuhi kuwa, ujio wa Rais Samia katika wilaya ya Chato katika kuadhimisha kumbukizi ya mwaka mmoja tangu kufariki dunia kwa rais Magufuli huenda kukaenda sambamba na mojawapo kati ya mambo mawili kama sio yote mawili, yaani Chato kupewa hadhi ya kuwa mkoa au tarehe 17/Machi kuwa siku ya mapumziko kitaifa (Magufuli day).

Lengo haswa ni kuenzi mema yaliyowahi kufanywa na Magufuli (kulinda legacy ya Magufuli) japokuwa wadadisi wanasema ni mbinu za Rais Samia kutafuta uungwaji mkono kutoka kanda ya ziwa baada ya kupata ukosoaji mkubwa kutoka kwa wakazi na wazawa wa mikoa ya kanda ya ziwa tangu aingie madarakani.

Kuhusu hoja kuwa ingepaswa kwanza kuwepo kwa Mkapa day kabla ya kufikiria kuwepo Magufuli day, wapigia debe wa kuwepo Magufuli day wanasema kuwa, Magufuli alifariki akiwa madarakani jambo ambalo linajenga hoja ya upekee na msukumo wa kutaka uwepo wa siku maalum ya kumkumbuka Magufuli kwa kuwa kifo kilimkuta katikati ya jukumu la kuwatumikia watanzania.
Hivi kuna Jambo jema kuwahi fanywa na magufuli, watanzania wengi hatujui, labda mauaji kuteka na kulawiti wakosoaji
 
Back
Top Bottom