Niliwahi kuleta uzi kuhusu hili jambo humu lakini kama kawaida yao mods walijitwalia madaraka wasiyokuwa nayo wakaufuta! Sijui ni uoga.. Sijui ni tudalili za udikteta.. Au ni kuminya mawazo mbadala sijuhi..!
Anyway iko hivi!
Kuna kitongoji kimoja kijijini kweli kweli, yaani very very remote na interior kilibahatika kumtoa mgombea ubunge..
Pamoja na upinzani mkali ndani na nje ya chama chake jamaa akasustain kura za kutosha.
Mara tu aliposhinda ubunge akaanza harakati za kujimilikisha jimbo lote liwe chini yake!
Alifanya rafu nyingi sana. Jimbo likapata hadhi ya kuwa wilaya kamili..!
Makao makuu yakajengwa ndani ya himaya ya familia yao!
Rafu zikaendelea zikaendelea mkoa mpya wa Geita ukalazimishwa kwa kumega maeneo ya mikoa mingine.
Lengo ni kuwakata ngebe na kuondokana na wapinzani wake (Mwanza na Kagera).
Pamoja na hayo upinzani ukazidi kukita mizizi yake ndani na nje ya chama chake..!
Yawezekana watu (hasa hasa mods) wasielewe namaanisha nini but kwa sasa ni dhahiri mubashara kuwa kitongoji chake kinaendelea kuwastawishwa kuliko hata makao makuu ya mkoa!
Hayo yote si bahati mbaya! Labda uwe mgeni wa siasa za hapa mkoani!
Yalianzia kwenye vibanda-umiza na vijiwe vya kahawa.. Lakini sasa ni wazi kuwa kuna mkoa mpya utaanzishwa hivi punde..
Na makao makuu ya huo mkoa mpya yatakuwa pale pale kwenye kitongoji yalipo makao makuu ya wilaya ya Chato!
Niliambiwa mkoa utaitwa Rubondo au jina linalokaribia kuwa sawa na hilo..!
Maandalizi yalishaanza na yameshika kasi.. hospitali, viwanda, vyuo, TRA, uwanja wa ndege, mabenki, n.k
Si ajabu smelters za makenikia pia zikajengwa pale kitongojini..!!
Uongozi wa Mkoa wa Geita kwa sasa umepigwa na butwaa!!!
Lengo kuu ni kuwakata ngebe na kuwanyamazisha wapinzani wetu..
Na hii ni awamu yetu!!
Itaendelea..!!