LGE2024 CHAUMMA yapata ushindi wa kiti 1 kati ya viti 181 Mbeya na kuwa chama pekee cha upinzani kilichopata ushindi mkoani humo

LGE2024 CHAUMMA yapata ushindi wa kiti 1 kati ya viti 181 Mbeya na kuwa chama pekee cha upinzani kilichopata ushindi mkoani humo

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Sana tena sana shida ya Chadema hizi vurugu sio jambo wa Tanzania wanapenda watu hawataki fujo wa Tanzania watu wakupenda raha nadhani muda muafaka wakirudi kwenye reli wakafanya siasa badala ya uanaharakati watafanikiwa kipindi pekee walifanya siasa baada ya kumchukua CCM Lowasa vs CCM walifanya siasa na walifanikiwa. Siasa za kufanya kama unagombania uhuru zimepitwa na wakati.
Walivyo wajinga wanadhani siasa aggressive zinaweza watoa Kwa hapa Tanzania,siasa za hivyo wakafanye Kenya.

Hapa Tanzania ni Bora ukashieikiana na chama Tawala kufanya saisa za kistaarabu watu watakuchagua na Wala hutokuwa na uadui na ccm Wala viongozi wa Serikali.

Ukiangalia siasa za Prof.J kama ataendelea na sera na ustaarabu ni rahisi sana kushinda kuliko kuwa na mafujo kama kina Sugu.

Maeneo yote ambako Chadema wameshinda ni wale wagombea ambao ni waungwana na wanakubalika na jamii,Sasa hizo ndio siasa za Tanzania Kwa Sasa.

Unaleta vurugu na malalamiko daily ijue imekukata.

Lowasa aliwasaisia Kwa sababu hiyo hiyo hajawahi kuwa na miliki Wala kutukana lakini ndio alivunja rekodi but Kwa walivyo wajinga Wameshindwa kusoma mood ya watu.
 
Hivi watu wapuuzi kama hao wasio na staha unaweza wasimamisha Kwa watu wastaarabu wakawachagua?

Sasa huo ni mfano mmja tuu,watu wa hivyo wasio na maadili Wala Heshima ndio walisimamishwa kushindana na CCM ambayo Ina wazee wenye Heshima zao wengine wamedumu kwa miaka 30.

Bahati mbaya sana uchaguzi wa Serikali za Mitaa tunatambuana
Ulionà msafara wa Mbowe pia ulimjumuisha Mh. Mdude?
Hàwa jàmaa wanafikiri kinyumbunyumbu tuu.
 
Mzee wa ubwawa wa Chauma Kwa mara ya kwanza amenyakua ushindi wa mgombea wake kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Mtaa Jijini Mbeya.

Ikumbuke Mbeya Kwa kina Sugu ndiko Chadema wanajifanyaga ni ngome Yao lakini Wameambulia Sifuri yaani zero huku nafasi zote zikienda Kwa Tulia-CCM na Chauma 😁😁😁😁.👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DC677rwoMNd/?igsh=cXg0ZXM5bXB2YWht

My Take:
Ukiweka Wagombea wenye staha na maadili Wananchi wanakuchagua maana Viongozi wa Mitaa tunaishi wote huku huku tunatambuana sio sawa na Wabunge au Madiwani Hadi tuhadithiwe.

Una akili zako timamu unaweza kuita huu ni uchaguzi kweli??
 
Mmh! kuna watu wana nguvu kubwa sana ya ushawishi siasani, nakumbuka miaka hiyo Rungwe mashariki (Busokelo sasa). Prof. Mwandosya akiwa kwenye kampeni, wazee wanamkataza yeye kujiombea kura wanaweka alama ya tick ardhini na wanamwambia "Mwandosya umepita baba".

Basi Mh. alikuwa anaishia kuwaombea kura diwani na rais(Mzee Kikwete) na kupiga stori zingine tu na raia.

Usishindane na aliyejaliwa
 
Ni Upuuzi wa Machadema na wewe,yaani Tulia aliyeibadilisha Mbeya Kwa miaka 5 apigwe chini uchague Mzee Sugu aliyekaa miaka 10 na hakuna alichofanya.?

Zama za ushabiki wa kijinga hazipo Kwa Sasa na bahati mbaya Machadema wamekalia hayo hayo.

Ngoja mwakani washikishwe adabu sawa sawa.
acha ushabiki we msisiemu. Unaamini ni kweli huyo mgombea awashinde ccm, chadema na act ambao wana trend? Hiyo ni political pattern, pale unaachia kule unabana huku ukijuja utaibuka na ushindi mkubwa. Hata uchaguzi mkuu ujao mbinu hii ya kugawa ushindi kidogokidogo kwa wapinzani itatumika vema ila ushindi mkubwa itakuwa ni kwa ccm.
 
acha ushabiki we msisiemu. Unaamini ni kweli huyo mgombea awashinde ccm, chadema na act ambao wana trend? Hiyo ni political pattern, pale unaachia kule unabana huku ukijuja utaibuka na ushindi mkubwa. Hata uchaguzi mkuu ujao mbinu hii ya kugawa ushindi kidogokidogo kwa wapinzani itatumika vema ila ushindi mkubwa itakuwa ni kwa ccm.
Watu wanachagua ku trend Kwa wagombea na Vyama vyenu au wanachagua mtu sahihi? Wahuni wenu wale nani anaweza kuwachagua? Huyo Jamaa wewe unamuinaje kwanza?

Baada ya kupigwa za uso visingizio buku 😂😂
 
Mitandao inadanganya sana.Vuguvugu la wanachadema jukwaa la siasa unaweza ukadhani mitaani Chadema wametapakaa kila kona,kumbe sio bana,,,dah!.
Humu jf kuanzia wenye jukwaa na Wafuasi wengi wa humu ni wanachadema Sasa ukiwajuta wanajitapa unaweza shanj huko mtaani ukivaa hata t shirt ya CCM utaoigwa mawe 😁😁

Wanaleta siasa za kipumbavu za kutukana mitandaoni Kwa Wananchi? Wacha wapewe za uso.
 
Mzee wa ubwawa wa Chauma Kwa mara ya kwanza amenyakua ushindi wa mgombea wake kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Mtaa Jijini Mbeya.

Ikumbuke Mbeya Kwa kina Sugu ndiko Chadema wanajifanyaga ni ngome Yao lakini Wameambulia Sifuri yaani zero huku nafasi zote zikienda Kwa Tulia-CCM na Chauma 😁😁😁😁.👇👇
View attachment 3164865
My Take:
Ukiweka Wagombea wenye staha na maadili Wananchi wanakuchagua maana Viongozi wa Mitaa tunaishi wote huku huku tunatambuana sio sawa na Wabunge au Madiwani Hadi tuhadithiwe.

======

WENYEVITI WA MITAA MBEYA WABEBESHWA JUKUMU LA WATOTO WA MITAAN.

Wenyeviti wa Mitaa 181 ya Jiji la Mbeya kutoka vyama vya CCM na CHAUMA pamoja na wajumbe 905 wanaounda uongozi wa serikali za Mitaa, wameapishwa baada ya zoezi la uchaguzi kukamilika na kutangazwa kuwa washindi kwenye nafasi hizo.

Wenyeviti hao 181, kati yao 180 wanatokana na chama cha mapinduzi CCM huku mmoja kati yao akitokana na chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA, wamehimizwa kuzitumia nafasi hizo vyema ikiwa ni pamoja na Kupambana na ongezeko la watoto wa mitaani.

Mohamed Aziz ni Katibu tawala wa Wilaya ya Mbeya, anasema Kama viongozi wa serikali za Mitaa wakishindwa kusimamia usalama kwenye Mitaa yao hakutakua na utulivu hivyo ni jukumu lao kuyasimamia hayo, huku msimamizi msaidizi wa uchaguzi Ally Nnunduma akiwataka kuchangia mawazo yao katika maendeleo ya Jiji la Mbeya.

Nae mwenyekiti pekee anayetokana na chama cha ukombozi wa Umma, (CHAUMA) Brayan Mwakalukwa kutoka mtaa wa Soko kata ya Ruanda amesema anayofuraha kubwa kushinda nafasi ya mwenyekiti kupitia Chama hicho na anaahidi kutoa ushirikiano kwa wenyeviti wenzake, Diwani wa kata Ruanda na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt Tulia Ackson.
Mods wapuuzi sana,Kwa nini mnabadilisha heading wakati my interest ilikuwa ni CHAUMA chama Cha Ubwabwa? 👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DDAHB-5N9Pb/?igsh=Ynh0cDZrYmVwZ2w5
 
Kuna wakati nilikuwa nasikia kelele mitandaoni eti Tulia amekalia kuti kavu kwenye jimbo Sugu anasubiri kuapishwa.

Mitandao inawadanganya sana Chadema.
uchaguz huu mpk polisi wanaua wapinzan nao unauamin?
 
Back
Top Bottom