LGE2024 CHAUMMA yapata ushindi wa kiti 1 kati ya viti 181 Mbeya na kuwa chama pekee cha upinzani kilichopata ushindi mkoani humo

LGE2024 CHAUMMA yapata ushindi wa kiti 1 kati ya viti 181 Mbeya na kuwa chama pekee cha upinzani kilichopata ushindi mkoani humo

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Mzee wa ubwawa wa Chauma Kwa mara ya kwanza amenyakua ushindi wa mgombea wake kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Mtaa Jijini Mbeya.

Ikumbuke Mbeya Kwa kina Sugu ndiko Chadema wanajifanyaga ni ngome Yao lakini Wameambulia Sifuri yaani zero huku nafasi zote zikienda Kwa Tulia-CCM na Chauma 😁😁😁😁.👇👇
View attachment 3164865
My Take:
Ukiweka Wagombea wenye staha na maadili Wananchi wanakuchagua maana Viongozi wa Mitaa tunaishi wote huku huku tunatambuana sio sawa na Wabunge au Madiwani Hadi tuhadithiwe.

======

WENYEVITI WA MITAA MBEYA WABEBESHWA JUKUMU LA WATOTO WA MITAAN.

Wenyeviti wa Mitaa 181 ya Jiji la Mbeya kutoka vyama vya CCM na CHAUMA pamoja na wajumbe 905 wanaounda uongozi wa serikali za Mitaa, wameapishwa baada ya zoezi la uchaguzi kukamilika na kutangazwa kuwa washindi kwenye nafasi hizo.

Wenyeviti hao 181, kati yao 180 wanatokana na chama cha mapinduzi CCM huku mmoja kati yao akitokana na chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA, wamehimizwa kuzitumia nafasi hizo vyema ikiwa ni pamoja na Kupambana na ongezeko la watoto wa mitaani.

Mohamed Aziz ni Katibu tawala wa Wilaya ya Mbeya, anasema Kama viongozi wa serikali za Mitaa wakishindwa kusimamia usalama kwenye Mitaa yao hakutakua na utulivu hivyo ni jukumu lao kuyasimamia hayo, huku msimamizi msaidizi wa uchaguzi Ally Nnunduma akiwataka kuchangia mawazo yao katika maendeleo ya Jiji la Mbeya.

Nae mwenyekiti pekee anayetokana na chama cha ukombozi wa Umma, (CHAUMA) Brayan Mwakalukwa kutoka mtaa wa Soko kata ya Ruanda amesema anayofuraha kubwa kushinda nafasi ya mwenyekiti kupitia Chama hicho na anaahidi kutoa ushirikiano kwa wenyeviti wenzake, Diwani wa kata Ruanda na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt Tulia Ackson.

View: https://www.instagram.com/reel/DDADK0HIyvb/?igsh=ajJtc3Q0aGowZ29k

Hapa tukijadili ushindi wa CCM tunapoteza tu muda,kwa yanayoendelea ni dhahiri CCM inajidhihirisha kuwa ni chama cha majambazi.Na kimejionesha hivyo maana kinaiba kura ,kinauwa watu ,kinateka,kinatesa,na mengine mengi ya kuumiza na kusikitisha.Je hii ndio CCM aliyoiasisi mwalimu Nyerere kweli.
 
Hapa tukijadili ushindi wa CCM tunapoteza tu muda,kwa yanayoendelea ni dhahiri CCM inajidhihirisha kuwa ni chama cha majambazi.Na kimejionesha hivyo maana kinaiba kura ,kinauwa watu ,kinateka,kinatesa,na mengine mengi ya kuumiza na kusikitisha.Je hii ndio CCM aliyoiasisi mwalimu Nyerere kweli.
Mlidhani Watanzania watawachagua Kwa kuimba pipoozi power na kuzungusha ngumi? 😆😆😆😆

Kamanda wa mchongo unafeli wapi?
 
Na wewe Kwa akili zako za kushikiwa ulitegemea Machadema yatasema yameshindwa? Kwamba watu waliokosa Hadi wagombea na mawakala ndio wanaweza shindana na maccm wazoefu na wabobesi kala Hawa ? 👇👇View attachment 3166017

Ambako hawakuenguliwa ilikuaje? Hujasikia wameshinda Baadhi ya maeneo? Kwa nini washinde huko ?

Mwisho Kuna uchaguzi usio na taratibu? Kama walienguliwa Kwa kuonewa Kwa nini hawakwenda kusimamisha uchaguzi mahakamani?

Tunaimba na uchaguzi wa mwakani wakurupuke tena waone moto 🤣🤣
Wewe unafikiri mtakubali kwamba maeneo mengi 'mlifunga mabao ya mkono'?
 
Duh!
Yaani jamaa alitaka kuanza kumshukuru Mungu, ghafla akagundua kakosea, akabadilisha, akamshukuru Samiah.
 
Kuna wakati nilikuwa nasikia kelele mitandaoni eti Tulia amekalia kuti kavu kwenye jimbo Sugu anasubiri kuapishwa.

Mitandao inawadanganya sana Chadema.
Polisi wa nini na mitutu mitaani wakati wa uchaguzi ili tuamini hicho mnacho kisema?
 
Ni Upuuzi wa Machadema na wewe,yaani Tulia aliyeibadilisha Mbeya Kwa miaka 5 apigwe chini uchague Mzee Sugu aliyekaa miaka 10 na hakuna alichofanya.?

Zama za ushabiki wa kijinga hazipo Kwa Sasa na bahati mbaya Machadema wamekalia hayo hayo.

Ngoja mwakani washikishwe adabu sawa sawa.
Uhakika zaidi ni pale SUGU vs TULIA. Halafu mazingira yawe yanavyopaswa kuwa bila makandokando. Jibu litapatikana baada ya hapo. Kinyume na hapo itakuwa ni hisia tu ktk kuhukumu.
 
Uhakika zaidi ni pale SUGU vs TULIA. Halafu mazingira yawe yanavyopaswa kuwa bila makandokando. Jibu litapatikana baada ya hapo. Kinyume na hapo itakuwa ni hisia tu ktk kuhukumu.
Mtapigwa kama mlivyopigwa kwe Serikali za Mitaa.

Endeleeni kunidanganya huyo baby yenu Ili mumlie pesa zenu wakati hawezi kuwa Mbunge.
 
Back
Top Bottom