Facts!wote ni hot garbage. Taka mbichi.
Waliondoka kwasababu zao tofautiWamekupa majibu gani?
wivu utakuuaFacts!
Tanzania imeanza kupeleka wanahabari wa odhaa ya Kiswahili nje ya nchi toka uhuru. Nani alirudi anafanana na waandishi wa BBC?
Waandishi wa idhaa za Kiswahili kimsingi ni wakalimani tu, habari zote zinatengenezwa na Wazungu, kazi yao kuzitapika kama zilivyo ila kwa Kiswahili. Hawana editorial leeway. Hawawezi kujifunza chochote, wanarudi kama walivyoondoka.
Mungalieni Charles Hillary, kwa mfano. Amerudi na uweledi gani yule mwenzetu ?
Mtu bila mbavu hawezi kuishi!Mpumbavu wewe,Mimi nilikuwa najaribu kumuonesha makosa ya kimaandishi aliyoyafanya kwa sababu si kweli kwamba wanalipwa mamilioni ya paundi kwa mwezi huko BBC kama alivyoandika mwandishi labda angesema hizo paundi wanazolipwa ukija kuzibadilisha kwa hela ya Bongo ndio utapata hayo mamilioni(kwa Tshs).
Uwe unatumia akili sio kukurupuka tu kama nyumbu.
Diploma ya Kilimo aliisoma akiwa hapa kabla hajaenda Ulaya! Alijiendeleza baadae! Na hivi mnachukuliaje Salim nyie wabongo?!Hana degree yule wewe.Ana diploma ya chuo cha kilimo Tangeru. Yule amalize Masters UK na aspost picha akiwa na Joho la graduation na kupost cheti chake ?
Hata kuandika hujui... unaonesha hujielewi. Kaa hivyohivyo na ujinga wako wa kukariri.Unamaliza shule na F4, unataka akasema msemaji wa Serikali ipi?
Wengine wanalipwa kiasi gani? Huna data unapinga tu?Umeandika vizuri sana isipokua kwenye kulipwa mamilioni ya paundi.
BBC ina matangazo ya lugha nyingi sana, kwenye Radio na kwenye Tv wana channel nyingi.
Anaelipwa paundi milioni ni mmoja tu Gary Lineker analipwa £ 1.35m kwa mwaka. Kipindi chake pendwa kinaitwa MATCH OF THE DAY.
Probably possible, maana CCM Kwa fitina Wana dunia yaoKama aliwahi kuwaharibia akiwa huko basi wamelipa kisasi.. CCM wana tabia ya kulea kisasi hawasahau na hawajui kusamehe
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna siri ndugu, wanasagana waleKuna yasirini nasikia ndio maana yupo hapo.
Waafrika hasa watanzania wana laana.Kwa mtu mwenye maarifa hawezi kutoa kashfa kama hizi kwa mwenzake kwa sababu tu ya chuki binafsi
Labda niulize tu; Kwani huko BBC alijipa kazi mwenyewe au lile ni shirika la ndugu yake???
By the way, angekuwa hafanyi vizuri wangempandisha ngazi kiasi kile?
kuweni basi na kiasi tunapo ongelea maisha ya mtu (mwenzetu)
Baadhi ya Watanzania tuna hulka ya kuoneana wivu sana na ndio sababu watu hawasaidiani, badala yake tuna achia majirani zetu wanachukua fursa zote nzuri huko nje sisi tukiendelea kupiga domo kwa kuchafuana....
Mamilioni ya pounds Kwa mwezi si billion Kwa Bongo,Kumbe wale waswahili wenzetu watangazaji wa idhaa ya kiswahili ya BBC wanalipwa mamilioni ya paundi ya Uingereza kila mwezi!
Kilichomuingiza BBC ni nini??Kikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Hata Muhuza alikwenda BBC usishangae kuingia shangaa kwanini katoka.Kilichomuingiza BBC ni nini??
Mmmmh sijui kwa kweli.Hakuna siri ndugu, wanasagana wale
Uchawa ni hasara tupu. Unapata furaha ya Muda tuHakuna salamu hapa, naingia kwenye mada moja kwa moja. Kama ilivyokuwa kwa Tido Mhando aliyetolewa BBC na kuletwa kusimamia TBC, ndivyo ilivyokuwa kwa Salim Kikeke. Taarifa za kiintelejensia zinapenya kuwa ndugu Kikeke aliombwa kung’atuka BBC ili arudi nchini kuandaliwa kuwa msemaji wa serikali. Baada ya kufika nchini alisubiri kwa muda mama aachie nafasi ya uteuzi bila mafanikio. Ndipo akaamua kwenda kujishikiza pale EFM ili mama akipangua nafasi za uteuzi yeye ateuliwe kuwa msemaji wa serikali. Inavyoonekana ni kama vetting bado ilikuwa haijakamilika.
Baadaye upekuzi ulipofanyika kwa kina zaidi, ikaonekana nafasi ya usemaji wa serikali haitamfaa. Nafasi ile inamfaa mtu muongeaji na mwenye uwezo wa kuelekezwa kusema uongo akatoka hadharani kuusema na kuutetea kwa macho makavu. Kikeke ni mtu wa msimamo na asiyefundishwa nini cha kuongea. Ni mtu mwenye kusimamia maadili ya habari na anamuogopa Mungu. Ni vigumu sana kumwambia aende hadharani kusema uongo kwa lengo tu la kutetea jambo au madudu ya serikali.
Hiki ndiko kilichomponza kijana wa watu licha ya kushawishiwa kurudi nyumbani apewe kazi na serikali lakini kazi aliyoahidiwa amekuja kupewa mtu mwingine. Wafanyakazi wa BBC huwa wanafundishwa maadili ktk taaluma ya habari yanawafanya waive sawasawa na kutokubali kuyumbishwa.
Tukumbuke pia Tido Mhando misimamo yake ni sawa na ya Kikeke. Tido aliombwa kurudi nchini akapewa TBC. Baada ya kunyesha msimamo usioyumba katika kusimamia ukweli kwenye habari, serikali ikamtupa nje na kisha kumfungulia kesi ya bandia ya uhujumu uchumi. Mpaka sasa nadhani hiyo kesi anateseka nayo mahakamani.
Kumbuka mtu kaacha kazi BBC anakolipwa mamilioni ya paundi za kingereza anashawishiwa kurudi nyumbani apewe kazi nzuri halafu hapewi! Hii sio sawa. Kama kazi hakuna au huna uhakika wa kumpa kazi, ni bora wangemuacha abaki BBC aendelee kuvuna paundi zake angerudi nyumbani afungue media awaajiri vijana wenzake.
Tazama mfano wa Abdalla Bulembo Majura aliyevuna paundi za kutosha akiwa BBC aliporudi nyumbani amefungua kituo cha redio ABM FM kule Dodoma amewaajiri vijana wa kitanzania wanapata ridhiki zao za kila siku bila tatizo. Kama Kikeke angeachwa aendelee kukaa BBC hadi astaafu angerudi nchini akiwa na paundi za kutosha akafungua kituo cha TV au redio akawaajiri vijana wenzake. Sio haki kumuahidi mtu kuacha kazi ya pesa nyingi halafu anarudi nyumbani kwa matumaini ya kupewa kazi, anatoswa mazima. Tabia hii sio nzuri na haitoi mfano mzuri kwa vijana wachapa kazi kama Kikeke.
USHAURI WANGU
Naishauri serikali impangie kazi nyingine ndugu Salim Kikeke kwa kuwa wameamua kugawa nafasi yake kwa mtu mwingine kinyume na makubaliano. Huu mchezo wa kutosana ukiendelea, itakuwa vigumu kuwashawishi vijana wezalendo kutoka ughaibuni kurudi nyumbani kuitumikia nchi yao. Nchi hii ni yetu sote, sio mali ya kikundi fulani cha watu.
Nawasilisha.
Punguza makasiriko Mzee,Facts!
Tanzania imeanza kupeleka wanahabari wa odhaa ya Kiswahili nje ya nchi toka uhuru. Nani alirudi anafanana na waandishi wa BBC?
Waandishi wa idhaa za Kiswahili kimsingi ni wakalimani tu, habari zote zinatengenezwa na Wazungu, kazi yao kuzitapika kama zilivyo ila kwa Kiswahili. Hawana editorial leeway. Hawawezi kujifunza chochote, wanarudi kama walivyoondoka.
Mungalieni Charles Hillary, kwa mfano. Amerudi na uweledi gani yule mwenzetu ?
WEWE NI MPUMBAVU!
USIPENDE KUONGELEA WATU USIOWAJUA NA KUWACHUKULIA POA!
YULE SIO MWENZIO HATA KIDOGO NA HII INAONESHA DHAHIRI WABONGO NI WAKURUPUKAJI WA KUONGEA VITU MSIVYOVIJUA...
SALIM KIKEKE ANA DEGREE ZAIDI YA MOJA NA MASTERS ALIYOISOMEA UINGEREZA KIPINDI YUKO ULAYA MIAKA MINGI. KASOMEA SIASA ZA KIMATAIFA NA NAMNA YA KU-RESOLVE MIGOGORO YA KISIASA YA KIMATAIFA. BISHANA NIKUTAJIE MPAKA NA CHUO NA MAHALA KILIPO NA PICHA YAKE AKIWA AMEHITIMU. MEDIA ZA KIMATAIFA HAZICHUKUI WATU ANGALAU WASIO NA DEGREE! TENA ZA KIMATAIFA... POLE KAMA ULIHISI YULE NI MWENZIO AU WALE WANAOKAA PALE NI WENZIO
TENA POLE SANA!
Masters kasoma wapi?! Au muulize hakuna course yoyote alisoma nje?!We muongo, nina rafiki yupo BBC kasoma SAUT au nacho kina Degree za Kimataifa (kwanza ni zipi hizo)