Checkmate: Ndege mpya ya kivita ya Urusi inayoikosesha Marekani usingizi

Checkmate: Ndege mpya ya kivita ya Urusi inayoikosesha Marekani usingizi

mohamedidrisa789

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2015
Posts
5,258
Reaction score
22,552
Siku ya Jumanne, Urusi ilizindua ndege yake mpya ya kivita na inayoweza kufanya misheni za kijasusi ya Sukhoi "Checkmate" katika onyesho la ndege mbele ya Rais Vladimir Putin.

Habari juu ya muundo na uwezo wa ndege hii ya kivita ya kizazi cha tano ilitolewa kwenye onyesho la anga la Max-2021 lililofanyika Zhukovsky nje ya Moscow.

Ndege hii ya kivita inachukuliwa kuwa mshindani wa ndege ya kijeshi ya Marekani yenye uwezo wa kujificha F-35 na Urusi imepanga kuiuza kwa nchi nyingi ulimwenguni.

Checkmate imetengenezwa na kampuni kubwa inayomilikiwa na serikali Rostec na Shirika la Ndege la United


"Checkmate" ni nini?

Kulingana na habari zilizopo, ndege hii ya kivita ya Checkmate ni nyepesi kuliko ndege ya injini-mbili ya Sukhoi Su-57 na inaweza kubeba makombora matano ya hewani kwa safu tofauti.

Ndege hii ina uwezo wa kuzindua droni wakati ikiwa hewani na kubeba jumla ya tani 7.5 za silaha.

Checkmate inahitaji barabara fupi sana ili kupaa au kutua hiyo inachukuliwa kuwa sifa maalum ya ndege hii.

Ndege hiyo imetengenezwa kama ndege ya kivita ya kizazi kipya yenye injini moja na utumiaji teknolojia ya kisasa inahesabiwa kati ya nguvu zake kuu.
Watengenezaji wa ndege hiyo wanasema kuwa teknolojia ya kisasa inayotumiwa katika Checkmate inafanya kazi kama rubani mwenza na itamsaidia rubani mkuu katika hali za kupigana.

Kulingana na watengezaji wa ndege hii, inaweza kupiga hadi malengo sita juu ya ardhi, hewani au baharini kwa wakati mmoja na inafanya kazi hata inapokabiliwa na usumbufu mkubwa wa kielektroniki.

Checkmate itagharimu karibu dola milioni 25 hadi 30 za Kimarekani. Baada ya majaribio ya ardhini, ndege hii itafanya safari yake ya kwanza mnamo 2023 na Urusi itaanza kuiuza kwa nchi mbali mbali kutoka 2026.

United Aircraft Corporation imesema inapanga kutengeza ndege 300 aina ya Checkmate katika kipindi cha miaka 15 ijayo. Kulingana na kampuni hiyo, idadi ya 300 imekadiriwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndege hii.

Watengenezaji wa Checkmate pia wanafanya kazi kutengeneza toleo la ndege hii ambalo halitahitaji rubani.





images%20(6).jpg
images%20(1).jpg
images%20(4).jpg
images%20(2).jpg
images%20(5).jpg


Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Siku ya Jumanne, Urusi ilizindua ndege yake mpya ya kivita na inayoweza kufanya misheni za kijasusi ya Sukhoi "Checkmate" katika onyesho la ndege mbele ya Rais Vladimir Putin.

Habari juu ya muundo na uwezo wa ndege hii ya kivita ya kizazi cha tano ilitolewa kwenye onyesho la anga la Max-2021 lililofanyika Zhukovsky nje ya Moscow.

Ndege hii ya kivita inachukuliwa kuwa mshindani wa ndege ya kijeshi ya Marekani yenye uwezo wa kujificha F-35 na Urusi imepanga kuiuza kwa nchi nyingi ulimwenguni.

Checkmate imetengenezwa na kampuni kubwa inayomilikiwa na serikali Rostec na Shirika la Ndege la United


"Checkmate" ni nini?

Kulingana na habari zilizopo, ndege hii ya kivita ya Checkmate ni nyepesi kuliko ndege ya injini-mbili ya Sukhoi Su-57 na inaweza kubeba makombora matano ya hewani kwa safu tofauti.

Ndege hii ina uwezo wa kuzindua droni wakati ikiwa hewani na kubeba jumla ya tani 7.5 za silaha.

Checkmate inahitaji barabara fupi sana ili kupaa au kutua hiyo inachukuliwa kuwa sifa maalum ya ndege hii.

Ndege hiyo imetengenezwa kama ndege ya kivita ya kizazi kipya yenye injini moja na utumiaji teknolojia ya kisasa inahesabiwa kati ya nguvu zake kuu.
Watengenezaji wa ndege hiyo wanasema kuwa teknolojia ya kisasa inayotumiwa katika Checkmate inafanya kazi kama rubani mwenza na itamsaidia rubani mkuu katika hali za kupigana.

Kulingana na watengezaji wa ndege hii, inaweza kupiga hadi malengo sita juu ya ardhi, hewani au baharini kwa wakati mmoja na inafanya kazi hata inapokabiliwa na usumbufu mkubwa wa kielektroniki.

Checkmate itagharimu karibu dola milioni 25 hadi 30 za Kimarekani. Baada ya majaribio ya ardhini, ndege hii itafanya safari yake ya kwanza mnamo 2023 na Urusi itaanza kuiuza kwa nchi mbali mbali kutoka 2026.

United Aircraft Corporation imesema inapanga kutengeza ndege 300 aina ya Checkmate katika kipindi cha miaka 15 ijayo. Kulingana na kampuni hiyo, idadi ya 300 imekadiriwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndege hii.

Watengenezaji wa Checkmate pia wanafanya kazi kutengeneza toleo la ndege hii ambalo halitahitaji rubani.





View attachment 1865036View attachment 1865037View attachment 1865038View attachment 1865040View attachment 1865041

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Gharam 25m usd , ingekuwa marekani tungeambiwa 2b usd
 
Siku ya Jumanne, Urusi ilizindua ndege yake mpya ya kivita na inayoweza kufanya misheni za kijasusi ya Sukhoi "Checkmate" katika onyesho la ndege mbele ya Rais Vladimir Putin.

Habari juu ya muundo na uwezo wa ndege hii ya kivita ya kizazi cha tano ilitolewa kwenye onyesho la anga la Max-2021 lililofanyika Zhukovsky nje ya Moscow.

Ndege hii ya kivita inachukuliwa kuwa mshindani wa ndege ya kijeshi ya Marekani yenye uwezo wa kujificha F-35 na Urusi imepanga kuiuza kwa nchi nyingi ulimwenguni.

Checkmate imetengenezwa na kampuni kubwa inayomilikiwa na serikali Rostec na Shirika la Ndege la United


"Checkmate" ni nini?

Kulingana na habari zilizopo, ndege hii ya kivita ya Checkmate ni nyepesi kuliko ndege ya injini-mbili ya Sukhoi Su-57 na inaweza kubeba makombora matano ya hewani kwa safu tofauti.

Ndege hii ina uwezo wa kuzindua droni wakati ikiwa hewani na kubeba jumla ya tani 7.5 za silaha.

Checkmate inahitaji barabara fupi sana ili kupaa au kutua hiyo inachukuliwa kuwa sifa maalum ya ndege hii.

Ndege hiyo imetengenezwa kama ndege ya kivita ya kizazi kipya yenye injini moja na utumiaji teknolojia ya kisasa inahesabiwa kati ya nguvu zake kuu.
Watengenezaji wa ndege hiyo wanasema kuwa teknolojia ya kisasa inayotumiwa katika Checkmate inafanya kazi kama rubani mwenza na itamsaidia rubani mkuu katika hali za kupigana.

Kulingana na watengezaji wa ndege hii, inaweza kupiga hadi malengo sita juu ya ardhi, hewani au baharini kwa wakati mmoja na inafanya kazi hata inapokabiliwa na usumbufu mkubwa wa kielektroniki.

Checkmate itagharimu karibu dola milioni 25 hadi 30 za Kimarekani. Baada ya majaribio ya ardhini, ndege hii itafanya safari yake ya kwanza mnamo 2023 na Urusi itaanza kuiuza kwa nchi mbali mbali kutoka 2026.

United Aircraft Corporation imesema inapanga kutengeza ndege 300 aina ya Checkmate katika kipindi cha miaka 15 ijayo. Kulingana na kampuni hiyo, idadi ya 300 imekadiriwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndege hii.

Watengenezaji wa Checkmate pia wanafanya kazi kutengeneza toleo la ndege hii ambalo halitahitaji rubani.





View attachment 1865036View attachment 1865037View attachment 1865038View attachment 1865040View attachment 1865041

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Acha kuongeza maneno wapi wameandika USA kakosa usingizi kwa ndege ambayo imecopiwa kutoka kwenye ndege yake mwenyewe ya f35...hiyo ndege ni mapema kuisifia kwa sababu hakuna sehemu imeshawahi kuingia mzigoni wala parformance yake kiuhalisia haijajulikana kwa maana ya kuingia vitani lakini ndege zote zinasosifiwa leo duniani zipo mzigoni na zimepimwa kwa kazi vitani kuanzia f22 mpaka f35 lakini hiyo ya mrusi imeingia vitani wapi? Punguza mahaba mkuu ndege vita inapimwa kwenye uwanja wa mapambano sio showroom
 
Acha kuongeza maneno wapi wameandika USA kakosa usingizi kwa ndege ambayo imecopiwa kutoka kwenye ndege yake mwenyewe ya f35...hiyo ndege ni mapema kuisifia kwa sababu hakuna sehemu imeshawahi kuingia mzigoni wala parformance yake kiuhalisia haijajulikana kwa maana ya kuingia vitani lakini ndege zote zinasosifiwa leo duniani zipo mzigoni na zimepimwa kwa kazi vitani kuanzia f22 mpaka f35 lakini hiyo ya mrusi imeingia vitani wapi? Punguza mahaba mkuu ndege vita inapimwa kwenye uwanja wa mapambano sio showroom
😄😄😄
 
Su-75 Checkmate sio ya kutisha sana hata. Waingereza wanakuja na 6th generation jet inaitwa Tempest, Wakorea kusini wanakuja na 5th generation jet, Wajapan wanaileta 5th generation yao. Hizi zote naamini zitaizidi Checkmate

China inazo stealth J-20 na kuna nyingine inatengengezwa na Shenyang kwa ajili ya Navy. Hawa wakizipa injini kamili nazo zitakuwa na maana kuliko Su-75

US wana F-22 na F-35 ziko kamilifu na Checkmate haiwezi zikaribia. Su-57 ndio itashindana nazo ila nayo haijapata powerful engine ya Izdeliye 30, kwa sasa inatumia AL-41 ambayo haifiki supersonic speed bila afterburners na haiko stealth

US pia wana NGAD (Next Generation Air Dominance) iko mbioni ilikuwa siri mpaka mwaka huu. Muhimu zaidi US wana advanced secure datalink kamili kuliko Urusi ingawa mpaka leo F-22 na F-35 haziwezi communicate ni mpaka zitumie relay nyingine mfano kupitia U-2 reconnaissance plane. Datalink inasaidia kushare target na guidance ya radar, etc. Bado wana projects kadhaa za stealth drones

Checkmate inaletwa kama stealth flani ya kuwauzia wateja wasio na uwezo wa kumudu gharama kubwa za stealth jets zilizoko sokoni, au wateja wasioruhusiwa kunua stealth zilizopo mfano Turkey ambayo inakufa na project yake ya stealth jet pia. Ikumbukwe Su-57 haijapata foreign customers na bado iko kwenye development, mpaka ifikie maturity sio leo. Checkmate wanadai mpaka 2022 utaanza initial production ila siwaamini Warusi huwa wana estimations za uongo. Checkmate ndio ndege pekee ya Urusi kwenye karne ya 21 iliyotengenezwa kwa lengo la wateja tu, hata jeshi lao halijui kama ipo

Possible customers wa Checkmate ni kama Algeria, Egypt na India lakini haitakiwi ichelewe. Na hilo jina litabadilishwa, wakati Sukhoi wanatengeneza Su-57 walikuwa wanaiita PAK-FA ila MoD ikaibadili jina ilipotoa order

Mambo ni mengi
 
Su-75 Checkmate sio ya kutisha sana hata. Waingereza wanakuja na 6th generation jet inaitwa Tempest, Wakorea kusini wanakuja na 5th generation jet, Wajapan wanaileta 5th generation yao. Hizi zote naamini zitaizidi Checkmate

China inazo stealth J-20 na kuna nyingine inatengengezwa na Shenyang kwa ajili ya Navy. Hawa wakizipa injini kamili nazo zitakuwa na maana kuliko Su-75

US wana F-22 na F-35 ziko kamilifu na Checkmate haiwezi zikaribia. Su-57 ndio itashindana nazo ila nayo haijapata powerful engine ya Izdeliye 30, kwa sasa inatumia AL-41 ambayo haifiki supersonic speed bila afterburners na haiko stealth

US pia wana NGAD (Next Generation Air Dominance) iko mbioni ilikuwa siri mpaka mwaka huu. Muhimu zaidi US wana advanced secure datalink kamili kuliko Urusi ingawa mpaka leo F-22 na F-35 haziwezi communicate ni mpaka zitumie relay nyingine mfano kupitia U-2 reconnaissance plane. Datalink inasaidia kushare target na guidance ya radar, etc. Bado wana projects kadhaa za stealth drones

Checkmate inaletwa kama stealth flani ya kuwauzia wateja wasio na uwezo wa kumudu gharama kubwa za stealth jets zilizoko sokoni, au wateja wasioruhusiwa kunua stealth zilizopo mfano Turkey ambayo inakufa na project yake ya stealth jet pia. Ikumbukwe Su-57 haijapata foreign customers na bado iko kwenye development, mpaka ifikie maturity sio leo. Checkmate wanadai mpaka 2022 utaanza initial production ila siwaamini Warusi huwa wana estimations za uongo. Checkmate ndio ndege pekee ya Urusi kwenye karne ya 21 iliyotengenezwa kwa lengo la wateja tu, hata jeshi lao halijui kama ipo

Possible customers wa Checkmate ni kama Algeria, Egypt na India lakini haitakiwi ichelewe. Na hilo jina litabadilishwa, wakati Sukhoi wanatengeneza Su-57 walikuwa wanaiita PAK-FA ila MoD ikaibadili jina ilipotoa order

Mambo ni mengi
Sasa Japana akiwa na mandenge, chin ana mandege, na Korea kusini naye akiwa nayo. Hilo eneo si litakuwa la moto sana?
 
Sasa Japana akiwa na mandenge, chin ana mandege, na Korea kusini naye akiwa nayo. Hilo eneo si litakuwa la moto sana?
Asia pa moto ni kama Middle East. Tofauti ni kwamba Middle East kuna giants wawili Iran na Israel wengine ni wacheza ngoma inayopigwa, ila Asia-Pacific hasa Southern China sea kuna migogoro ya wakubwa mingi baina ya China vs Japan, China vs India, China vs Philippines, North Korea (DPRK) vs South Korea (ROK), China mainland (PRC) vs China ya uhamishoni (Taiwan). Pia Japan ana claims kwenye visiwa vya Kuril vya Russia. Australia nayo inajaribu kujiingiza kuitia pressure China. Marekani ndio kabisa ana bases kadhaa kuzunguka pale

Hao wagomvi wote wana uwezo wa kutengeneza silaha na wana uchumi mzuri. Silaha ambazo ni advanced sana ndio wananunua au wana-licence produce. Alafu migogoro yao sio ya kijinga kama Middle East walivyo: ukitazama Saudi Arabia vs Qatar ni wivu, Iran vs Israel ni dini, wengineo wanaburuzwa na idea ya kuiondoa Israel wamebaki nayo Wapalestina na Iran tu.
Kule Asia kila nchi inapigania mipaka yake, huu ni ugomvi mkubwa sio masihara
 
Ni kweli hiyo Checkmate haijajaribiwa popote ili kufahamu uthabiti wake. Siku hizi warusi wamekuwa watu wa mikwara sana.

Kuna kipindi miaka kadhaa nyuma walikuja na fix moja kali sana kwamba wamevumbua kombora moja isiyofuata "Trajectory"..!!! Kwamba ina uwezo wa kupiga piga kona hadi kwenda kupiga target...!!!
 
Back
Top Bottom