Checkmate: Ndege mpya ya kivita ya Urusi inayoikosesha Marekani usingizi

Checkmate: Ndege mpya ya kivita ya Urusi inayoikosesha Marekani usingizi

Ni kweli hiyo Checkmate haijajaribiwa popote ili kufahamu uthabiti wake. Siku hizi warusi wamekuwa watu wa mikwara sana.

Kuna kipindi miaka kadhaa nyuma walikuja na fix moja kali sana kwamba wamevumbua kombora moja isiyofuata "Trajectory"..!!! Kwamba ina uwezo wa kupiga piga kona hadi kwenda kupiga target...!!!
Hayo makombora mbona yapo. Marekani wanazo Tomahawk ni ship launched cruise missiles waliyafanyia modifications kitambo kidogo kwa sasa yanatumia terrain following. Yanapita chini kabisa mita chache kutoka ardhini ili yakwepe radar, katika hali hii yanakuwa hatarini kugonga milima hivo yanatumia terrain following kusogelea target na yanapita anga za mabondeni tu ili yazuiliwe na milima yasionekane kwa radar. Kampuni za Raytheon na General Dynamics walipiga kazi sana hapa kuyapa uwezo huu

Urusi wanayo ya Kalibr family wametoa kwenye 2010s ni submarine launched na ship launched, nazo zinafanya kazi kama Tomahawk. Tomahawk yametumika sana vita ya Saddam Hussein na Kalibr yamekuwa tested nchini Syria dhidi ya ISIS
 
Asia pa moto ni kama Middle East. Tofauti ni kwamba Middle East kuna giants wawili Iran na Israel wengine ni wacheza ngoma inayopigwa, ila Asia-Pacific hasa Southern China sea kuna migogoro ya wakubwa mingi baina ya China vs Japan, China vs India, China vs Philippines, North Korea (DPRK) vs South Korea (ROK), China mainland (PRC) vs China ya uhamishoni (Taiwan). Pia Japan ana claims kwenye visiwa vya Kuril vya Russia. Australia nayo inajaribu kujiingiza kuitia pressure China. Marekani ndio kabisa ana bases kadhaa kuzunguka pale

Hao wagomvi wote wana uwezo wa kutengeneza silaha na wana uchumi mzuri. Silaha ambazo ni advanced sana ndio wananunua au wana-licence produce. Alafu migogoro yao sio ya kijinga kama Middle East walivyo: ukitazama Saudi Arabia vs Qatar ni wivu, Iran vs Israel ni dini, wengineo wanaburuzwa na idea ya kuiondoa Israel wamebaki nayo Wapalestina na Iran tu.
Kule Asia kila nchi inapigania mipaka yake, huu ni ugomvi mkubwa sio masihara
Upo vizuri hongera
 
Acha kuongeza maneno wapi wameandika USA kakosa usingizi kwa ndege ambayo imecopiwa kutoka kwenye ndege yake mwenyewe ya f35...hiyo ndege ni mapema kuisifia kwa sababu hakuna sehemu imeshawahi kuingia mzigoni wala parformance yake kiuhalisia haijajulikana kwa maana ya kuingia vitani lakini ndege zote zinasosifiwa leo duniani zipo mzigoni na zimepimwa kwa kazi vitani kuanzia f22 mpaka f35 lakini hiyo ya mrusi imeingia vitani wapi? Punguza mahaba mkuu ndege vita inapimwa kwenye uwanja wa mapambano sio showroom
Nani muongo sasa kati ya mimi na wewe?
Screenshot_20210724-222521.jpg


Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Acha kuongeza maneno wapi wameandika USA kakosa usingizi kwa ndege ambayo imecopiwa kutoka kwenye ndege yake mwenyewe ya f35...hiyo ndege ni mapema kuisifia kwa sababu hakuna sehemu imeshawahi kuingia mzigoni wala parformance yake kiuhalisia haijajulikana kwa maana ya kuingia vitani lakini ndege zote zinasosifiwa leo duniani zipo mzigoni na zimepimwa kwa kazi vitani kuanzia f22 mpaka f35 lakini hiyo ya mrusi imeingia vitani wapi? Punguza mahaba mkuu ndege vita inapimwa kwenye uwanja wa mapambano sio showroom
Nitajie siraha yoyote ile ya Mrusi aliyoitangaza alafu kwenye uwanja wa vita ikawa tofauti na alivyosema?

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Siku ya Jumanne, Urusi ilizindua ndege yake mpya ya kivita na inayoweza kufanya misheni za kijasusi ya Sukhoi "Checkmate" katika onyesho la ndege mbele ya Rais Vladimir Putin.

Habari juu ya muundo na uwezo wa ndege hii ya kivita ya kizazi cha tano ilitolewa kwenye onyesho la anga la Max-2021 lililofanyika Zhukovsky nje ya Moscow.

Ndege hii ya kivita inachukuliwa kuwa mshindani wa ndege ya kijeshi ya Marekani yenye uwezo wa kujificha F-35 na Urusi imepanga kuiuza kwa nchi nyingi ulimwenguni.

Checkmate imetengenezwa na kampuni kubwa inayomilikiwa na serikali Rostec na Shirika la Ndege la United


"Checkmate" ni nini?

Kulingana na habari zilizopo, ndege hii ya kivita ya Checkmate ni nyepesi kuliko ndege ya injini-mbili ya Sukhoi Su-57 na inaweza kubeba makombora matano ya hewani kwa safu tofauti.

Ndege hii ina uwezo wa kuzindua droni wakati ikiwa hewani na kubeba jumla ya tani 7.5 za silaha.

Checkmate inahitaji barabara fupi sana ili kupaa au kutua hiyo inachukuliwa kuwa sifa maalum ya ndege hii.

Ndege hiyo imetengenezwa kama ndege ya kivita ya kizazi kipya yenye injini moja na utumiaji teknolojia ya kisasa inahesabiwa kati ya nguvu zake kuu.
Watengenezaji wa ndege hiyo wanasema kuwa teknolojia ya kisasa inayotumiwa katika Checkmate inafanya kazi kama rubani mwenza na itamsaidia rubani mkuu katika hali za kupigana.

Kulingana na watengezaji wa ndege hii, inaweza kupiga hadi malengo sita juu ya ardhi, hewani au baharini kwa wakati mmoja na inafanya kazi hata inapokabiliwa na usumbufu mkubwa wa kielektroniki.

Checkmate itagharimu karibu dola milioni 25 hadi 30 za Kimarekani. Baada ya majaribio ya ardhini, ndege hii itafanya safari yake ya kwanza mnamo 2023 na Urusi itaanza kuiuza kwa nchi mbali mbali kutoka 2026.

United Aircraft Corporation imesema inapanga kutengeza ndege 300 aina ya Checkmate katika kipindi cha miaka 15 ijayo. Kulingana na kampuni hiyo, idadi ya 300 imekadiriwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndege hii.

Watengenezaji wa Checkmate pia wanafanya kazi kutengeneza toleo la ndege hii ambalo halitahitaji rubani.





View attachment 1865036View attachment 1865037View attachment 1865038View attachment 1865040View attachment 1865041

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Watu hawalali huko urusi . . Ikifika mwaka wa kuuza watakuwa na ndege kubwa zaid ya hiyo
 
Su-75 Checkmate sio ya kutisha sana hata. Waingereza wanakuja na 6th generation jet inaitwa Tempest, Wakorea kusini wanakuja na 5th generation jet, Wajapan wanaileta 5th generation yao. Hizi zote naamini zitaizidi Checkmate

China inazo stealth J-20 na kuna nyingine inatengengezwa na Shenyang kwa ajili ya Navy. Hawa wakizipa injini kamili nazo zitakuwa na maana kuliko Su-75

US wana F-22 na F-35 ziko kamilifu na Checkmate haiwezi zikaribia. Su-57 ndio itashindana nazo ila nayo haijapata powerful engine ya Izdeliye 30, kwa sasa inatumia AL-41 ambayo haifiki supersonic speed bila afterburners na haiko stealth

US pia wana NGAD (Next Generation Air Dominance) iko mbioni ilikuwa siri mpaka mwaka huu. Muhimu zaidi US wana advanced secure datalink kamili kuliko Urusi ingawa mpaka leo F-22 na F-35 haziwezi communicate ni mpaka zitumie relay nyingine mfano kupitia U-2 reconnaissance plane. Datalink inasaidia kushare target na guidance ya radar, etc. Bado wana projects kadhaa za stealth drones

Checkmate inaletwa kama stealth flani ya kuwauzia wateja wasio na uwezo wa kumudu gharama kubwa za stealth jets zilizoko sokoni, au wateja wasioruhusiwa kunua stealth zilizopo mfano Turkey ambayo inakufa na project yake ya stealth jet pia. Ikumbukwe Su-57 haijapata foreign customers na bado iko kwenye development, mpaka ifikie maturity sio leo. Checkmate wanadai mpaka 2022 utaanza initial production ila siwaamini Warusi huwa wana estimations za uongo. Checkmate ndio ndege pekee ya Urusi kwenye karne ya 21 iliyotengenezwa kwa lengo la wateja tu, hata jeshi lao halijui kama ipo

Possible customers wa Checkmate ni kama Algeria, Egypt na India lakini haitakiwi ichelewe. Na hilo jina litabadilishwa, wakati Sukhoi wanatengeneza Su-57 walikuwa wanaiita PAK-FA ila MoD ikaibadili jina ilipotoa order

Mambo ni mengi
Ebu kuwa serious ndugu,yani ndege ya Wachina,Wajapan na Wakorea ziwe bora kuliko ndege ya Warusi.
Nitajie ndege hata moja waliyowahi kutengeneza inayofanana na ndege ya Mrusi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Ebu kuwa serious ndugu,yani ndege ya Wachina,Wajapan na Wakorea ziwe bora kuliko ndege ya Warusi.
Nitajie ndege hata moja waliyowahi kutengeneza inayofanana na ndege ya Mrusi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Japan ana silaha nyingi za maana kuliko unavyodhania. Japan ina diesel submarines zinazotumia Air-Independent Propulsion system na ni nchi chache sana duniani zinajua kutengeneza hizi. Sweden ndio mgunduzi wa hii system na kaiweka kwenye subs zake za Gotland

Japan ina Type 10 main battle tank. Duniani ukiniuliza ni kifaru gani kiko optimized kwa matumizi naitaja Type 10 ikifuatiwa na Black Panther MBT ya S. Korea iliyoyengenezwa na Samsung. Hawa ukiwafuata kwenye ardhi yao ukaenda na vifaru vyako wanakupiga navyo wala huwashindi

Wote wana frigates za kisasa na pia wana modern amphibious assault ships wakati Russia mwaka 2014 alivunjiwa mkataba na France kuuziwa meli za Mistral, ziliuzwa kwa Misri yuko analinga nazo. Kwahiyo Russia HAWEZI sasahivi kutengeneza meli za kubeba helicopter kuzidi uwezo wa Japan au S. Korea

Japan sio mara yake ya kwanza kutengeneza ndege. Kwa sasa wana F-2 inayotengenezwa na Mitsubishi, ni derivative ya F-16. Wamehusika pia kwenye F-35 project na wanazo.

Checkmate haijaundwa kuwa air superiority fighter wala air dominant. Ipo kama mbadala wa stealth nyingine na hata Russian Airforce hawakutoa configuration kuwa iwe hivi, wao hawajui itakuwaje kwa hiyo sio kwa ajili yao. Na tender ya kuitengeneza hawajatoa hivo usidhani itakuwa ya maajabu, ila watatoa order ya units kadhaa. Naifananisha na China ilivyotoa J-17 ikaiachia Pakistan ifanye licence production

Japan na ROK wanaunda mlinzi wa anga lao kwa miaka ijayo. Russia anaunda bidhaa ya kuuza ndio lengo kuu na kukaa nayo kama subsidiary, anazo Sukhoi na MiG nyingi za kumlinda
 
Japan ana silaha nyingi za maana kuliko unavyodhania. Japan ina diesel submarines zinazotumia Air-Independent Propulsion system na ni nchi chache sana duniani zinajua kutengeneza hizi. Sweden ndio mgunduzi wa hii system na kaiweka kwenye subs zake za Gotland

Japan ina Type 10 main battle tank. Duniani ukiniuliza ni kifaru gani kiko optimized kwa matumizi naitaja Type 10 ikifuatiwa na Black Panther MBT ya S. Korea iliyoyengenezwa na Samsung. Hawa ukiwafuata kwenye ardhi yao ukaenda na vifaru vyako wanakupiga navyo wala huwashindi

Wote wana frigates za kisasa na pia wana modern amphibious assault ships wakati Russia mwaka 2014 alivunjiwa mkataba na France kuuziwa meli za Mistral, ziliuzwa kwa Misri yuko analinga nazo. Kwahiyo Russia HAWEZI sasahivi kutengeneza meli za kubeba helicopter kuzidi uwezo wa Japan au S. Korea

Japan sio mara yake ya kwanza kutengeneza ndege. Kwa sasa wana F-2 inayotengenezwa na Mitsubishi, ni derivative ya F-16. Wamehusika pia kwenye F-35 project na wanazo.

Checkmate haijaundwa kuwa air superiority fighter wala air dominant. Ipo kama mbadala wa stealth nyingine na hata Russian Airforce hawakutoa configuration kuwa iwe hivi, wao hawajui itakuwaje kwa hiyo sio kwa ajili yao. Na tender ya kuitengeneza hawajatoa hivo usidhani itakuwa ya maajabu, ila watatoa order ya units kadhaa. Naifananisha na China ilivyotoa J-17 ikaiachia Pakistan ifanye licence production

Japan na ROK wanaunda mlinzi wa anga lao kwa miaka ijayo. Russia anaunda bidhaa ya kuuza ndio lengo kuu na kukaa nayo kama subsidiary, anazo Sukhoi na MiG nyingi za kumlinda
Mbona ni swali dogo tu naona maelezo mengi ila unashindwa kunijibu.nitajie ndege moja tu ya kuifananisha na ndege ya Mrusi

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Hiki kifaa kina uwezo wa kuchapa angani,majini na ardhini.
60fc1d6a85f5405b0268386c.jpg
 
Ngoja nikazindue ungo usioonekana hewani na kupaa kwa kasi ya roboti
 
Mbona ni swali dogo tu naona maelezo mengi ila unashindwa kunijibu.nitajie ndege moja tu ya kuifananisha na ndege ya Mrusi

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Japanese F-2 ni sawa na F-16 ya Marekani zina tofauti kidogo. Japan ndio nchi ya kwanza duniani kuweka AESA radar kwenye fighter jet. F-16 ina kill/loss ratio kubwa almost 5:1 kuliko Mig-29 ya Russia yenye almost 1:1 vitani zilikoshiriki. Ingawa hii ratio hutegemea pia uwezo binafsi wa marubani na mafunzo yao

Kwahiyo Japanese F-2 inaizidi Russian Mig-29
 
Siku ya Jumanne, Urusi ilizindua ndege yake mpya ya kivita na inayoweza kufanya misheni za kijasusi ya Sukhoi "Checkmate" katika onyesho la ndege mbele ya Rais Vladimir Putin.

Habari juu ya muundo na uwezo wa ndege hii ya kivita ya kizazi cha tano ilitolewa kwenye onyesho la anga la Max-2021 lililofanyika Zhukovsky nje ya Moscow.

Ndege hii ya kivita inachukuliwa kuwa mshindani wa ndege ya kijeshi ya Marekani yenye uwezo wa kujificha F-35 na Urusi imepanga kuiuza kwa nchi nyingi ulimwenguni.

Checkmate imetengenezwa na kampuni kubwa inayomilikiwa na serikali Rostec na Shirika la Ndege la United


"Checkmate" ni nini?

Kulingana na habari zilizopo, ndege hii ya kivita ya Checkmate ni nyepesi kuliko ndege ya injini-mbili ya Sukhoi Su-57 na inaweza kubeba makombora matano ya hewani kwa safu tofauti.

Ndege hii ina uwezo wa kuzindua droni wakati ikiwa hewani na kubeba jumla ya tani 7.5 za silaha.

Checkmate inahitaji barabara fupi sana ili kupaa au kutua hiyo inachukuliwa kuwa sifa maalum ya ndege hii.

Ndege hiyo imetengenezwa kama ndege ya kivita ya kizazi kipya yenye injini moja na utumiaji teknolojia ya kisasa inahesabiwa kati ya nguvu zake kuu.
Watengenezaji wa ndege hiyo wanasema kuwa teknolojia ya kisasa inayotumiwa katika Checkmate inafanya kazi kama rubani mwenza na itamsaidia rubani mkuu katika hali za kupigana.

Kulingana na watengezaji wa ndege hii, inaweza kupiga hadi malengo sita juu ya ardhi, hewani au baharini kwa wakati mmoja na inafanya kazi hata inapokabiliwa na usumbufu mkubwa wa kielektroniki.

Checkmate itagharimu karibu dola milioni 25 hadi 30 za Kimarekani. Baada ya majaribio ya ardhini, ndege hii itafanya safari yake ya kwanza mnamo 2023 na Urusi itaanza kuiuza kwa nchi mbali mbali kutoka 2026.

United Aircraft Corporation imesema inapanga kutengeza ndege 300 aina ya Checkmate katika kipindi cha miaka 15 ijayo. Kulingana na kampuni hiyo, idadi ya 300 imekadiriwa kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wa ndege hii.

Watengenezaji wa Checkmate pia wanafanya kazi kutengeneza toleo la ndege hii ambalo halitahitaji rubani.





View attachment 1865036View attachment 1865037View attachment 1865038View attachment 1865040View attachment 1865041

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Punguza kutumia Google translate. Mada hiieleweki kama habari za BBC Swahili kule FB

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Sasa Urusi wanataka kutuaminisha kuwa Checkmate itakuwa na bei ndogo mara mbili ya Su-35. Yani Su-35 Flanker E inachezea $85 million alafu Checkmate iwe na flyaway cost ya $35. Labda wakiipa Checkmate operation na supporting cost kubwa sana kufidia gharama. Ni kama Sweden wanakuuzia Saab Jas 39E/F Gripen kwa zaidi ya $75 million ila operations cost ndogo sana. Wakati US wanauza kwa wahusika F-35A kwa $80 million ila operation cost utazikimbia

Ila procurement ya ndege ni very complex subject sio ya kusema hapa ukamaliza
 
Back
Top Bottom