Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

La mkuu..tunataka mabao zaidi.Hawa mabwana wakifunga bao la
kusawazisha sisi nje.

Hiyo ni kweli AT, tunatakiwa tusiruhusu hata kagoli kamoja ni full defend and full attacks hadi filimbi ya mwisho.
 
Hatuna maneno mengi tunafanyakazi iliyotupeleka uwanjani. Tuendelee kuangalia total attack.
Shadow nilikwambia wewe na wenzako mna gundu

Nakubali ustadh mwenzangu.Itabidi tunyweshe watu juisi ya pilipili.
Hapa dili ni kufunga zaidi tu.Hamna ku-defend bao moja wala nini.
 
Ebanaeeeeeeeeeeeeeee tunawakosakosa tuuuu. Kibao kisije kikatugeukia!
 
We acha, enzi zile Mourinho alikuwa anaonekana mkorofi lakini kuna wakati marefarii hawana mana hata kidogo.

Amewaacha na foul on Moulada na pia Drogba kategwa ndani ya boksi.
Hii kitu bana.tungekua bao mbili juu sasa.
 
Mechi ishaisha hii ngoma mpaka mwisho itakuwa 1-0.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…