Chenga ya mwili: Walininukuu vibaya, sikusema nyongeza ni asilimia 23.3 kwa kima cha chini bali nyongeza ni sh 23,300/= kwa kima cha chini!

Kiukweli hii wiki tutasikia na kuona mengi.

Japo mwisho wa siku ndo imeshatoka hivyo.
 
Reactions: nao
Haya ndo madhara ya kuwa na mbumbumbu wengi Bungeni, tuliendekeza ushabiki tukaacha kuwapa Wapinzani Ubunge sasa tunajionea nchi inapelekwa jinsi majizi yanavyotaka, 2025 Watanzania tuamke,tuwachague Wabunge radical ili watusemee mjengoni
 
CCM wanajipa viti wenyewe.... Hawajali umempigia kura nani. Mahela na team yake wanapokea maelekezo tu.
 
Wewe umesema na wapewe tu wabunge wa upinzani sababu hakuna watetezi wa watumishi mm ndugu yangu kapata mshutuko alichokiona ni siri yake
 
Tatizo si mwigulu ni Boss wake.
 
Watu wengi hawajui Hili Mwigulu ni waziri wa fedha ambae ndie huumiza Watanzania ...mtu akijua hili hawez kumpenda huyo jamaa
Si kweli tatizo ni mkubwa wake tu anatekeleza maagizo ya juu
 
Wanaoandika humu ni wajinga wasio na kazi serikalini. Tumeridhika kwanza ametimiza ahadi ya kuongeza hata kama ni kidogo. Tulikaa miaka 7 bila hata ahadi.
Asante Mama tuna imani kikubwa kitakuja. MaCHADEMA kakimbieni barabarani.
 
Kwani nani huwa anawapigia kura?

Hao wasiopata huu mshahara ndio wanafurahi wakisikia mmeminnywa na ndio watajitokeza kupiga kura kwa wingi
 
Wanaoandika humu ni wajinga wasio na kazi serikalini. Tumeridhika kwanza ametimiza ahadi ya kuongeza hata kama ni kidogo. Tulikaa miaka 7 bila hata ahadi.
Asante Mama tuna imani kikubwa kitakuja. MaCHADEMA kakimbieni barabarani.
Ndo maana unaitwa fisi
 
Wewe mtu katoka kuchunga Ng'ombe na Punda Singida akaja mjini kusoma na akaajiriwa kimchongo Bengi kubwa na baadaye apipopata mtaji wa kununua Jimbo akanunua,alafu unampa kuwa Waziri wa hela kwa experience na exposure gani!!.Nchi ngumu sana hii!!
 



Na nasikia kaleta tozo tena mpya ya kila muamala wa kuchukua hela bank iwe ndani counter, ATM, TIss, n.k hela nyingi kuliko wanazotoza bank wenyewe siku zote [emoji24][emoji24]

Wakati gharama za maisha zikipanda kila siku afadhali ya jana bila huruma wanaongeza kuchukua hela za wananchi [emoji24]

Kwa kila muamala ukichukua hela utakatwa.

Kwa msingi upi ?

Kwa hiyo turudi kwenye ujima tuache kutumia huduma za ki-bank ili kuepukana na makato ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…