Chereko chereko ujio Tume Huru ya Uchaguzi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Zimesikika chereko chereko na mayowe ujio wa tume huru ya uchaguzi.



Bila shaka katika wote kina Addo Shaibu pale mtaa wa Jukwani nao pia hawajabakia nyuma.

Haiyumkiniki tume hii itaundwa kwa kuzingatia msingi uliopo katika katiba pendekezwa ili kupisha shari:



Kwa kuzingatia msingi huo, bila shaka basi kwa sasa, utakuwa na majina mazito mazito haya:

1. Prof. Ibrahim Juma
2. Khamis Ramadhan (Kaimu CJ Zanzibar)
3. Job Ndugai
4. Zubeir Maulid (Zanzibar)
5. Jaji Mustapha Siyani
6. Jaji Ibrahim Mipawa

Tusaidiane kama kuna nilipotereza kuweka kumbukumbu kuwa sahihi.

CCM mbele kwa mbele 🎼🎼!

Kazi iendelee.
 
Hamna kitu hapo
 
Wajumbe wa kamati ya uteuzi wameteuliwa na Rais.Baadae tena Rais atamteua mwenyekiti wa tume miongoni mwa walioteuliwa na kamati ya uteuz i.sioni tofauti.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Hakuna utumwa mbaya kama ule unaojiona upo huru...ndio tume itakavyoundwa🤣

 
Hii nchi siyo ya wanasiasa, wanasheria na wanaharakati- TUHESHIMIANE
 
Tume ya mahera, siyo? kura zipigwe kwa njia ya mtandao......haina kuingia na mabegi meusi hiyo.
 
Hiyo tume huru mbona wateuzi wake ni wana CCM?
 
CCM hawawezi kukubali tume huru ya uchaguzi hiyo ni danganya toto. Wanajua the moment wanaruhusu kitu cha namna hiyo ndio utakuwa mwisho wao.

Wana roho ngumu kuliko ya paka. Wanataka kuja kivingine. Nani atairidhia time hii?
 
Makungu ni Jaji mkuu wa Zanzibar?

Palikuwa na angalizo pale. Wengine sisi si wakazi wa huko:

"Tusaidiane kama kuna nilipotereza kuweka kumbukumbu kuwa sahihi."

Vipi mlishafanya mabadiliko tufanye maboresho stahiki?

CCM mbele kwa mbele 🎵🎵.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…