China imeondoa ushuru kwa bidhaa za Tanzania

China imeondoa ushuru kwa bidhaa za Tanzania

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, Kwa mara ya kwanza Jamhuri ya watu wa China imepitisha uamuzi wa kuondoa kodi (Zero-Tarrif) kwa asilimia 98 ya bidhaa zinazotoka Tanzania kuanzia Mosi Disemba 2022. Msamaha huu kwa bidhaa za Tanzania ni matokeo ya juhudi za Rais Samia katika kukuza diplomasia.

Bidhaa zilizoondolewa ushuru ni pamoja na bidhaa za bahari, Korosho, Parachichi, Karafuu, Kahawa, bidhaa za madini, Tumbaku, bidhaa za ngozi n.k, China ni soko lenye watu zaidi ya bilioni 1.4 ikiongoza Duniani na pia ikiwa na pato ghafi (GDP) linalo kadiriwa kuwa zaidi ya Dola Trilioni 17.

Kwa mujibu wa Takwimu zilizopo, katika kipindi cha Mwezi Octoba 2022 ukilinganisha na kipindi kama hiki mwaka
2021, Tanzania imeendelea kuimarisha uwezo wake wa kuuza bidhaa nje(Export) ambapo kiwango kimeongezeka kutoka Dola Bilioni 9.4 hadi Dola Bilioni 11.6. Kasi hii ni kubwa na inayotoa tumaini kubwa.

Pia, katika maeneo mengine kiuchumi serikali chini ya Rais Samia inaendele kufanya vizuri, mfano katika Mfumuko wa Bei, kiwango kimeendelea kuwa cha 5.4% (Single digit index), ni nchi chache Duniani zenye kiwango hiki.
 
sio juhudi ni juhudi za wananchi wakiwa wafanyabiashara alisikika Dkt bashiru akisema
Yes ni juhudi za watanzanzania wafanyabiashara pamoja na kuwa na mazingira magumu ya biashara wameendelea kukomaa kufanya biashara na haya ndio matokeo.
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, Kwa mara ya kwanza Jamhuri ya watu wa China imepitisha uamuzi wa kuondoa kodi (Zero-Tarrif) kwa asilimia 98 ya bidhaa zinazotoka Tanzania kuanzia Mosi Disemba 2022. Msamaha huu kwa bidhaa za Tanzania ni matokeo ya juhudi za Rais Samia katika kukuza diplomasia.

Bidhaa zilizoondolewa ushuru ni pamoja na bidhaa za bahari, Korosho, Parachichi, Karafuu, Kahawa, bidhaa za madini, Tumbaku, bidhaa za ngozi n.k, China ni soko lenye watu zaidi ya bilioni 1.4 ikiongoza Duniani na pia ikiwa na pato ghafi (GDP) linalo kadiriwa kuwa zaidi ya Dola Trilioni 17.

Kwa mujibu wa Takwimu zilizopo, katika kipindi cha Mwezi Octoba 2022 ukilinganisha na kipindi kama hiki mwaka
2021, Tanzania imeendelea kuimarisha uwezo wake wa kuuza bidhaa nje(Export) ambapo kiwango kimeongezeka kutoka Dola Bilioni 9.4 hadi Dola Bilioni 11.6. Kasi hii ni kubwa na inayotoa tumaini kubwa.

Pia, katika maeneo mengine kiuchumi serikali chini ya Rais Samia inaendele kufanya vizuri, mfano katika Mfumuko wa Bei, kiwango kimeendelea kuwa cha 5.4% (Single digit index), ni nchi chache Duniani zenye kiwango hiki.

It's like taking a candy from a baby...

Baada ya kuwauzia bandari sio...hilo halina ubishi...
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, Kwa mara ya kwanza Jamhuri ya watu wa China imepitisha uamuzi wa kuondoa kodi (Zero-Tarrif) kwa asilimia 98 ya bidhaa zinazotoka Tanzania kuanzia Mosi Disemba 2022...
Ukiona hivyo ujue serikali ya tanzania nayo imekubali kuwaachia wahalifu wooooote wa kichina waliokuwa wanashikiliwa kwa makosa mbalimbali waliyofanya humu nchini ikiwemo ujangili....!
 
Nasie tukifuata ule utaratibu wa nipe nikupe, kati ya sie na China, nani anamuuzia zaidi mwenzake bidhaa?
Tukijitutumua kusamehe Kodi Kwa bidhaa kutoka China nani ataumia?
China ndio imesamehe na sio Tanzania mzee
 
Tujiulize hao wachina wenyewe wanapata nini hawawezi kusamehe Kodi kizembe ndio tuamue kama ni jambo jema au tumepigwa
 
Ukiona hivyo ujue serikali ya tanzania nayo imekubali kuwaachia wahalifu wooooote wa kichina waliokuwa wanashikiliwa kwa makosa mbalimbali waliyofanya humu nchini ikiwemo ujangili....!
Rais Samia Suluhu anapambana kwaajili yetu punguza makasiliko
 
Back
Top Bottom