China kuongeza kima cha chini cha mshahara na kuwasaidia watu wenye matatizo ya kiuchumi

China kuongeza kima cha chini cha mshahara na kuwasaidia watu wenye matatizo ya kiuchumi

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111308282310.jpg

Hivi karibuni, mikoa mingi ya China imetangaza kupandisha kima cha chini cha mshahara kwa mwaka 2021. Kwa mujibu wa kiwango cha sasa, Shanghai inaongoza kwa Yuan 2,480 kwa mwezi, sawa na dola za kimarekani 384. Kadri kima cha chini cha mshahara kinavyopanda, kipato cha wafanyakazi wenye kipato kidogo kinaongezeka. Hii ni hatua nyingine ya China kuongeza hisia ya usalama na uwezo wa kupata ajira kwa watu wenye kipato kidogo.

Kupandisha kima cha chini cha mshahara kinaongeza kipato cha watu wenye kipato kidogo
Baada ya kuondoa umaskini uliokithiri, pengine kuboresha maisha ya watu wanaoishi maisha magumu kiasi na kuongeza kipato chao itakuwa moja ya kazi za kuwasaidia watu maskini za China siku za baadaye. Janga la COVID-19 lililokuja ghafla limeathiri sana kipato cha watu waishio mijini na vijijini hapa China. Na ili kukabiliana nalo, serikali itapandisha kima cha chini cha mshahara, kitendo ambacho sio tu kinalingana na sera ya kupandisha kima hicho kila baada ya muda, bali pia ni kuhakikisha maisha ya watu wenye kipato kidogo, pamoja na kukidhi madai ya wafanyakazi ya kuongezewa mshahara.

Kuendeleza vijiji na kuboresha maisha ya watu wenye kipato cha chini
Waraka wa kwanza uliotolewa na Chama cha Kikomunisti cha China mwaka huu, umesisitiza kuendelea kukuza sehemu za vijiji ambazo tayari zimeondokana na umaskini, na kuwasaidia watu wenye kipato cha chini vijijini. Hali halisi ni kuwa serikali ya China siku zote imehimiza maendeleo yenye uwiano na uhamaji huria wa watu kati ya miji na vijiji, kustawisha vijiji kupitia huduma za kifedha, kuongeza usawa wa huduma za kijamii za kimsingi, kukamilisha usimamizi wa vijiji na kupunguza pengo la maendeleo na kipato kati ya watu wa mijini na vijijini. Teknolojia ya uchumi wa kidigitali imeongeza kwa kiasi kikubwa huduma za jamii za kimsingi, na kutimiza utoaji elimu na huduma za matibabu kwenye mtandao wa internet ili maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanufaishe watu wenye kipato cha chini na cha kati.

Kuimarisha utoaji elimu ya ufundi stadi ili kuongeza uwezo wa watu wenye kipato cha chini kupata ajira
Mapinduzi ya teknolojia ya raundi mpya yamepunguza madai ya ukosefu wa baadhi ya nafasi za ajira kwa uwezo wa ufundi wa wafanyakazi, lakini kwa upande wa pili pia yameongeza pengo la mshahara kati ya aina tofauti za kazi. Kipato cha watu wanaofanya kazi katika mashirika binafsi na wale wanaojiajiri kinaongezeka polepole, na hii ndio sababu ya mshahara wa kundi la watu wenye kipato cha chini kuongezeka polepole kuliko makundi mengine. Ndiyo maana, ni lazima kujenga na kukamilisha utaratibu wa kutoa elimu ya ufundi stadi kwa watu wenye kipato cha chini. Hii si kwa China tu bali hata kwa nchi za Afrika, elimu ya ufundi stadi inaweza kutoa uhai kwa soko la ajira linalokabiliwa na mageuzi ya kiuchumi na kiteknolojia.

Kwa muda mrefu, haswa baada ya kufanyika kwa mkutano wa 18 wa wajumbe wote wa Chama cha Kikomunisti cha China CPC, serikali ya China imejitahidi kutenga fedha, na kuwatambua kwa usahihi na kuwasaidia watu wenye kipato cha chini. Katika miaka mitano ijayo, China itaendelea kuongeza kipato cha watu wenye kipato kidogo, kupunguza pengo kati ya matajiri na maskini, na kufanya ongezeko la kipato cha wakazi kuendana na ongezeko la ukuaji wa uchumi.
 
Aya ndo Mambo mazur serikali yetu inapaswa kuiga.

Watumishi wa umma wa kada za chini skuhizi wamegeuka omba omba mitaani.

Watumishi Hawa wamekua waathirika wakubwa wa MIKOPO CHEFU CHEFU nna MIKOPO UMIZA kutoka kutoka taasisi mbalimbali.

Watumishi Hawa wamekua waathirika wakubwa wa matukio ya utapeli wa michezo ya UPATU.

SERIKALI INAPASWA KULIANGALIA HILI KWA JICHO LA TATU
 
Mabeberu hawajaliona mpaka sasa hilo? Yasiwafike kama ya Libya tu
 
china imetajirika kwa kuwa nyonya wafanyakazi na kufanya wawekazaji kuwekeza makampuni makubwa kwa sababu ya wafanyakazi bei rahisi.mifano hipo kampuni zilizopo ulaya na usa inapenda kuzalishia china kwa vile ndio chip
 
Je, mfanyakazi wa Bank za huku anapokea ngapi kwa mwezi?? Inafika hata laki tano?

380 × 2319= 881220
Unakusudia bongo? Hivi bongo nayo nchi ya kuihisabia? Nilikusudia kwenye nchi za wenye akili.. mshahara wa week mkubwa kuliko huo wa mwezi mzima huko China..cha kushangaza wao maraisi wao hawawaabudu wala kuwaogopa kama sisi,ndio kwanza wanawavunjia mayai...when I think of this I really wonder what's wrong kwa watu weusi..
 
Unakusudia bongo? Hivi bongo nayo nchi ya kuihisabia? Nilikusudia kwenye nchi za wenye akili.. mshahara wa week mkubwa kuliko huo wa mwezi mzima huko China..cha kushangaza wao maraisi wao hawawaabudu wala kuwaogopa kama sisi,ndio kwanza wanawavunjia mayai...when I think of this I really wonder what's wrong kwa watu weusi..
Na ndio maana makampuni mengi yakakimbilia kwenda kuzalisha china sababu ya unafuu wa mishahara na gharama za maisha kwa wafanyakazi
 
Unakusudia bongo? Hivi bongo nayo nchi ya kuihisabia? Nilikusudia kwenye nchi za wenye akili.. mshahara wa week mkubwa kuliko huo wa mwezi mzima huko China..cha kushangaza wao maraisi wao hawawaabudu wala kuwaogopa kama sisi,ndio kwanza wanawavunjia mayai...when I think of this I really wonder what's wrong kwa watu weusi..

Ingependeza zaidi ukatuwekea na kima chao cha chini huko kwa mabeberu, pia usisahau population ya china ni kubwa kuliko nchi yoyote duniani, may be kaulaya kote kanamezwa na baadhi ya nchi za amerika.
 
Ingependeza zaidi ukatuwekea na kima chao cha chini huko kwa mabeberu, pia usisahau population ya china ni kubwa kuliko nchi yoyote duniani, may be kaulaya kote kanamezwa na baadhi ya nchi za amerika.
Kima cha chini kabisa kwenye Nchi so called MABEBERU kima cha chini kabisa cha malipo ya mtu kwa saa

National living wage

United Kingdom [emoji636] ni £ 8.72 per hour
United States [emoji631] ni $ 7.25 per hour lkn hii ni chini kabisa kwenye state zingine inaanzia $14 per hour.

Scandinavian countries wanalipa vizuri kuliko UK or US kwa hiyo malipo hayo ya Wachina wanayo lipa kwa mfanyakazi wa kawaida ni sawa sawa na mchahara wa MABEBERU KWA watu wake wanalipwa kwa WEEK tena in basic workweek hours ambayo ni MASAA 40HRS Monday to Friday .

Huo mchahara wa mchina haujajieleza ni masaa mangapi wanafanya usije kuta ni 12hours shift kwa siku unafanya kazi hadi unasikia harufu ya Damu .
 
Kima cha chini kabisa kwenye Nchi so called MABEBERU kima cha chini kabisa cha malipo ya mtu kwa saa

National living wage

United Kingdom [emoji636] ni £ 8.72 per hour
United States [emoji631] ni $ 7.25 per hour lkn hii ni chini kabisa kwenye state zingine inaanzia $14 per hour.

Scandinavian countries wanalipa vizuri kuliko UK or US kwa hiyo malipo hayo ya Wachina wanayo lipa kwa mfanyakazi wa kawaida ni sawa sawa na mchahara wa MABEBERU KWA watu wake wanalipwa kwa WEEK tena in basic workweek hours ambayo ni MASAA 40HRS Monday to Friday .

Huo mchahara wa mchina haujajieleza ni masaa mangapi wanafanya usije kuta ni 12hours shift kwa siku unafanya kazi hadi unasikia harufu ya Damu .
Wow yaani kama mbingu na ardhi..mbaya zaidi hawa wachina ndio kigizo chetu, kikubwa,Utasikia wachima hawaongei English wachina rafiki wakweli, wazungu wanawapenda watu wao...ndio maana serikali inachukia watanzania kwenda Ulaya.
 
Kima cha chini kabisa kwenye Nchi so called MABEBERU kima cha chini kabisa cha malipo ya mtu kwa saa

National living wage

United Kingdom
emoji636.png
ni £ 8.72 per hour
United States
emoji631.png
ni $ 7.25 per hour lkn hii ni chini kabisa kwenye state zingine inaanzia $14 per hour.

Scandinavian countries wanalipa vizuri kuliko UK or US kwa hiyo malipo hayo ya Wachina wanayo lipa kwa mfanyakazi wa kawaida ni sawa sawa na mchahara wa MABEBERU KWA watu wake wanalipwa kwa WEEK tena in basic workweek hours ambayo ni MASAA 40HRS Monday to Friday .

Huo mchahara wa mchina haujajieleza ni masaa mangapi wanafanya usije kuta ni 12hours shift kwa siku unafanya kazi hadi unasikia harufu ya Damu .
Inategemea na population ya nchi, nchi kama uingereza yenye idadi ya watu milioni 68 na ushee watashindwaje kuwalipa raia wake huo mshahara ulioutaja!!!! Population ya china with a population of around 1.4 billion in 2019, sasa unategemea watalingana!
 
Kima cha chini kabisa kwenye Nchi so called MABEBERU kima cha chini kabisa cha malipo ya mtu kwa saa

National living wage

United Kingdom [emoji636] ni £ 8.72 per hour
United States [emoji631] ni $ 7.25 per hour lkn hii ni chini kabisa kwenye state zingine inaanzia $14 per hour.

Scandinavian countries wanalipa vizuri kuliko UK or US kwa hiyo malipo hayo ya Wachina wanayo lipa kwa mfanyakazi wa kawaida ni sawa sawa na mchahara wa MABEBERU KWA watu wake wanalipwa kwa WEEK tena in basic workweek hours ambayo ni MASAA 40HRS Monday to Friday .

Huo mchahara wa mchina haujajieleza ni masaa mangapi wanafanya usije kuta ni 12hours shift kwa siku unafanya kazi hadi unasikia harufu ya Damu .
Na gharama za .maisha kwenye hizo nchi zote zipoje compared na China
 
Back
Top Bottom