Ndege ya kukodi ya China iliwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing jumanne tarehe 2, ikibeba abiria zaidi ya 140 wa China waliorejea kutoka nchini Sudan. Kabla ya hapo, manowari za China zilizokuwa zikifanya kazi ya ulinzi katika Ghuba ya Aden zilikwenda Sudan na kuwachukua karibu raia 1,000 wa China, na hadi sasa, karibu raia wote wa China waliokuwa nchini Sudan wameondoka nchini humo. China pia imekuwa nchi iliyorejesha raia wake wengi zaidi kutoka nchini Sudan tangu nchi hiyo ikumbwe na migogoro.Mwaka jana, kulikuwa na filamu iliyopata umaarufu sana nchini China iitwayo “Safari ya Maelfu ya Maili”. Filamu hiyo iliyotungwa kufuatia matukio ya kweli na kuelezea hadithi ya wanadiplomasia wa China kuwarejesha raia wa China kutoka kwenye nchi fulani ya Afrika ya kaskazini kwa kutumia juhudi zao zote.
Baada ya kutokea kwa mapigano ya ghafla nchini Sudan, serikali ya China ilikuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa raia wake nchini humo. Rais Xi Jinping wa China aliiagiza Wizara ya Mambo ya Nje, kwa kushirikiana na idara mbalimbali, kuongoza ubalozi wa China nchini Sudan kuanzisha haraka mchakato wa kuwaondoa Wachina walioko nchini Sudan, haswa maeneo yaliyoathiriwa zaidi na mapambano ikiwemo Khartoum. Tarehe 22 mwezi Aprili, ubalozi wa China nchini Sudan na katika nchi nyingine jirani zilitoa taarifa ya dharura ya kuwahamisha Wachina nchini Sudan. Tarehe 26 mwezi huo, Jeshi la Ukombozi la Watu wa China liliagiza manowazri zake za kivita zilizokuwa zikifanya kazi ya ulinzi katika Ghuba ya Aden kwenda Sudan mara moja, ili kuwachukua raia wa China. Kulingana na ripoti, mchakato wa kuwajeresha watu kutoka nchini Sudan ni hatari zaidi kuliko iliyosimuliwa katika filamu. Kaimu wa balozi wa China nchini Sudan Zhang Xianghua, amekuwa akitekeleza majukumu yake akiwa amevaa nguo na kofia nzito zinazoweza kuzuia risasi. Amesema wakati wa kusaidia watu kuondoka, milio ya risasi ilikuwa inasikika mara kwa mara, na ndege za kivita zikirushiana makombora angani.
Hii siyo mara ya kwanza ya China kuwaondoa raia wake kutoka nchi zilizokumbwa na vita. Mwezi Februari mwaka 2011, mapigano makali yalizuka nchini Libya. China ilituma vyombo vya baharini, nchi kavu na anga vikiwemo ndege za abiria, meli za kibiashara, manowari, na mabasi kuwahamisha raia wake zaidi ya 32,000 kutoka Libya hadi sehemu zenye usalama. Mwezi Machi mwaka 2015, wakati vita ilipozuka nchini Yemen, manowari za kijeshi za China zilienda nchini humo kuwaokoa raia 621 wa China na raia 279 wa nchi nyingine 15.
Hatua hizo zimethibitisha kuwa, bila kujali Wachina wako wapi, na wanakabiliwa na hali gani, watapata msaada wa haraka na wenye nguvu kutoka kwa taifa lao. Aidha, hatua hizo pia zimethibitisha tena msimamo wa serikali ya China ya kuzingatia zaidi maslahi ya watu wake.