China wamezindua 6th Gen Jet Figher inaitwa Baidi: Ina uwezo wa kuoperate kwenye air na Space!

Wewe sasa ndio unachekesha f 22 zimeuzwa kwa nchi ipi na ipi je nazo mbovu au zina shida gani mpaka zisiuzwe
 
Umeandika vizuri.

Ila pia 6th gen itafocus sana kwenye AI, maana kama speed LM washakuaga na mach 3+ kitambo tokea 1960s.

Kila mmoja anaogopa kutangulia kuonesha au ni secret project usikute vyuma tayari vipo
Secret project ya Lockheed Martin huwa kwa Skunk Works walewale walioasisiwa na engineer Clarence "Kelly" Johnson wakatoa SR-71 Blackbird. Sasa kama Blackbird ilikuwa ni secret project hata funding walikuwa wanadanganya kupewa bajeti basi lazima na SR-72 iwe secret.

Na si kwamba Marekani wanashindwa Mach 3 maana kina LM na Boeing waliishaifanyia demonstration ila kibiashara, gharama za uendeshaji na ulazima bado havishawishi Mach 3 fighter kwa sasa. SR-71 iliundwa iwe high altitude fast flying reconn jet, baadae missile tech ikaruhusu interceptors zenye 3.5 Mach na sasa hadi 4 Mach interceptors unapata. Idea ya SR-71 ilikuwa ni utaniona naingia kwenye anga lako, utafyatua kombora kunipiga ila nitakimbia nilizidi. Sasa hivi haifanyi kazi hivyo hakuna ulazima sana wa Mach 6.

Hata Urusi baada ya Mig-25 hawajatoa ndege yenye kasi zaidi ya ile sababu kasi kubwa sana haina haja mwisho wa siku ni hasara. Mig-25 ilikuwa ikikimbia sana inakatika joints, inalegea nati na inapata leakage. Ilikuwa inamshinda control rubani alafu gharama zake kubwa tu.

Marekani wakati wanaunda SR-71 walijua aluminium itakataa properties zile ngumu wakahitaji kupata titanium, na titanium inachimbwa Urusi tu kwa kipindi kile. Wakatafuta kampuni uchwara ya Marekani ikaenda Urusi kununua titanium ikidai inatengenezea flying pan za pizza. Warusi wakauza component ya silaha alafu kwao ndege yao hawataki gharama ikawa na performance ndogo. Sema walikuja kurekebisha kwa Mig-31 ambayo si mbaya.
 
Wewe sasa ndio unachekesha f 22 zimeuzwa kwa nchi ipi na ipi je nazo mbovu au zina shida gani mpaka zisiuzwe
Umezungumzia F-35 sasa unapigwa za uso unakuja kwa F-22.
F-22 haiuzwi na iko kwenye sheria kabisa tangu ndege inaanza.

Sio kila kitu ni cha kuuza kama vipi waambie China wenye J-20 zaidi ya 200 kwa sasa waanze kuuza. Urusi ndio inataka kuuza Su-57 na wateja bado, joint project na India ilikufa India ikaona hamna kazi ikachukua hela yake ikakimbia. Kitambo Su-57 inaitwa PAK FA.
 
Helmet ya F 35 inauzwa dola 400K, 2 billions Tzshs.

F35 wanaipigia sana kelele watoe hata mbili ziingie kuisadia Ukraine..


F35 ni tolea limebuma, hakuna cha stealth wala electronics warfare... Wajinga ndio waliwao.. mbona hawauzi hizo F22 raptor?
 
Ona unavyojikanyaga hapo nimekuomesha tu kwamba ndege kuuzwa sana sio kama ndio ubora ushawahi kujiuliza kwanini hio 22 haiuzwi ila hio 35 inauzwa
 
Ila si uwa tunaziona F-7s. They are old ila nice, maybe zipo ambazo hawaziweki public.
Ndege sio mapera kwamba unazificha, hakuna cha maybe ni kwamba hatuna modern fighter jet angalau ya kutulinda.

J-7 au F-7 ni ndege za kizazi kilichopita hata kama nyingine zimenunuliwa na Kikwete zile 7G. Kenya na hasa Uganda wana airforce ina ndege nzuri kuliko sisi. Tuna majirani wengi sana inabidi kuwa na air dominance ndio utawale vita lolote likitokea. J-7 hata BVR haina sasa ndege gani hiyo lazima uone adui kwa macho ni kama unapigana acrobatic.
 
Helmet ya F 35 inauzwa dola 400K, 2 billions Tzshs.

F35 wanaipigia sana kelele watoe hata mbili ziingie kuisadia Ukraine..


F35 ni tolea limebuma, hakuna cha stealth wala electronics warfare... Wajinga ndio waliwao.. mbona hawauzi hizo F22 raptor?
Nimemuuliza hapo juu badala ya kujibu anaanza kutoa vioja f35 hamna ndege pale kama ndege kweli wauze 22 tuone
 
Actualy how ndio leading aircraft military aircraft manufactures, even recent chines war planes nyingi wamecopy kutoka kwa design za lockheed
So hawajapoteana, focus ipo kwenye drones zaidi
Lok he'd wanaondoka hao ohoooo
 
Helmet ya F 35 inauzwa dola 400K, 2 billions Tzshs.
Na wamenunua ndege zaidi ya 1000.

Urusi ana Su-57 tuambie ni nani kanunua😂
F35 wanaipigia sana kelele watoe hata mbili ziingie kuisadia Ukraine..
Fighter jet sio bodaboda za kubebea kitimoto kwamba unatoa mbili zinafanya delivery.

Fighters zina formation, zina squadron ndege kama 12 au juu/pungufu kidogo kutokana na mfumo wa Airforce ya nchi husika. Sasa utoe ndege mbili kwani hizo zimekuwa AWACS?

Kama F-35 haziendi Ukraine mbona pia bado Su-57 haziendi Ukraine.
F35 ni tolea limebuma, hakuna cha stealth wala electronics warfare... Wajinga ndio waliwao.. mbona hawauzi hizo F22 raptor
F-22 sio ndege ya kuuza. Marekani sio machinga kwamba kila kitu inauza kama nchi fulani hadi Alaska iliuza hata Flanker jets iliuzia China teknolojia.
 
Nimemuuliza hapo juu badala ya kujibu anaanza kutoa vioja f35 hamna ndege pale kama ndege kweli wauze 22 tuone
Hii mada tukijadili humu miaka imepita, F35 ni toleo la ndege walitaka kufanya iwe na uwezo kufanya mambo lukuki kitu ambacho ilipelekea kikatikea kituko kinaitwa F35...

Mission F35 imefanya? Israel si anazo, na F35 inasifika ni stealth na ina uwezo kushambulia radar, mbona Israel hajazitumia kufanya retaliation nchini Iran, angeingiza hata F35 nne tu...

Badala yake kishia mipakani...

Hata watengenezaji wenyewe hawaamini hizo ndege uwezo wake kama wanavyo present..

F22 kwenye uwanja wa mapambabo inai outperform F35 katika uhalisia... F35 ina outperform F22 kwenye maneno na specs za maabara ambazo ni kinadharia zaidi not practical...
 
Helmet ya F 35 inauzwa dola 400K, 2 billions Tzshs.

F35 wanaipigia sana kelele watoe hata mbili ziingie kuisadia Ukraine..


F35 ni tolea limebuma, hakuna cha stealth wala electronics warfare... Wajinga ndio waliwao.. mbona hawauzi hizo F22 raptor?
Mwenye toleo kali la stealth plane ni nan?
 
Naunga mkono hoja 35 walitaka kuitia mambo mengi ikafeli ila Ile 22 hatari sana Ile 35 inajionesha tu hamna jambo ndege zinaanguka tu zenyewe kila siku
 
Tusubiri ya wamagharibi .... nadhani Ulaya sasa watatafuta yao bila kuihusisha Marekani.

T14 Armata
 
Hapo juu umesema marekani sio ya kuuza kila kitu halafu huku chini umetaka Russia auze su je kama nae anafanya kama marekani anavyo fanya kwa 22
 
Ona unavyojikanyaga hapo nimekuomesha tu kwamba ndege kuuzwa sana sio kama ndio ubora ushawahi kujiuliza kwanini hio 22 haiuzwi ila hio 35 inauzwa
Ndege itauzwa kama iko sokoni, kama haipo sokoni haitauzwa.

F-35 iko sokoni na inashinda tenda zote inazoshiriki, imeuzika units zaidi ya 1,000.

J-20 ya China haiko sokoni, huwezi sema haiuziki wakati haiuzwi. F-22 haipo sokoni vilevile.

Su-57 ya Warusi iko sokoni ila imedoda hakuna mwendawazimu anaweza nunua ndege hata injini yake maalum haina mpaka leo. Mpaka sasa Su-57 inatumia AL-41F1 injini ileile ya Su-35 na some Su-30 variants. Injini ya 4th gen kwenye 5th ni vichekesho.
Injini ya Su-57 ni Izdeliye AL-51 mpaka leo haijawa tiyari wako wanateseka uko kuunda.

Su-57 yenyewe hata squadrons kadhaa Warusi hawana, ukiwaambia wapige elephant walk wanapoteana. Sasa unalinganishaje vitu havina hadhi sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…