China yaanza mazoezi ya kijeshi karibu na Taiwan

Taiwan sio mtoto. Taiwan kamuacha mbali sana Ukraine kiuchumi, technology,jeshi, etc,etc
Eneo la taiwani ni dogo sana kupambana na nguvu za china siyo kama ukrain pale taiwani hata kungekuwa na askari wa marekani mi2 awawezi kamwe kuishinda china ...kuhusu uchumi ..kwenye vita mambo ya 8chumi haya angaliwi ikiwa uwanja wa vita ni hizo nchi zinazo pigana ...mfano Russia ikipigana na Marekani vita vya nchi kwa nchi uwezi kusema mambo ya uchumi na viwanda maana vyote vinapigwa mabomu hadi mabenki nk
 
Marekani hii inakiri silaha za Hitler zilikuwa bora sana kuliko zao ila wao ndo walishinda vita
 
Ona kinachowatokea Ukraine sasa hivi, marekani ni hypocrisy mmoja tu asiyeaminika tena.
Wewe unaandika hivi huko taiwan wenzako wapo tumbo joto sababu china anazidi kupitisha ndege jeshi katikati ta taiwan.
Ona kinachomtokea mvamizi Russia kule Ukraine.
 
Vipi wewe unavyopenda kuibeza marekani, afu unajiona uko sahihi ila wanaobeza hao uwapendao ndo hawako sahihi.
 
Vita sio baikoko. Urusi walifika just few kilometres from Kyiv ila walikwama . Hii vita inapigwa mbungi ya maana aisee
 
Vipi wewe unavyopenda kuibeza marekani, afu unajiona uko sahihi ila wanaobeza hao uwapendao ndo hawako sahihi.
Sija ibeza Merikani, nataka members to know the other side of the story ambazo niza kweli - nimeona kuna baadhi ya watu wanakasirika kweli kweli mpaka wanafikia hatua ya kutumia lugha chafu/kutukana watu,kisa? Umeigusa their omnipotent and omnipresent NATION - ni hilo tu na wala hawana hoja mbadala zaidi ya matusi tu na majibu ya mkato - yaani badala ya jukwaa kutumika kuelimishana na kubadirishana mawazo linageuzwa kuwa jukwaa la mipasho kama taabaru za Khadija Kopa - tofauti kabisa na jamiiforums ya zamani ambayo watu walikuwa wana heshimiana, we mtu ambaye wala hakujui anakwambia eti unavuta bang!! Akili gani hizi?? Cha kushangaza wasimamizi wa JF they don't take any punitive action to contain tabia hii ambayo imeanza kuota mizizi, so sad.
 
Tuchambuwe vita weee ila kikinuka sisi ndo tutawekwa mbele ili tufe mapema
 
Wewe umekuwa kinara wa kuhamasisha uvamizi wa urusi dhidi ya Ukraine..,unafikia hatua kutoa ushauri kwa vikosi vya Putin kufanya haraka sana kuipindua serikali Halali ya rais zelensiky huko Ukraine..,unashangilia mauaji haramu yanayofanywa na vikosi vya Putin ukidhani wanamkomoa rais zelensiky [emoji848] alafu unategemea watu watumie lugha ya staha dhidi yako?????
Hivi akinamama waliopoteza watoto wao huko Ukraine, ndugu na jamaa waliopoteza wapendwa wao ,unafikiri watatumia lugha gani dhidi yako wakiona unasapoti waziwazi kabisa unyama uliofanywa na vikosi vya Putin????
SI watakuona wewe ni shetani kabisa uliyevaa mwili wa binadamu???


Unashabikikia udhalim unaofanywa dhidi ya taifa huru alafu unategemea uheshimiwe?? Maajabu haya[emoji848]
 
Hata wewe na wenzio huwa mnaelezea na kusifu tu uwezo wa China na Russia, Sasa hao unaowalaumu nao wanapost uwezo uliotukuka wa US ili nyie mjue upande mwingine wa story.
 
I think china should end taiwan drama by this time taking the island. No legal problems at all as the highest jurisprudence bodies in this world the united nations especialy recognise taiwan as a renegade province of china. Taiwan generals should help the island avoid distruction from war caused just by greed of politicians representing western interests.
 
Unaibeza HIMARS zimeletwa 8 Tu Ukraine zimebadiri upepo umesema mrusi anazo HIMARS zake zinaitwa tornado mbona hatuzioni? Pamoja na misifa kedekede uzoipa hiyo tornado mbona Russia kakwama Kwa HIMARS za USA ?....Acha mahaba HIMARS za USA zimeleta mageuzi kwenye Vita ya Ukraine wewe bishana Russia wanalijua Hilo ndio maana wamepoa...
 
We jamaa natamani nijue jinsia yako maana Una chuki za kike sana unaichukia Sana USA Naona jamaa hapo juu kataja HIMARS wewe umekuja na maelezo mareefu kuonyesha China pia inayo hizo HIMARS kama za USA ila zake ni Bora Sana....

swali Tu kwako sijui wewe ni KE au ME hizo za HIMARS za China unazosema Bora kuliko za USA zimepigana Vita gani ambazo mwezetu umeziona?

USA kaleta HIMARS 8 Tu dunia imeona kinachomkuta Putin Ukraine SASA hiv
HIMARS ni zaidi ya popobawa anakugonga anasepa.... Russia kichwa kinamuuma
 
Hii vita ni ya kimkakati mkuu. America ni mtu hatari sana. Kwa sasa amewafanya China na Urusi kila mtu apambane na lake. Soon tutegemee kusikia ya India na Pakistan yakiibuka. Hawa ndio USA, wajanja wa dunia na viranja wakuu.
Macho ya America yapo pale,ikirushwa hata gurunet moja,ikaingia Taiwan,aisee hayo ma HIMMARS,mbona Mchina atalia,yeye amuache Urusi apigane tu kule,asiombee yamkute nayeye.
 
Maajabu gani?? Zelensky na jeshi lake la KINAZI (Azov) linavaa mpaka beji za Hitler, limeua zaidi ya Waukraine 14,000 wenye asili ya Urusi bila sababu za msingi kosa lao eti hawakubaliani na mapinduzi yaliyo iondoa madarakani Serikali iliyo kuwa umechaguliwa ki-demokrasia na raia wa Ukraine, mapinduzi hayo yalichochewa na US mpaka wabunge wa Merikani(McCaine,Nulad na engine) wakawa wanafunga safari kutoka Merikani kuja Ukraine kuchochea mapinduzi na vurugu, swali ni,je,Wabunge wa Urusi au Uchina wanaweza kudiriki kuingia Merikani na kuchochea vurugu??

Mbona miaka kama mitatu iliyo pita raia wa Merikani walivamia Bunge kwa nguvu wakidai kwamba Trump ndiye alishinda kura hivyo ndiye
ana haki ya kuwa Rais sio Biden, vurugu zilikuwa kubwa kabisa kuna watu walipoteza maisha katika vurugu hizo,mbona wabunge wa Urusi au Uchina hawaku ingilia kati na kuunga mkono a potential colour revolution nchini Marekani kama ilivyo fanyika huko Ukraine au ndio hayo ya mkuki kwa nguruwe?

Hapa naona mnamlahumu sana Putin lakini hamtaki to know kiundani kwa nini Putin alihamua ku-resort to a pre-emptive strike dhidi ya majeshi ya Zelensky ,je,NATO/UN waliwahi ku-address kikamilifu concerns za Taifa la Urusi kuhusu usalama wa Taifa lao, jibu ni hapana badala yake NATO/US wanatishia tishia Urusi kwa kufanya mazoezi ya kivita karibu na mipaka ya Urusi all the year round, hata Papa alitamuka wazi wazi kwamba NATO specifically US ndio wana provoke Urusi kila mara, US wanakwenda mbali zaidi wanatumia Ukraine kama stepping stone ya kuihujumu Urusi kiuchumi na kutaka kuidhoofisha kijeshi wanataka Urusi iwe destroyed kabisa ili husiwe tena tishio kwa maslahi ya magharibi - vurugu zote huko Ukraine chimbuko lake ni hilo - haya mambo ya kudai eti nchi za magharibi zinatetea Taifa la Ukraine huo ni ulaghai mtupu na unafiki. Tafuteni ukweli kuhusu kiini cha matatizo nchini Ukraine na sio kumulahumu Putin/Urusi wholesale, yeye anataka kujihakikishia usalama wa Taifa lake na huo ndio wajibu wake, kumbe afanyeje?
 
Mkuu tayar umesharusha missiles za kutosha mashariki mwa Taiwan ngoja nitafute ile video niweke hapa
Tafuta pesa, hacha ushabiki maandazi kama una KAZI ya kufanya nenda kwy CRDB Marathon
 
Mastory ya uongo uongo tuuu. Miaka 70 ya wapi? Wewe Acha kamba
 
Mambo yao waachieni wenyewe...

Wapigane, mafuta yapande tena lita moja iwe elfu50...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…