China yasema ipo tayari kuharibu uhuru wa Taiwan kwa njia yoyote

Wa Ukraine wanayapigania maeneo yao,
they are fighting for their sovereignty...

Hakuna taifa litakubali taifa lingine liingilie maeneo yao
Hata ukiwa nyumbani kwako ukifanya kitu chakuhatarisha usalama wa nyumba ya jirani yako huyo jirani hawezi kukuchekea.
Atakuonya, ukikaidi atakuvamia na kukupiga ili kulinda usalama wake.
 
Kwa Sababu wanataka mapatano Kwa njia ya Amani kwanza
Taiwan Hawataki, wameshaona kilichotokea Hong Kong. Sasahivi Hong Kong hamna tena uhuru wa watu na Demokrasia. Serikali ya Xi hata itoe ahadi gani wataiwan na nchi za Kidemokrasia hazitoweza kukubali kwasababu ahadi za China huwa ni za uongo.

Aliahidi kuiacha Hong Kong iendelee na system yake yaani one country two systems mpaka 50 years ili wa Hong Kong wafanye transition waone kama wataweza kufit na hajafanya hivyo.

So chochote atakacho ahidi Taiwan hawezi kusikilizwa
 
1. Sio wajibu wako kuwapangia China ni muda gani sahihi wa kuvamia Taiwan, wala Taiwan sio priority ya kwanza ya China. Kwahiyo kutovamia haimaanishi hawawezi, Mwakinyo kukataa pambano na Mandonga haimaanishi hamuwezi.

2. Issue sio rahisi, haijawahi tokea vita rahisi. Vita zote unazoona duniani huwa ni maamuzi magumu. There is no easy or short war na kila anayejua lolote kuhusu vita anajua hili.

3. Yanayoendelea China mainland huyajui peke yako, katika nchi nafuatilia inaanza Uturuki inafuata China ila katika majeshi nafuatilia China ni ya kwanza. Kwahiyo siandiki kama mashabiki lialia wa mpira.

4. Migomo, lockdown, pension, housing, unemployment, restrictions na government intervention kwenye investments, firewall, mass surveillance, authoritarianism ya Xi na matatizo mengine mengi ya China nimeyazingatia sana kabla ya kuandika. Pension haifyatui risasi, marubani wa jeshi hawatoshindwa kuendesha fighters kisa mabilionea wa China wamezuiwa na CCP kuwithdraw pesa wakimbilie Western countries kwenye uhuru.

Nazi Germany wakati inaanzisha Operation Barbarossa dhidi ya USSR kwani Wasovieti walishindwa kupigana kisa Stalin jeshini alifanya The Great Purge ya late 1930s? Stalin kwa mkono wake mwenyewe aliua Wasovieti zaidi ya milioni 6 kwa mass containment, akaua mamia ya maofisa wa jeshi, akatumia Cheka kuua komredi wenzake wa Bolshevik, akaanzisha Gurags kule far East na kuwafunga waandishi wapendwa na wanasiasa kisa wamemkosoa. Akafunga huduma za kidini zote, sio kanisa katoliki wala kanisa pendwa la serikali lile Orthodox. Ujerumani ilipovamia matokeo si unayajua mwenyewe.

Unajua mazingira gani wananchi wa Japan walipitia kabla ya IJN kuvamia Pearl Harbour na kuanzisha vita dhidi ya Marekani. Mbona walipigana vita kali miaka mitatu tena Wajapan wakajitoa hadi muanga na suicide missions zao za kamikaze attack na banzai charges. Kuna nchi ambayo raia wakishirikiana na jeshi kwenye WW2 kuizidi Japan?

5. Nani kakwambia vita haina prediction? Vita ina prediction na military schools na institutions duniani ndio kazi zake hizo. Marekani hadi wana wargames wanalipa hela nyingi private companies zidevelop hypothetical scenarios.
Prediction kuwa sahihi au sio sahihi ni jambo lingine, na kuna options nyingi. Usahihi wake utategemea ni information kiasi gani unayo na uwezo binafsi wa kuichakata kutoa hitimisho.

6. China wana mapungufu mengi kama nchi nyinginezo, hakuna nchi haina mapungufu. Au basi waambie Waarabu kwamba Israel kwa sasa ina mapungufu kisiasa, maandamano, kesi za rushwa za vigogo, mgogoro wa Wakristo & Waislamu na Wayahudi na unyanyasaji kwa raia wenye asili ya Kiarabu kwahiyo waivamie uone.

Kununua vyeo vya kijeshi haimaanishi walionunua ni vilaza completely, kwanza ni asilimia ngapi ya vyeo vinanunuliwa au umeambiwa vyote wananunua. Morali ya kipindi cha amani sio ya kipindi cha vita, inanishangaza kuona unatarajia China wanajeshi wasiwe na morali.
Airbases za Taiwan zote zinajulikana, ground facilities baaadhi zinajulikana, highways kwa ajili ya emergency runways zinajulikana, naval bases na submarine pans, fixed radar installations, shore based defense lines kule Western sides. Vyote hivyo kwenye eneo linazidiwa sana ukubwa na Tabora, then useme jeshi superior la China lisiwe na morali kwa kisa cha kuokoteleza eti maofisa wananunua vyeo.

Amka usingizini wewe. Taiwan haitoshinda vita kisa China ina matatizo, na uache kukimbilia Marekani badala utaje hiyo Taiwan kwanza. 82nd Airborne Division ambayo ndio hutakiwa kuwa standby muda wote haiwezi peke yake kuipiga China, US Marines wakiongezeka hawawezi, hata Pacific Fleet yote ikija haiwezi mpaka ije task force. Sasa task force na logistics zake mpaka zikamilike kufanya uvamizi kwa China, Taiwan ishatekwa muda sana.

Narudia kusisitiza, hii ni CHINA vs TAIWAN. Marekani sio guarantee itakuja na ikija ni vita nyingine hiyo yenye mazungumzo tofauti na haya.
 
Kwa akili zako unadhani nchi za west zitakubali Demokrasia iliyojengeka vyema ya Taiwan iharibiwe kirahisi.

Halafu, Xi akishaichukuwa Taiwan so what?

Unafkiri China ipo tayari kwamba ipo self sufficient enough kupambana na vikwazo na mizozo ya ndani na nje itakayoibuka baada ya vita?

Migomo ya white hair movement na white pape movement tu ya juzi iliitetemesha selikari ya Xi mpaka akaondoa ghafla lockdown, sasa imagine migomo ya hali duni na njaa itakayokuja kwababu ya vikwazo.

China na selikari nzima ya Xi inajua fika madhara yatakayowapata na itakayoikumba CCP. Na ndio maana wanatumia kila njia kuprotect their regime, kwasababu anajua fika watu wa kwanza kuufuta utawala wa kikomunist ni wachina wenyewe.

China akiivamia Taiwan ndio utakuwa mwisho wa PRC, msipokuwa makini Xi atawapeleka shimoni. Covid 19 mpaka Leo hii ni janga China kwasababu ya sera mbovu, the same kwa sera za mambo ya nje. Sasahivi mataifa mengi yanaiangali China kama taifa tukutu wachina wanapoteza ile picha yao ya mwonekano wa watu wenye juhudi na busara na kuwa taifa ovu.

Selikari ya Xi itakipata inachokitafuta.
 
Hiv unaakiri sawasawa kweli, maeneo yanayokwapuliwa na mvamizi na watu kwenye nchi yao( Taiwan) kuna ufanano hapo[emoji848]
 
Itakuwa siku mbaya kwa china siku mbaya kwa Dunia. Nisiku ambayo china itakuwa kama mavumbi na ndege wa angani watakuwa wakila mizoga kama Tai. Nisiku mbaya kwa china ikiwa ataigusa Taiwan. Kwanini? China anafikiri anamarafiki ila ana maadui wengi kutokana na siasa zake na mienendo yake. Mwarabu hawezi mpendwa mchina kwasababu hana dini na waarabu wanapata shida ktk Taifa hili Wazungu ndio kabisa wanahasira name maana amewaibia taarifa nyingi za teachnology
 
Haya yote uliyoandika hayaonyeshi ni vipi Taiwan itaishinda vita. Umeandika dhana yako ya baada ya vita kitakachotokea. Ngoja nikupe mifano wa hoja iliyopo hapa.

1. Vita ya Tanzania na Uganda nani alishinda? Jibu - Tanzania.
Hatujauliza nani alikimbia nchi kati ya Nyerere na Amin, hatujauliza nani alisaidiwa silaha, hatujauliza jinsi Nyerere ujamaa na uchumi ulivyomshinda baadae akang'atuka. Tumeuliza nani alishinda vita, sio matokeo baada ya kushinda vita.

2. Nani alishinda WW2 kati ya Nazi Germany na allied forces? Jibu - Allied forces.
Swali haliulizi Ulaya walivyopokea lend lease, Marekani ilivyopitisha Marshal plan, USSR walivyokufa zaidi ya 20 million, Nazi na USSR zilivyoshirikiana kuivamia Poland.

Swali letu ni nani anashinda baina ya Taiwan na China kivita. Jibu ni China, pigia mstari na ufanye bold. Mambo ya West hawatakubali hayo ni matokeo baada ya ushindi wa China. Sasa kama hawatokubali ndio guarantee China watawasikiliza?
Kwani Ujerumani ilivyoiteka France na Poland nani alikubali, je ilimzuia Ujerumani? Nusu ya Ulaya nzima ilitekwa na Ujerumani na kukataa kwao hakukubadili matokeo mpaka vita yenyewe.
Unamtaja Xi hivi unajua Xi ni mpole kiasi na kuna mtazamo ndani ya CCP unaotaka Taiwan itekwe? Una quarantee gani kwamba Xi akiondoka Taiwan inasalimika.

Unajua mgogoro wa ndani wa Pakistan mwaka 1999 ukivyosababisha jeshi lao livamie India ili kupoteza concentration. Unajua kwanini baada ya vita PM Nawaz Sharif na General Pevrez Musharaf walivyosingiziana nani kaanzisha vita?

Yani Urusi ambaye hata top 10 kiuchumi duniani hayupo, hana industrial sector kubwa ya kusupport vita ila bado hajapigwa na hao Marekani mwaka mzima sasa sembuse China anayejiweza kiuchumi na kiviwanda. Urusi inafunga gesi yake Ulaya wananunua hata Qatar kwa bei ghali na wanaongeza bei bidhaa, sasa China inapigwa vikwazo na Marekani ghafla US inaikosa nchi #1 inayomuuzia na wakati uleule #1 inayonunua bidhaa kwa mwaka. Atakayeziba gap ya China ni nani, unadhani ni maamuzi rahisi tu kama kuifungia Urusi ambayo ikivimba sawa tu watachuuza mafuta kutoka Angola, Libya, Nigeria or whatever.

Una safari ndefu sana kwenye geopolitics. Kwenye jeshi ndio kabisa hata hujaanza. Unataja vita na mtazamo wote umekaa kiuchumi na kimataifa. Popote hugusii silaha, teknolojia, geography, population, landmass wala lolote. Vita ya Ukraine hii hapa imekaa zaidi ya mwaka, kama unayosema ni rahisi kufanyika si wangeshamvamia Urusi wampige?

Vita baina ya China na Taiwan wakijitegemea inayoshinda ni China. Baada ya hapo ni agenda nyingine ambayo unaisemea hapa, unachosema wewe ni kuikomboa Taiwan ambayo ishapigwa. Watoto wakigombana anayetetewa ndio kapigwa, huwezi ona mtoto kampiga mwenzie alafu anadai subiri nimuite kaka yangu uje uone.
 
Sasa kwanini PLA pamoja na Xi na selikari yake hawajaivamia Taiwan mpaka sasahivi? Kama wanajijua fika wana uwezo mkubwa kijeshi?

Biden alishasema wazi iwapo China itaivamia Taiwan jeshi la Marekani litakwenda kuitetea Taiwan na ukisikia Marekani inakwenda vitani ujue ma allies wa Marekani wote watakuwepo vitani kushirikiana na Marekani na tunaona hatua zinazochukuliwa ikiwemo kuweka militarily bases Philippines ambayo inatazamana kabisa na Taiwan, kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na Japan, south Korea na Australia.

Yaani China ikiivamia Taiwan itaibua mambo mengi Sana, there is no way China iingie vitani na Australia, Japan, Philippines, Marekani na nchi za ulaya zinazounda umoja wa NATO halafu ashinde hiyo vita.

No way...., utaongea sana lakini uhalisia ndo uko hivyo. Nchi zote zinazosapoti Demokrasia hazitoweza kukubali Taiwan ipoteze Demokrasia yake hivihivi tu kirahisi kama unavyosema. Nchi za west zinaitazamia Taiwan kama one of the representatives of good form of governance and leadership hawatoweza kuiacha ipotee.

China ikipigana na Taiwan itapigana na nchi zote zenye mfumo wa Demokrasia na there will be no way atashinda hiyo vita.

Xi anajua fika madhara watakayopata wachina na ndomana anatamani China iweze KUJITEGEMEA kwa kila kitu eti yaani isitegemee kitu chochote from outside no way hii kitu haiwezekani.

Technolojia ya semiconductor tu kuhusu electronics chip bado anahaha, more tha 75% ya mafuta na gas anaagiza bado migomo na mitazamo ya negative ya ndani ya China yenyewe halafu uje useme watakuwa salama.

Watakao athirika kwa kiasi kikubwa sana na huu mgogoro ni wachina zaidi ya milion 600 ambao hawana uwezo wanaotegemea kufanya kazi za viwandani ili mkono uende kinywani. Hawa ndio watakao teseka na ndio watakao Tishia stability ya selikari na chama cha CCP.... Xi analijua fika hili jambo.
 
Hapo umenifungua akili , china sio nchi salama kwa dunia ya leo , soon anaturudisha kweny ukolon
 
Urusi kumetokea nini?
Unaongea km umekatwa kichwa.
Wayukren wapo kwenye shida sababu ya viburi vya hao wamarekani wewe unatuletea porojo za Hollywood?
Hao jamaa USA wanaipeleka Dunia kubaya
Hv unasahau kuwa Urusi alipora Crimea ipa bado Ukraine hakutaka vita ? Umesahau Putin alitoka hadharan na kukiri kuwa na upande kwenye civil wars za east ukraine ila serikali ya ukraine ilikaa kimya , je Nyerer angemuacha Idd apige mpk dsm , ww ungekuwa unatype hiz pumba muda huu? Muwe mna reason , Ukraine amejitahid kuepusha direct war na urusi ila urus amekuwa anaitaka hii vita ili apore ardhi ya ukraine , hata ww ungekuwa rais wa ukraine ungekuwa ushafanya maamuz magumu tangu muda mrefu sanab, urusi ni wakorof , ww usijikute unaijua urui kuliko majiran zake , huu utomaso wetu ndi imetupelekea kwenye utumwa duniani na baadae tulitawaliwa kisa utomaso wetu , huko C.Africa wagner wanabaka na kuua watu hovyo ila mpo kimya kama nyumbu
 
Hata ukiwa nyumbani kwako ukifanya kitu chakuhatarisha usalama wa nyumba ya jirani yako huyo jirani hawezi kukuchekea.
Atakuonya, ukikaidi atakuvamia na kukupiga ili kulinda usalama wake.
Kitu gan ukraine alifanya cha kuhatarisha usalama wa urusi ? Wengi wenu hamuelew lolote kwenye huu mgogoro
 
Unazungumzia zama mbili tofauti , zama hzo watu walikuwa na ukanda hata watz walikuwa na usolidarity ila je ni sw na leo ? Unapofananisha zingatia zama pia , zama hz had ndan ya serikali ya kila nchi kuna raia wana asili zaidi ya moja so kupigana vita leo inabidi uweke mazingira ya watu kuguswa na vita na sio kuwaamsha tu wakapigane utapigana pekee yako kama kinachomkuta urusi , urusi angepigana na japan kwa misaada anayopewa ukraine basi urusi angekuwa hoi , ila inexperiencee Ukrainians ndo wanampa pumz Urusi maana wanaingia tiktok wakiwa kwny mtanange ivyo warusi inakuwa nyepes kupata za chini kuhus adui yao
 
Bdo upo 18c wenzio hawawaz kushinda vita bali kushinda vita yavkiuchumi kupitia vita
 
Kitendo cha kuitaja Tiktok kwenye vita kinaonyesha uwezo wako ulivyo, sitasema ukoje. Kwanza umeandika vitu irrelevant, kwamba zama hizo watu walikuwa na ukanda?
Marekani ina mchanganyiko wa weusi, Wahindu, Waarabu, Wachina, Wajapani, Wakorea, Wayahudi, wazungu na kila kona ya dunia na ndio inapigana vita kuliko nchi zote duniani. Tena inapigana bila kuvamiwa yani inajiingiza yenyewe. WW2 Marekani ilianzisha kambi za kuwaweka Wamarekani wenye asili ya Japan wakati Marekani iko vitani na nchi yao.
Ila mtu anayeleta habari za Tiktok kwenye vita hawezi jua haya mambo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…