My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,306
Cremea ilikuwa ni Jimbo tu, Taiwan ni Taifa kamili, China hana huo uwezo,nitaleta makala kueleza ni kwa nini China haweziHao wachina wawaige warusi walivyo kwapua jimbo crimea kutoka ukrane. Wakizubaa hao taiwan watajiunga nato.
Hilo sio rahisi,wewe unafikiri kwa Marekani anaweka makambi kila kona ya Dunia? Sababu ili aweze kupigana vita zaidi ya moja kwa wakati mmoja.
Embu tuongee kwa mazingira ya sasa ikitokea vita pale Mashariki ya Mbali,Marekani atapata shida gani ya logistics?Logistical issue zinasumbua hata mataifa makubwa tajiri si kwa si masikini tu peke yake mkuu
Logistical strains au long supply line ndio sababu moja wapo ya Mjerumani kupoteza katika Eastern Front wakati wa WWII ingawa zipo na sababu nyingine nyingine
Ingawa anyway naweza kuwa Wrong pia sababu mi mwenyewe na"digest" tu point -outs za analysts
Ndivyo inavyotakiwa na kuna uwezekano ikawa hivyo japo Taiwan ni tofauti na jimbo la CrimeaHao wachina wawaige warusi walivyo kwapua jimbo crimea kutoka ukrane. Wakizubaa hao taiwan watajiunga nato.
Kivipi kisiwa cha Taiwan kinaweza kusababisha hili?Ni wakati wa New World Order
It's said that Presidential Candidate must be very careful in selecting a running mate, in case they are elected.
At any Moment, a vice president is Just One heartbeat away from becoming the president of the United States of America - The most Powerful position in the World.
Wakati ambao Dunia itaongozwa na Mwanamke!
Ondoa hofu. China inaweza kunyakua eneo lake halali la Taiwan kwa siku moja sema mataifa washirika wa Taiwan wanaweza kufanya makosa yatakayoyopelekea dhoruba kubwa dunia nzimaUnawachukulia poa Taiwan sio? Hapo mchina anapaogopa sababu anajua akigusa tuu ni total destruction kwake na kwa Taiwan.
Embu tuongee kwa mazingira ya sasa ikitokea vita pale Mashariki ya Mbali,Marekani atapata shida gani ya logistics?
Taiwan inasema imeshuhudia ndege 38 zikiingia kwenye eneo lake la ulinzi
2 Oktoba 2021
Uvamizi huo wa Ijumaa uluihusisha ndege za kivita aina ya jet J-16 jets (kama zinavyoonekana kwenye picha hii ya maktaba), Taiwan imesema
Taiwan imeripoti kuwa ndege za kijeshi za Uchina 38 zimepaa na kuingia eneo lake la ulinzi la anga siku ya Ijumaa- ukiwa ni uvamizi mkubwa zaidi kuwahi kufanywa na Beijing hadi leo.
Wizara ya ulinzi ilisema kuwa ndege hizo, ikiwa ni pamoja na zana zenye uwezo wa kulipua mabomu, ziliingia katika eneo hilo kwa awamu mbili.
Taiwan ilijibu kwa kuzuwia haraka uvamizi huo kwa jeti zake na kutuma mifumo yake ya makombora angani.
China inaiona Taiwan yenye demokrasia kama jimbo lililojitenga, lakini Taiwan inajiona kama taifa huru.
Taiwan imekuwa ikilalamika kwa zaidi ya mwaka mmoja juu ya harakati za kijeshi za mara kwa mara za vikosi vya anga vya China karibu na kisiwa hicho.
"China imekuwa ikifanya uchokozi wa kijeshi, na kuharibu amani ya eneo ," Waziri mkuu wa Taiwan Premier Su Tseng-chang aliwaambia waandishi Jumamosi.
Serikali ya Beijing - ambayo inaadhimisha miaka 72 tangu kuanzishwa kwa Jamuhuri ya watu wa China- hadi sasa haijatoa kauli yoyote kuhusu tukio hilo.
Lakini awali ilisema kwamba safari kama hizo za anga zilikuwa ni za kulinda nchi na pia yalilenga "njama "baina ya Taiwan na Marekani.
Katika taarifa yake, wizara ya ulinzi ya Taiwani ilisema kuwa ndege 25 za kikosi cha jeshi la People's Liberation Army (PLA) ziliingia katika eneo la kusini -magharibi kama sehemu ya vikosi vya ulinzi ya utambuzi wa eneo (ADIZ) wakati wa saa za mchana, na kupaa karibu na visiwa vya Pratas.
Eneo la utambuzi wa kijeshi ni eneo lililoko nje ya eneo la nchi na ni eneo la anga la kimataifa - lakini ni eneo ambalo ndege ya kigeni bado inatambuliwa, kufuatiliwa, na kudhibitiwa kwa maslahi ya usalama wa taifa.
Ni eneo linalojitangaza na kiufundi linasalia kuwa eno huru la anga la kimataifa.
hii ilifuatiwa na wimbi la pili la ndege 13 za China katika eneo hilo hilo Ijumaa jioni. Zilipaa juu ya maji kati ya Taiwan na Ufilipino
Wizara ilisema kuwa ndege ya Kichina zilikuwa pamoja na zana za mabomu nne aina ya H-6 , ambazo zina uwezo wa kufanya mashambulio ya silaha za nyuklia, pamoja na ndege ya kuzuwia mashambulio yanayotoka kwenye manuari za kijeshi.
Mara kwa mara Beijing hufanya uvamizi wa aina hiyo kuelezea kutofurahishwa kwake na kauli zilizotolewa na Taiwan.
Haijafahamika nini kilichopsababisha uvamizi wa hivi karibuni
Maelezo zaidi juu ya mzozo baina ya Taiwan na China
Yapi maoni yako?
- Kwanini China na Taiwan zna uhusiano mbaya? China na Taiwan ziligawanyika tangu vilipotokea vita vya wenyewe kwa wanyewe katika miaka ya 1940, lakini Beijing inasisitiza kuwa kisiwa hicho kitarejeshwa kwake wakati mmoja, kwa nguvu iwapo itakuwa lazima.
- Taiwan inatawaliwa vipi? Kisiwa hicho kina katiba yake, viongozi waliochaguliwa kidemokrasia, na takriban wanajeshi 300,000 na vikosi vya usalama.
- Nani anaitambua Taiwan? Ni nchi chache tu zinazoitambua Taiwan. Wengi wanaitambua serikali ya Beijing badala yake. Marekani haina uhusiano rasmi na Taiwan lakini ina sheria inayoipasa kuipatia uwezo wa kujilinda
Naam! Ikitokea hivyo China itatumia mwanya huo.Niliwahi sikia analysis moja inayosema kwamba China atategea kipindi ambacho USA ametingwa na uvamizi fulani wa nchi kubwa nyingine halafu yeye ndio anautumia muda huo kuivamia Taiwan na ataichukua sababu kwa sasa China yupo Mbali sana kijeshi
China inaweza kupeleka jeshi kubwa kuliko raia wote wa Taiwan pamoja na vifaa vya kisasa vya kijeshi na kunyakua kwa siku moja. Labda tu Marekani atake kutia kiherehere ndipo vita vitageuka kuwa vya mafahali wawili au vya dunia nzima... Hili linawezekanaTaiwan haiwezi kuwa sawa na Crimea au Kashmir, ni ngumu kumezwa kwa nguvu bila kutokea madhara au uharibifu.
Kiutaniutani Taiwan inaweza kuchukuliwa kirahisi kabisa au ikawa sababu ya vita vikubwa vya duniaNdege 38 na bomber kama H6 ambazo ni nuclear capable, tena wameenda 2 times, asee hio ilikuwa ni vita kamili, walikuwa smart kutojibu...
Akifanya hivyo kumbuka maadui zake nao wanazo... Kwa kizazi hiki ukirusha bomu moja la nuclear wenzako watakurushia mabomu 20. Ukijibu kwa kurusha mabomu 50 wenzako watakurushia akiba yao yote maana watajua hakutakuwa na wakupona wala mshindi 😊😊😊najaribu kuvuta picha marekani inapigana kuilinda new York ama mji wake, either mshirika wake mhimu yoyote sijui ni silaha gani itatumika kumkabiri adui.
hope dunia itakuwa suppressed tena toka siku za Nagasaki na iroshima.
Wewe unaona mbaliChina kwa sasa Ina nguvu kama USA, vifaa vya kivita wanaweza kuvitengeneza kwa gharama ndogo na vyenye ubora kama USA, Purchasing power yao kubwa ndicho kitu kiliifanya USA ishinde WW2, sasa hivi hio sifa anayo Chinese, viwanda almost USA uzalishaji wake unafanyikia China... China si ya kupuuzwa..
Wasipoogopana wote wataporomoana na kupotezana... Kumbuka wote wana nguvu na wote wana washirika wenye nguvu.hatupaswi kuipuuza china lakini ni uupuzi kudhani china anaweza mess up na Us na akabaki kama alivyo.
Kwa vita vikubwa kati ya haya mataifa makubwa hawahitaji kuwa karibu ndio wapiganeLogistical issue zinasumbua hata mataifa makubwa tajiri si kwa si masikini tu peke yake mkuu
Logistical strains au long supply line ndio sababu moja wapo ya Mjerumani kupoteza katika Eastern Front wakati wa WWII ingawa zipo na sababu nyingine nyingine
Ingawa anyway naweza kuwa Wrong pia sababu mi mwenyewe na"digest" tu point -outs za analysts
chief hatupaswi kutemegea china kuivamia Taiwan hivi soon labda hapo baadae endapo wataona calculations zao zimekaa sawa.Naam! Ikitokea hivyo China itatumia mwanya huo.
Lakini tusisahau hata kama USA hatotingwa na uvamizi wowote, lazima China itataka na itafanya kuichukua taiwan kwa nguvu.
Sasa hatujui matokeo yatakuwa yapi maana hatujui ni nini Marekani itataka kufanya pale China itakapochukua uamuzi huo
Usiwe na hofu kisiwa hicho kitaunganishwa na China moja kiulaini tu.... Marekani ikisogeza pua yake ndipo vita vitaathiri dunia yote.Hawa wavimba macho watakipata wanachokitafuta ila varangati litakuwa ni la kukata na shoka ambalo litaathiri dunia nzima kwa miaka mingi ijayo hasa kama varangati hilo litakuwa ni la muda mrefu.
Anachoona China ni kwamba akichelewa Taiwan itazidi kujiimarisha na silaha za Marekani.chief hatupaswi kutemegea china kuivamia Taiwan hivi soon labda hapo baadae endapo wataona calculations zao zimekaa sawa.
china hawezi kubali kurudi kwenye stone age et kisa anatafuta uzibiti dani ya tawain.. hapo alipo ka- sacrifice mambo mengi hadi kufika levo hiyo ya kiuchumi, ni ngumu kufanya uamzi hatari kama huo.
hayo mengine ni Show off tu na kutuma ujumbe kwa Taiwan na mshirika wake kuwa sasa china sio ileee ya kipindi kile.
kuivamia Taiwan ni suicidal decision kwa china, china hajui ni majibu gani Taiwan itatoa ama mshirika wake mkuu Us atajibu nini.
tusitegemee insu ya taiwan ikawa kama Afghanistan.
kesi ya Afghanistan na Taiwan ni vitu viwili tofauti.