China yazindua Cruise Ship ya kwanza, 'Adora Magic City.'

Mzee wa kupambania

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2022
Posts
21,111
Reaction score
53,092
Shanghai, China
06/06/2023

Kampuni kubwa ya utengenezaji meli inayoitwa China State Shipbuilding Corporation (CSSC) yenye makao yake Shanghai walizindua meli ya kwanza ya kitalii (Cruise ship) kutengenezwa China, iliyopewa jina la Adora Magic City.

Itakuwa cruise ship ya kwanza duniani kuwa na internet ya 5G

Meli hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 5246 na vyumba vya kulala 2826 ina
•Restaurants
•Theaters
•Shopping centres
•Water parks & swimming pools
•Outdoor Cinema
•Casinos
•Gaming lounge
•Luxury-brand boutiques
•Photo Gallery & Shop
•Bar
•Modern gym
•Spa
•Beauty saloon
•Stage for live perfomance
•Multi-Sports Course (for playing volleyball/basketball/tennis
•Themed entertainment for kids in 3 age groups
(i)Age 2-5 yo, 6-8 yo, and 9-11 yo
(ii)Children Club Lounge is for older kids (12-14 yo/video games, movies, parties, planned activities),
(iii)Teen Club for teenagers (15-17 yo/movies, interactive video gaming, karaoke, themed parties, booking teen-only cruise shore excursion).


Mwonekano wa nje;




Baadhi ya picha za mwonekano wa ndani


Hotel



Restaurant


Theatre



Mall


Bar




Water park


Sasa ni wakati wa China kuingia katika ushindani na makampuni ya Ulaya, na America katika biashara ya cruise ships.

UTENGENEZAJI WA MELI CHINA
Mbali ya meli za abiria pia meli zinazotengenezwa kwa wingi nchini China ni meli za mizigo kama liquefied natural gas (LNG) tankers, oil tankers na container ships.

Baadhi ya rekodi zilizowekwa na China katika utengenezaji wa meli;

●Kwa miaka 13 mfululizo China inashikilia rekodi ya kuongoza uuzaji wa meli duniani.

●China State Shipbuilding Corporation (CSSC) ilisaini mkataba na kampuni ya Ufaransa ya CMA CGM kuitengenezea meli za kubeba kontena kubwa 16 zenye thamani ya 4 billion U.S. dollars. Imekuwa kampuni ya kwanza duniani kupewa oda kubwa kwa wakati mmoja

●Meli kubwa duniani ya kubeba container yenye ukubwa wa viwanja 4 vya mpira wa miguu, iliuzwa kwa kampuni ya Mediterranean Shipping Company (MSC) SA. Ilitengenezwa na kampuni ya Hudong-Zhonghua Shipbuilding Co Ltd, yenye makao yake Shanghai. Imepewa jina la MSC TESSA




●China pekee inachangia 47.3% ya meli za mizigo zinazotengenezwa duniani

●Kampuni za China zinaongoza kwa kuwa na zaidi ya nusu ya oda za meli zote ulimwenguni

Voice Of America (VoA):
China has 19 modern shipbuilding yards pumping out commercial and naval ships. One of China's shipyards is so large that its capacity surpasses that of all U.S. shipbuilders combined.
 

Attachments

  • images (2).jpeg
    54.6 KB · Views: 26
  • images (4).jpeg
    25.3 KB · Views: 23
  • images.jpeg
    48.3 KB · Views: 28
  • images (1).jpeg
    53 KB · Views: 21
  • a469943f-0f5c-490a-8c97-d8bc67028693_0.jpg
    89.3 KB · Views: 23
Hupendi Crazy ship building ya Tanzania ?


Hivi watanzania hatujachoka ku admire innovations za mataifa ya wenzetu ?
Mkuu jana nilikuwa natazama watubaki. Wakawa wanamshukuru niki wa pili kwa kuwa ana attend wakisema kuwa asante kwa kutuunga mkono. Akasema hapana siwaungi mkono ila mnanichekesha ndio maana nakuja siji kwa sababu ya kuwaunga mkono.
My point is, bidhaa ikiwa nzuri watu wataipenda tu haya masuala ya kuungana mikono kisa sijui ni mtanzania no. Si unaona siku hizi watu wanapenda suti local made, ni kwamba zimekuwa nzuri.
 
Tupambane mkuu , huko kwenye suti hakuwezi kututoa kama taifa.

Siku mkulima wa Tanzania akiacha kutumia jembe la mkono at least tutakuwa tumepiga hatua ya maana.
 
Amejitahidi ila bado sana kuwafikia royal Caribbean na madude kama symphony of the seas
Royal carobbean kumbuka wao wanatoa huduma za cruise lakini hawaundi meli. Meli zao zinaundwa na makampuni mengine toka ulaya.
China ukuaji wake ni wa ajabu sana yani ni kama atakuja kuwa kiongozi katika uzalishaji wa kila kitu. Sasa hivi anaongoza katika uzalishaji na uuzaji magari, anaongoza kwa meli huenda akianza uza ndegr za abiria akaongoza. Anaongoza katika kuuza electronics haya mambo miaka michache yalikuwa ya nchi kama korea kusini, japan et el
 
Tupambane mkuu , huko kwenye suti hakuwezi kututoa kama taifa.

Siku mkulima wa Tanzania akiacha kutumia jembe la mkono at least tutakuwa tumepiga hatua ya maana.
Mkuu badala ya serikali kuwekeza kwenye vitu kama hivyo walikuja na sera ya kilimo kwanza jeshi likaanza uza trekta ambazo thamani zake wakulima walio weng hawawez kuafford badala ya kubuni zana za kilimo local made.
Kwa sababu ya utanda wazi raia hazinunui bidhaa kisa ya uzalendo bali zinanunua bidhaa kwa sababu ni nzuri
 
Hii kitu inaweza ikawa sh ngapi? Nataki nijipange
 
Tuna safari ndefu sana kama taifa, mimi binafsi kichwa kinaniuma kuona sisi hapa duniani tunakaa kusubiri watu wa mataifa mengine wafanye ugunduzi halafu sisi tunabaki kuwa consumers tuuuuu.
 
Hivi wale wabunifu wetu wa helcopter waliishia wapi? Kwanini wasiwe accelerated ili siku moja wafike huku? Hawa wachina si nao walianza kama wetu?
 
Mdogomdogo wanaacha majina yao ya kichina

The 2023-built Adora Magic City cruise ship is the first of two China-built vessels ordered by CSSC CARNIVAL CRUISE and operated under the new travel brand Adora Cruises (2022-established/2023-inaugurated)


Magic city based on homeporting in Shanghai China
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…