Xi Jinping
JF-Expert Member
- Jun 14, 2023
- 3,651
- 11,548
Mwanamama Giorgia Meloni alishinda uchaguzi mkuu wa Italy mwaka 2023 na kuwa Waziri Mkuu wa taifa hilo ambalo pia ni member wa G7 na NATO.
Alipoingia tu madarakani, kwa shinikizo la Marekani na mataifa mengine ya Ulaya akaiondoa Italy kutoka kwenye mpango wa China unaoitwa BRI na kumkosoa mtangulizi wake, waziri mkuu mstaafu Giussepe Conte aliyesaini mkataba huo na China mwaka 2019.
Lakini sasa Waziri Mkuu huyo Giorgia Meloni ameanza kuona umuhimu wa China na anataka "kuanza awamu mpya" ya ushirikiano kati ya Rome na Beijing.
Jumamosi 27 July 2024 aliwasili China na atakuwa na ziara ya siku tano. Jumapili 28 July alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa China Li Qiang.
Alipoingia tu madarakani, kwa shinikizo la Marekani na mataifa mengine ya Ulaya akaiondoa Italy kutoka kwenye mpango wa China unaoitwa BRI na kumkosoa mtangulizi wake, waziri mkuu mstaafu Giussepe Conte aliyesaini mkataba huo na China mwaka 2019.
Lakini sasa Waziri Mkuu huyo Giorgia Meloni ameanza kuona umuhimu wa China na anataka "kuanza awamu mpya" ya ushirikiano kati ya Rome na Beijing.
Jumamosi 27 July 2024 aliwasili China na atakuwa na ziara ya siku tano. Jumapili 28 July alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa China Li Qiang.
"Italy ina nia ya kuanza awamu mpya, kuzindua upya ushirikiano wetu baina ya nchi hizi mbili.β
Giorgia Meloni (PM Italy)
Giorgia Meloni (PM Italy)
Pia ameshiriki kongamano la kibiashara na kutia saini ushirikiano wa miaka 3 katika sekta mbalimbali za kiteknolojia na kibiashara ambazo China imekuwa ikifanya vizuri:
- Ship building
- Aerospace
- Electric Vehicles (EVs)
- AI technology
Meloni alisema wanatambua kuwa Italy haina uwiano sawa wa kibiashara na China (trade deficit) hivyo akaomba Italy ipate nafasi zaidi katika soko la China.
Italy inakabili trade deficit katika biashara na China, inanunua bidhaa nyingi za China kuliko inavyouza bidhaa zake China.
Katika kongamano la biashara kati ya China na Italy, Meloni aliongozana na wawakilishi wa makampuni ya Italy kama vile kampuni kubwa ya kutengeneza matairi ya Pirelli, energy group ENI (zamani iliitwa Agip), defence group Leonardo, makampuni ya luxury fashion kama Dolce & Gabana, watengenezaji wa wine n.k.
Jumatatu anatarajia kufanya mazungumzo na raisi wa China, Xi Jinping.
Miaka hii ni ngumu sana kuikimbia China katika biashara, teknolojia na infrastructure. Who's next European leader will visit China? Lets wait and see!
Jumatatu anatarajia kufanya mazungumzo na raisi wa China, Xi Jinping.
Miaka hii ni ngumu sana kuikimbia China katika biashara, teknolojia na infrastructure. Who's next European leader will visit China? Lets wait and see!