Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 21,237
- 31,811
sera ya elimu ya taifa ya mwaka 2014 inataka primary education watoto wasome kwa miaka 9 mpaka 10 sasa wewe unapinga pinga tu bila kujua sera ya elimu ya taifa?Nimeisoma ilani ya CHADEMA sura ya tano ibara ya saba kifungu "e" nimekiambatanisha hapa chini, kinasema ili kuboresha elimu shule ya msingi itakuwa miaka tisa, binafsi ningependa shule ya msingi iwe miaka mitano, lengo la shule ya msingi kama lilivyo ainishwa na Friedrich Froebel ni kumuandaa mtoto kuanza maisha ya elimu na sio kumpa stadi za maisha.
Halafu kifungu "f" wanasema wata integrate na elimu ya ufundi yaani mwanangu anapenda kuwa daktari unaanza na kumfundisha uchomeleaji vyuma, naona sio sawa. Hebu tuiache elimu kama ilivyoasisiwa na akina Friedrich Froebel na Johann Friedrich Oberlin. Pamoja na kasoro ndogondogo ilani ina mambo mazuri pia ni bora wakatumia muda wao kuyaelezea.View attachment 1556345