Chochote kizuri nikimhusisha mama kinakufa

Chochote kizuri nikimhusisha mama kinakufa

Nawambiaga watu ukiwa unatafutanmaisha ukijua bado hujatusua wala huna any power nyuma yako..

Jitenge na Ndugu na wote wanaokujua yani wanaojua chimbuko lako,nenda mbali kasake maisha yako.

Kuna kitu kama hiyo inamtokea mdogo angu kwa namna yake, sababu naijua na siwezi mwambia Hachelewi niambia "kaka dunia imekuharibu" ukizingatia Asili yetu ulokole ndio kabisa.

Maisha haya ukitaka ufanikiwe kaa mbali na wanaokujua.

Watu huniambia silogeki Lakini hapana si kweli mimi ni mtu ambae sitaki kuzoeleka wala kujulikana wala ile Urafiki wa ndaniiii maana najua adui hupitia humo humo.

Watu huja serious na kuniomba niwapeleke kwa mganga wangu lakini hakuna siri kubwa ktk hii dunia kama Kuwa JESHI LA MTU MMOJA.

Wazazi,Ndugu,marafiki ni wamuhimu katika maisha yetu lakini katika upande na maswala ya mafanikio Binafsi hao watu wana asilimia chache sana za wewe kufanikiwa.

Ili ufike mbali zaidi ni lazima ujitenge na wote hao sehemu wasiokujua ANZA utaona utakavyofanya kila kitu kinafunguka.

Kuna watu wananifata PM kuniambia kila kazi wanayojaribu kufanya inakufa,biashara zina kufa Nawambiaga Hii SIRI ya kujitenga lakini wananchukulia kama nakosa cha kuwashauri, ila kuna faida kubwa sana kuishi na jamiii isiyojua wewe ni nani.

Unakua kama umezaliwa UPYA.
Asante sana
 
Correlation is not causation.

Inawezekana mtambo wa maji ya line inayokuja kwako ukawa unaruhusu maji yaingie sumu kila Jumapili jioni, labda kuna mfanyakazi mzembe zamu yake ni Jumapili jioni hajui kuweka filter ya kuzuia sumu kuingia kwenye maji line ya mwisho kuingia kwako, na mama yako anakuja kukutembelea kila Jumapili jioni.

Ukaona kila Jumapili jioni mama yako akija kukutembelea watu wa nyumbani kwako wanaumwa, kwa kunywa maji yenye sumu.

Ukasema huyu mama yangu ni mchawi, kila Jumapili jioni akija, watu wanaumwa.

Kumbe ni mambo tofauti yanaendana, bila moja kuwa sababu ya jingine.

Ila, kwa tabia zetu za kukimbilia kuunganisha mambo kichawi, huyo mama haponi hapo.
unakataa kiaina!
 
Mimi pia nina tatizo hili. Ni mwaka wa pili tangu nifahamu kwamba Kila ninachomshirikisha mama kinafeli. Kwa sasa najikusanya nihame mkoa kwa siri na kamwe sirudi hata nikisikia amefariki siji kumzika.

Nimejaribu ku Link dots hata huu umaskini unaotuandama unasababishwa na yeye.
Aisee!!

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Yaani nimefuatilia tangu kipindi nasoma, siku nikimuambia tarehe ya mitihani huwa ananiambia ataniaombea, huo mtihani hata kama ni mrahisi lazima nifeli. Siku nisipomuambia nitafauli hata kama huo mtihani ni mgumu

Michongo mingi ya kitaa nikimshirikisha lazima iende tofauti.

Mwaka huu nimekuja kuhitimisha kwamba mawazo yangu ni sahihi baada ya kufanya jaribio hili; Nimemshirikisha kwamba nitaotesha alizeti ekari 2 kwenye shamba la nyumbani akaniunga mkono. Nikanunua mbegu ya alizeti inayotosha ekari 4 nikaotesha ekari mbili hapo nyumbani, then nikaotesha ekari 2 kwa siri kwenye shamba la kukodi hapo jirani na shamba letu. Cha ajabu ile ya shamba la nyumbani haikuota lakini ile niliyootesha kwa siri imeota yote na inaendeleanvizuri kabisa. Kumbuka haya mashamba yamekaribiana sana; jiografia ni moja na tabia ya nchi ni moja. Hapo ndipo ni kahakikisha kwamba mawazo yangu ya mda mrefu ni ya kweli.
Kazi ya shetani hiyo

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom