Chondechonde Maalim Seif Sharif Hamad

Chondechonde Maalim Seif Sharif Hamad

wakiingia itakuwa nafasi nzuri ya kudai katiba mpya na tume huru ndani ya system kuliko kudai wakiwa nje ya system.
Ccm watakuwa na kichaa kukubali tume huru, tume ya 2015 ilikuwa na wajumbe kutoka kambi ya maalim seif lakini kilichotokea uchaguzi kufutwa bila wajumbe wa maalim kujulishwa.
 
Hata ikibidi wazungumze basi sio lazima maalim awe VP.

Act wazalendo watafute yule wanae muona kuwa anafaa kuwa mrithi wake.

Maalim yupo 77 sasa abaki kuwa mwenyekiti wa Act kukijenga chama zaidi.

VP waitoe hio nafasi kwa Dkt Faki aliekua mgombea mweza wa Membe au Othman Masoud aliekua Mwanasheria mkuu Zanzibar.

Maalim Atumie muda huu kukijenga Act na kuwajenga kisaikolojia wazanzibari wenye imani naye miongo ya 4 kuwa Struggle bila ya yeye inawezekana zaidi
Biden ana 77 pia, na Trump ana 74
 
Kwa ushauri tu,seif akubali tu,maridhiano,kugombana sio vizuri
 
Kumbuka kuna watu wako ndani na haijulikani mustakbali wao, kuna wale waliosafirishwa kupelekwa Tanganyika akina Mazuri Naibu Katibu wa ACT-Wazalendo lakini kuna wengine wengi Unguja na Pemba wanateswa kinyama, pia wewe hujui kinachoendelea kuna familia wamekimbia kusikojulikana kama pale Ngwachani Pemba kijiji kizima kimesambaratika kusikojulikana mateso kila aina kwa wapita njia eneo lile mpaka uonyeshe kitambulisho kama unakaa nje ya Ngwachani ndio unapita. Kule shumba Pemba karibu watu 60 wako ndani na mateso na kila siku polisi wanaenda kuangalia nani amerudi kijijini wanamshika zinaachwa nyumba za wana ccm tu.

Mimi nadhani maalim anaweza kukubali kwa masharti ili kunusuru zile familia ziwe huru na watu wengine ambao wanaumizwa kinyama. Kama watakubali kuwaacha huru ni bora kuliko hayo mengine watu watavumilia mpaka Mungu mwenyewe atakapoleta wepese juu ya hao madhalimu waliokubuhu.
Siwezi kubaliana na hilo. Kama wameamua kuuwa waache waendelee kuuwa lakini kurudi nyuma na kuingia kwenye mtego wao ni kujimaliza na kuziua hizi harakati za ukombozi.
 
Back
Top Bottom