CHRISTMASS ni ya kina Pope Julius I au ni yetu sisi na Yesu wetu?

CHRISTMASS ni ya kina Pope Julius I au ni yetu sisi na Yesu wetu?

Je ni maagizo kwa mujibu wa maaandiko? Au ni matakwa yako binafs..?

#MaendeleoHayanaChama

Jibu maswali yangu kwanza maana ndipo lilipo jibu lako. Kama kuna andiko litoe wewe unaeona kubadili siku ama tarehe kumeainishwa kama dhambi ipi ama kuvunja sheria ipi

Nikifanya kama inavyofanywa au nikatenga siku maalumu ya kuadhimisha kifo au kuzaliwa kwa Kristu. Nikafanya sala, kufunga na kumkiri kiimani.

Je, ninapata athari gani kiroho kwa kubadilisha siku hata kama ingekuwepo
 
Hakuna kinachoweza kubadilika, wewe kesho kula pilau tu.
 
wakina papa ndo wa anzilishi wa uchafu wote huu wakuchafua maandiko.watu mpaka Leo.wanajua siku inaisha saa6 usiku.wametu aminisha mungu.ana mtoto.tumekubali ukiwauliza mungu alizaa na nani uyo mtoto.wana kwambia ni mambo ya kiroho zaidi.japo Mimi ni mkristo ila sikubali kwamba mungu ana mtoto.maana nikujitoa akili.mungu.anazaha..
 
Sasa shida hapo iko wapi?? Kama warumi walikuwa wanaabudu na kusherehekea sikukuu ya Mungu jua tar. 25.. kisha Papa akaona huo ni upuuzi na ni afadhali hiyo siku tumsherehekee Mungu wa kweli, hapo ubaya upo wapi? Maana siku zote na tarehe ni vya Mungu... Inaonekana kinachokusumbua wewe ni siku hiyo ya tarehe 25... Ila elewa kuwa kwa wakristo suala kubwa sio tarehe wala siku bali ni kuzaliwa kwa mwokozi.. na hata pasaka ni hivyo hivyo ishu sio siku wala saa bali kufa na kufufuka.
Umemaliza kila kitu, ila kwa Mtu punguani mwenye asili ya ubishi atapingana nawewe
 
Biblia haituelekezi kusherehekea birthday ya Yesu, lakini Yesu mwenyewe alituagiza kukumbuka kifo chake yaani kusherehekea Pasaka, kwani hili ndilo tendo lililoleta ukombozi wa mwanadamu, kwa hiyo wanadamu wana ukaidi fulani wa kufanya mambo ambayo hawakuagizwa na kuacha yale waliyoagizwa, cha muhimu ni kufuata maagizo ya neno la Mungu tusifanye mambo kwa mkumbo kwa sababu siku ya mwisho kila mtu atajitetea mwenyewe, yaani mbele za Mungu huwezi kumsingizia kiongozi wako wa dini utaulizwa ulijua kusoma na kuandika utajibu ndio, ulisoma maandiko yanasemaje? basi.
Yesu alikuagiza waumini wasome Biblia kwa njia ya simu? Aliagiza watu waingie ibadani na suti?

Halafu hebu fahamuni neno ''KUADHIMISHA'' hamtapata shida yote hii.
 
wakina papa ndo wa anzilishi wa uchafu wote huu wakuchafua maandiko.watu mpaka Leo.wanajua siku inaisha saa6 usiku.wametu aminisha mungu.ana mtoto.tumekubali ukiwauliza mungu alizaa na nani uyo mtoto.wana kwambia ni mambo ya kiroho zaidi.japo Mimi ni mkristo ila sikubali kwamba mungu ana mtoto.maana nikujitoa akili.mungu.anazaha..
Wewe ni Mfuasi wa Mwamedi na kama wewe ni Mkristo basi ni Mkristo jina

Hakuna Mkristo sahihi asiyeamini katika TRINITY
 
Wewe ni Mfuasi wa Mwamedi na kama wewe ni Mkristo basi ni Mkristo jina

Hakuna Mkristo sahihi asiyeamini katika TRINITY
najua ukristo auna shida ila kuna wahuni wachache wali uchanganya na upagani ndani yake.ila ukristo walio kuwa wanafundisha wanafunzi wa yesu.ushaalibiwa ndo maana kwenye ukristo. kuna madhehebu mengi mengi ujue.kuna shida.
 
Kwanza, hii calendar tunayotumia(wanaiita gregory calendar nadhani) ilianza lini?
wasaalam, wakuu

Ninaandika haya huku , nikijua nitapingwa zaidi kuliko kuungwa mkono.

Naandika huku nikitaraji pia dhihaka na kashfa kuliko majadaliano yenye mapenzi mema

Naandika sio kwa vile naelewa athari za upagani katika dini na madhehebu yetu

Naandika kwa sababu naelewa ,maafa ya kibinaadamu ambayo wapagani na nyingi zao mila na desturi ambazo zimeacha nyuma katika madhehebu yetu na dini zetu.

Naandika kwasababu pia mimi sio wa kwanza kuandika hapa na wala si wa mwisho kuandika haya.

Naandika kwasababu nilitamani kuandika hiki na nmeandika.

Tumezoea makala za namna hii kwingi tuendako katika majira haya ,lakini kila zama zinavyozidi kujongea taswira mpya inajengeka ndivyo navyo tunazidi kukumbushana kwa hekima njema

Basi

Kama utauliza popote duniani kuhusu 'christ mass' majawabu yake yatakuwa ni sikukuu ya kuzaliwa bwana yesu....lakini moja kwa moja hilo sio jibu la kweli la swali hilo ......kama ungeli ipata na ungelirejelea vitabu vya history ya kale na biblia kwa ujumla ungelipata sababu ya kupinga na kupangua kumbukizi hii ya mazazi ya kiongozi na mwokozi yesu kristo.
View attachment 1655856
Katika injili zote haijapata kuwepo thibati, ya bwana YESU eti ya kwamba alizaliwa majira yapi?? na tarehe zipi.

Na mpaka ilipofikia mwaka 349 AD dunia haikuwahi kuwa na sikukuu ya kusherekea mazazi ya bwana yesu.

Kila ifikapo tarehe 25 Disemba watu husherekea kuzaliwa kwa bwana yesu na Wengi wetu kwa pumbao letu tulilo nalo tunaamini hiyo ni siku haswa bwana mwokozi alipoletwa duniani na mama yake, mama mwema , mtakatifu, mkarimu, mweupe wa moyo na nafsi alietakasika kabisa MARIAMU hata ALLAH (s.w) katika QUR'AN akamtaja na kuwa mwanamke pekee aliyetajwa katika maandishi hayo matukufu Sio kumtaja tu LaHashaa! ALLAH (s.w) akampa sura yake kabisa Mama wa Yesu (amani za mwenyezimungu ziendelee kuwa naye huko aliko)

Lakini ni kweli bwana YESU alizaliwa 25 disemba???
View attachment 1655857
Ninajua kwamba bwana Yesu Hakuzaliwa mwishoni mwa mwaka,, kama ni hivyo sitakuwa na mashaka nikikuambia ya kwamba ninajua pia bwana yesu alizaliwa katikati ya mwaka wa 6 kuelekea wa 5 B.C.

Thibati hiyo ya Bwana Yesu kuzaliwa Katikati ya mwaka wa 6 kwenda wa 5 BC Pia imetambulika na Biblia ijulikanayo kwa jina la
Life Application Study Bible , katika ukurasa wa A20 .

Lakini hata maelezo yameeleza kwa ufupi kuzaliwa kwa bwana yesu na yanatosha kuonyesha 25 disemba sio sikukuu ya kuzaliwa bwana


Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, kwa msichana mmoja bikira aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu, ewe uliyejaliwa neema na Mungu! Bwana yuko nawe!” Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: Maneno hayo yanamaanisha nini? Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu..... LUKA 1:26-31

Mafundisho hayo yanagongea msumari , kwamba habari za kupokea taarifa za mimba kwa Mariamu kulitokea mwezi wa sita ,na kama ujuavyo mwezi huo kwa jamii za kale nyingi hata zama za sasa ni mwezi wa katikati ya mwaka.....
wasomi wa histori wengi wamejaribu kuonyesha mwezi wa saba napo ndipo Mama mariamu alichukua mimba yake na akazaa kwa utimilifu pasi na kasoro yoyote.... kwa maana mtoto hakuwa na kasoro yoyote ya muda.

ikawa katika kukaa huko siku zake za kuzaa zikatimia ,akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni. LUKA 2: 6-7

Pasi na shaka bwana yesu alizaliwa katika mda timilifu kabisa

Tutake nini tena??? tuombe tujue na tusijue


pia ukirejelea mwanzo na takwimu hizo, hata mwaka wa kwanza A.D bwana Yesu tayari alikuwa na umri wa miaka mitatu na Nusu,, Na hapo pia panakinzana na ile dhana inayosemwa na wengi kuwa Bwana Yesu alipozaliwa ndipo miaka ikaanza kuhesabiwa....(ni vyema ukaingia mtandaoni kupata taarifa kwa uyakinifu zaidi)

POPE JULIUS WA I

Hilo fundisho kuhusu Bwana Yesu kuzaliwa tarehe 25, ya mwezi wa Disemba ni POPE shupavu wa roman aitwae Julius I alitangaza rasmi kuwa tarehe 25 Disemba ndiyo itakuwa siku ya kusheherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.......Pia hii ilikuwa siku ambayo wapagani wa walikuwa wakisherehekea kuzaliwa kwa Mungu wao, mungu jua na mwanzo wa majira ya michepuo ya mimea basi JULIUS akaingiza siku hiyo kwa minajili ya mungu wao wapagani wa rumi ili afanyiwe matukuzo na kuwatia katika makufuru wana wa Adamu
View attachment 1655853
Katika majira hayo hayo pia kulikuwa na sikukuu ya wapagani wa Kirumi inajulikana sana kwa jina la “Roman Saturnalia” ambayo pia Waroma walikuwa wanampa heshima mungu wao SATURN, ambaye wao walikuwa wanamwabudu....Mungu huyu ni sayari ya SATANI
Waroma walikuwa wanasherekea sherehe hiyo kila tarehe 19 ya mwezi wa Disemba na ilikuwa inaadhimishwa kwa kufulululiza kwa siku saba hadi tarehe 25 ya mwezi huo wa Disemba ndipo maadhimisho ya siku kuu hiyo yalipohitimishwa.
View attachment 1655860
Pia ilipofika miaka ya elfu na miamoja (1100s )AD Warumi walitangaza kuwa sikukuu (christmass) hii ni ya kidini na wakaweka ulazima pasi na shuruti kwa mataifa yaliyo chini ya makoloni yake kuifata na kutenga fedha kwa ajili ya sikukuu hii....pasi hiari

Kuna kiongozi wa ukatoliki wakati huo mjanja mjanja mmoja bwana nicholas....alifanikiwa kuzishawishi nchi nyingi za ulaya kuipokea sikukuu hii kama ndiyo sikukuu ya kidini na kitaifa ,, umashuhuri wa christmass ukaongezeka na uliendelea kuwa mkubwa miaka ya 1500 AD.

Na hapo ndipo uliponza kujitokeza mgawanyiko mkubwa mno katika ukristo,,jambo lililopelekea kuanzishwa kwa madhehebu mengi ya kikristo ya kiprostentanti, mpaka sasa yanakadiriwa kufikia takribani 3000..

Lakini mgawanyiko huo wa madhehebu ulisaidia sana kufichua mambo mbalimbali na kutoa uhuru wa mafundisho mengi mengi na hapo wakristo wengi walipata mwanya wa kueleza namna na maana ya christmass ni UPAGANI tena ni sherehe ya kutungwa.

Haya mafundisho yalifanya UINGEREZA kuiondoa sikukuu hiyo mwaka 1600 AD, kama sikukuu yake ya kitaifa na kidini hata katika makoloni yake yote.
View attachment 1655866
Hata hivyo tamaduni ya sherehe hizi zilirudi kwa sura ya pili ya kikristo.....ambapo mtindo wa kusherekea wa sasa uliambatana na kupambwa kwa miti ya krismass katika makanisa na kutumina kadi za salam zilizosheheni maandiko ya biblia takatifu na maadhimisho yakazidi kupamba moto kila mwaka hata sasa katika zama zetu za kina SANTA CLAUS
View attachment 1655864

DA'VINCI XV
 
... hakuna mahali maandiko yanasema ifanywe kumbukumbu..pasaka tu ndiyo alisema ifanywe kumbukumbu..
Na hakuna anayelazimishwa kufanya kumbukumbu, kila mtu na imani yake. Kama unaona si sawa kukumbuka siku ya kuzaliwa mwokozi ila ni sawa kukumbuka kuzaliwa kwako, hakuna shida yoyote maana ni imani yako, na si jambo jema kumshangaa anayefanya kumbukumbu ya kuzaliwa mwokozi wake. Kama tungekuwa tunaelewa maana ya IMANI, hata huu uzi haungestahili kuanzishwa maana wanaoadhimisha kumbukumbu sio wa imani moja na mleta uzi na wafuasi wake

Yaani ni sawa na na mwana CCM kushangaa ACT Wazalendo kuwa na cheo cha Kiongozi wa Chama eti kwa kuwa hakipo CCM, wakati katiba yao ACT inawaelekeza kuwapo kwa cheo hicho
 
wakina papa ndo wa anzilishi wa uchafu wote huu wakuchafua maandiko.watu mpaka Leo.wanajua siku inaisha saa6 usiku.wametu aminisha mungu.ana mtoto.tumekubali ukiwauliza mungu alizaa na nani uyo mtoto.wana kwambia ni mambo ya kiroho zaidi.japo Mimi ni mkristo ila sikubali kwamba mungu ana mtoto.maana nikujitoa akili.mungu.anazaha..
Kwanza hakuna Mkristu anayeandika kwa makosa mengi ya kiuandishi kama haya
 
tusherekeeni tu hizi sikukuu za wenzetu maana hamna namna🍾🍾🍾
visikukuu vyetu hivi saba saba sijui nane nane hakuna vibe kabisa
 
Kuna kiongozi wa ukatoliki wakati huo mjanja mjanja mmoja bwana nicholas....alifanikiwa kuzishawishi nchi nyingi za ulaya kuipokea sikukuu hii kama ndiyo sikukuu ya kidini na kitaifa ,, umashuhuri wa christmass ukaongezeka na uliendelea kuwa mkubwa miaka ya 1500 AD. Na hapo ndipo uliponza kujitokeza mgawanyiko mkubwa mno katika ukristo,,jambo lililopelekea kuanzishwa kwa madhehebu mengi ya kikristo ya kiprostentanti, mpaka sasa yanakadiriwa kufikia takribani 3000..

Haujiulizi, kama sababu ya madhehebu kujitoa katika Ukatoliki ilikuwa ni moja (common), ni kwa nini basi yaanzishwe mengi kwa sababu hiyo hiyo? Kama A amejitoa katika B kwa sababu fulani, kuna haja gani na C kujitoa katika B na kuanzisha dhehebu lake kwa sababu ile ile? Kwa nini asimfuate A kwa kuwa sababu yao ya kujitoa katika B ni ile ile?
 
Mtoa post ungetoa na ushauri pia.
Dhidi ya Yesu kutokuzaliwa njiti, usilazimishe kwani hata mimba yenyewe ilitungwa kwa uwezo wa Roho Mtakaktifu. (shangaa hili kwanza)
Na kama tarehe 25 ilikuwa ni sikukuu ya kipagani na badala yake imegeuzwa kuwa ni sikukuu ya wakristo kusherekea kuzaliwa kwa Yesu ubaya uko wapi?
Kule makanisani anatajwa Yesu Kristo hiyo miungu imefutika kabisa ni wewe tu ndio unaifufua kwa faida zako binafsi. Kusanyiko la wakristo limetamalaki.

Haujapata kusikia kuwa vilima vitasawazishwa na mabonde yatafukiwa?
Wana wa Nuru wakishindana na wana wa giza , wana wa Nuru hushinda , pengine ndiyo maana hiyo siku yako ya miungu ikafutiliwa mbali na badala yake ikawekwa Krismas.

Amen!
 
Mwanzo nlipata ugumu ,kidogo ila nikakumbuka yawezekana utakuwa una simu janja ambayo inakuwezesha kupata taarifa mtandaoni , labda kwa kukusaidia ungeanza kumsoma kwanza julius I kwa undani,baada ya hapo malizia na costantine Augusto kama utapenda zaidi utawasoma na hao kina nicholas.

nasikitika kwanini??? sikumzungumzia POPE julius I kwa undani
Mkuu kwa nini hukumzungumzia japo kidogo pope julius, una muda bado waweza hata kwenye comments
 
wasaalam, wakuu

Ninaandika haya huku , nikijua nitapingwa zaidi kuliko kuungwa mkono.

Naandika huku nikitaraji pia dhihaka na kashfa kuliko majadaliano yenye mapenzi mema

Naandika sio kwa vile naelewa athari za upagani katika dini na madhehebu yetu

Naandika kwa sababu naelewa ,maafa ya kibinaadamu ambayo wapagani na nyingi zao mila na desturi ambazo zimeacha nyuma katika madhehebu yetu na dini zetu.

Naandika kwasababu pia mimi sio wa kwanza kuandika hapa na wala si wa mwisho kuandika haya.

Naandika kwasababu nilitamani kuandika hiki na nmeandika.

Tumezoea makala za namna hii kwingi tuendako katika majira haya ,lakini kila zama zinavyozidi kujongea taswira mpya inajengeka ndivyo navyo tunazidi kukumbushana kwa hekima njema

Basi

Kama utauliza popote duniani kuhusu 'christ mass' majawabu yake yatakuwa ni sikukuu ya kuzaliwa bwana yesu....lakini moja kwa moja hilo sio jibu la kweli la swali hilo ......kama ungeli ipata na ungelirejelea vitabu vya history ya kale na biblia kwa ujumla ungelipata sababu ya kupinga na kupangua kumbukizi hii ya mazazi ya kiongozi na mwokozi yesu kristo.
View attachment 1655856
Katika injili zote haijapata kuwepo thibati, ya bwana YESU eti ya kwamba alizaliwa majira yapi?? na tarehe zipi.

Na mpaka ilipofikia mwaka 349 AD dunia haikuwahi kuwa na sikukuu ya kusherekea mazazi ya bwana yesu.

Kila ifikapo tarehe 25 Disemba watu husherekea kuzaliwa kwa bwana yesu na Wengi wetu kwa pumbao letu tulilo nalo tunaamini hiyo ni siku haswa bwana mwokozi alipoletwa duniani na mama yake, mama mwema , mtakatifu, mkarimu, mweupe wa moyo na nafsi alietakasika kabisa MARIAMU hata ALLAH (s.w) katika QUR'AN akamtaja na kuwa mwanamke pekee aliyetajwa katika maandishi hayo matukufu Sio kumtaja tu LaHashaa! ALLAH (s.w) akampa sura yake kabisa Mama wa Yesu (amani za mwenyezimungu ziendelee kuwa naye huko aliko)

Lakini ni kweli bwana YESU alizaliwa 25 disemba???
View attachment 1655857
Ninajua kwamba bwana Yesu Hakuzaliwa mwishoni mwa mwaka,, kama ni hivyo sitakuwa na mashaka nikikuambia ya kwamba ninajua pia bwana yesu alizaliwa katikati ya mwaka wa 6 kuelekea wa 5 B.C.

Thibati hiyo ya Bwana Yesu kuzaliwa Katikati ya mwaka wa 6 kwenda wa 5 BC Pia imetambulika na Biblia ijulikanayo kwa jina la
Life Application Study Bible , katika ukurasa wa A20 .

Lakini hata maelezo yameeleza kwa ufupi kuzaliwa kwa bwana yesu na yanatosha kuonyesha 25 disemba sio sikukuu ya kuzaliwa bwana


Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, kwa msichana mmoja bikira aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu, ewe uliyejaliwa neema na Mungu! Bwana yuko nawe!” Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: Maneno hayo yanamaanisha nini? Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu..... LUKA 1:26-31

Mafundisho hayo yanagongea msumari , kwamba habari za kupokea taarifa za mimba kwa Mariamu kulitokea mwezi wa sita ,na kama ujuavyo mwezi huo kwa jamii za kale nyingi hata zama za sasa ni mwezi wa katikati ya mwaka.....
wasomi wa histori wengi wamejaribu kuonyesha mwezi wa saba napo ndipo Mama mariamu alichukua mimba yake na akazaa kwa utimilifu pasi na kasoro yoyote.... kwa maana mtoto hakuwa na kasoro yoyote ya muda.

ikawa katika kukaa huko siku zake za kuzaa zikatimia ,akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni. LUKA 2: 6-7

Pasi na shaka bwana yesu alizaliwa katika mda timilifu kabisa

Tutake nini tena??? tuombe tujue na tusijue


pia ukirejelea mwanzo na takwimu hizo, hata mwaka wa kwanza A.D bwana Yesu tayari alikuwa na umri wa miaka mitatu na Nusu,, Na hapo pia panakinzana na ile dhana inayosemwa na wengi kuwa Bwana Yesu alipozaliwa ndipo miaka ikaanza kuhesabiwa....(ni vyema ukaingia mtandaoni kupata taarifa kwa uyakinifu zaidi)

POPE JULIUS WA I

Hilo fundisho kuhusu Bwana Yesu kuzaliwa tarehe 25, ya mwezi wa Disemba ni POPE shupavu wa roman aitwae Julius I alitangaza rasmi kuwa tarehe 25 Disemba ndiyo itakuwa siku ya kusheherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.......Pia hii ilikuwa siku ambayo wapagani wa walikuwa wakisherehekea kuzaliwa kwa Mungu wao, mungu jua na mwanzo wa majira ya michepuo ya mimea basi JULIUS akaingiza siku hiyo kwa minajili ya mungu wao wapagani wa rumi ili afanyiwe matukuzo na kuwatia katika makufuru wana wa Adamu
View attachment 1655853
Katika majira hayo hayo pia kulikuwa na sikukuu ya wapagani wa Kirumi inajulikana sana kwa jina la “Roman Saturnalia” ambayo pia Waroma walikuwa wanampa heshima mungu wao SATURN, ambaye wao walikuwa wanamwabudu....Mungu huyu ni sayari ya SATANI
Waroma walikuwa wanasherekea sherehe hiyo kila tarehe 19 ya mwezi wa Disemba na ilikuwa inaadhimishwa kwa kufulululiza kwa siku saba hadi tarehe 25 ya mwezi huo wa Disemba ndipo maadhimisho ya siku kuu hiyo yalipohitimishwa.
View attachment 1655860
Pia ilipofika miaka ya elfu na miamoja (1100s )AD Warumi walitangaza kuwa sikukuu (christmass) hii ni ya kidini na wakaweka ulazima pasi na shuruti kwa mataifa yaliyo chini ya makoloni yake kuifata na kutenga fedha kwa ajili ya sikukuu hii....pasi hiari

Kuna kiongozi wa ukatoliki wakati huo mjanja mjanja mmoja bwana nicholas....alifanikiwa kuzishawishi nchi nyingi za ulaya kuipokea sikukuu hii kama ndiyo sikukuu ya kidini na kitaifa ,, umashuhuri wa christmass ukaongezeka na uliendelea kuwa mkubwa miaka ya 1500 AD.

Na hapo ndipo uliponza kujitokeza mgawanyiko mkubwa mno katika ukristo,,jambo lililopelekea kuanzishwa kwa madhehebu mengi ya kikristo ya kiprostentanti, mpaka sasa yanakadiriwa kufikia takribani 3000..

Lakini mgawanyiko huo wa madhehebu ulisaidia sana kufichua mambo mbalimbali na kutoa uhuru wa mafundisho mengi mengi na hapo wakristo wengi walipata mwanya wa kueleza namna na maana ya christmass ni UPAGANI tena ni sherehe ya kutungwa.

Haya mafundisho yalifanya UINGEREZA kuiondoa sikukuu hiyo mwaka 1600 AD, kama sikukuu yake ya kitaifa na kidini hata katika makoloni yake yote.
View attachment 1655866
Hata hivyo tamaduni ya sherehe hizi zilirudi kwa sura ya pili ya kikristo.....ambapo mtindo wa kusherekea wa sasa uliambatana na kupambwa kwa miti ya krismass katika makanisa na kutumina kadi za salam zilizosheheni maandiko ya biblia takatifu na maadhimisho yakazidi kupamba moto kila mwaka hata sasa katika zama zetu za kina SANTA CLAUS
View attachment 1655864

DA'VINCI XV
Ningependa kuchangia mada hii LAKINI nimesita baaada ya kuipitia yote na kuona uelewa wa mleta mada. Kitu mabacho nataka nimkumbushe mleta mada ni kuwa hata katika maandishi ya kwaida, majina siku zote yanaandikwa kwa herufi kubwa. Kwa mfano si sahihi katika lugha yoyote kuandika jina la mtu kwa herufi ndogo, huwezi kuandika kwa mfano john joseph au mohamedi n.k. Hivyo namshauri anapoandika majina yoyote ayaandike kwa herufi kubwa! Inapendeza.
 
Christmas is not a Biblical festival. Hii ni sikukuu kama siku nyingine za kihuni duniani, Ni kama siku ya kuwakumbuka ma kayaman wote
Mzee katika Ukristo hakuna sikukuu zinazoamriwa kibiblia. sikukuu zote zimetokana na maazimio ya waumini walioona ni vema kukumbuka ukweli fulani ya imani na kuikumbuka kwenye siku maalumu.
Hakuna amri kukumbuka siku ya kufufuka kwa Yesu (Pasaka) wala hakuna amri ya kukumbuka kufika kwa Roho Mtakatifu kwa watu wengi (Pentekoste) wala kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu (Krismasi).
Kwa Pasaka na Pentekoste hao waumini wa siku za kwnaza waliweza kutumia tarehe zilizotajwa katika Biblia kwa hiyo walipanga tarehe zilizofaa na taarifa (kwa ufahamu wao - maana kalenda zilibadilika hivyo kila tarehe ni ya kibinadamu).
Kuhusu Krismasi hakuna dokezo la tarehe, Hivyo waliteua siku kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu.
Ambako hakuna ubaya, maana katika Ukristo hakuna amri wala maagizo kutoka Mungu kuhusu tarehe fulani.

Ndugu Waislamu wengi wanapenda sikukuu ya Maulidi, ambayo pia si tarehe ya kuzaliwa ya Mtume bali sikukuu iliyoanzishwa karne kadhaa baadaye. Waislamu wengine wanaipinga wakidai si halali kuanzisha sherehe isiyoamriwa katika Qurani au sunna ya mtume mwenyewe.

Waingereza husheherekea Queens Birthday kwenye mwezi ulioteuliwa kwa sababu hali ya hewa inafaa zaidi kwa sherehe ya umma, si kwenye siku alikozaliwa.

Ubaya wapi?
 
Back
Top Bottom