Chuki binafsi ya Haji Manara kwa Shaffi Dauda inatokana na nini?

Haji aliwahi kukiri insta kuwa anaugomvi binafsi na shaffih... Sasa nkajiuliza kama anaugomvi binafsi Kwann anamuatatack dauda katika Mahala pasipo sahihi??

Dauda alipost Picha yammoja wa wachezaji wa simba akiwa ameediti Picha ikiwa nusu jezi nyingine.. Haji aliwaka sana.. Nkajiuliza kosa la shaffih pale ni lipi??
Siamini kama haji anafaa kuwa msemaji wa timu... Haji alitakiwa awe na cheo cha uhamasishaji wa mashabiki wa simba na si msemaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haji Manara anakosa diplomasia/busara katika kuitumikia nafasi yake. Ana maneno ya chuki na majigambo. Hizo si sifa za msemaji mkuu wa Taasisi. Hatakiwi kuanzisha "attack"/confrontations" kwenye vyombo vingine, anadhalilisha cheo chake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shaffih ana wivu wa kike kwa Simba sababu ya kubaniwa kuingia. yanga mbona ilipangwa kundi la kiubwete kombe la shirikisho na ikaburuza mkia. Lakini wala hakufungua bakuli lake kukosoa. Boban kasajiliwa yanga kimyaa, lakini Simba ilivyomsajili boko na baadaye kagere kakurupuka oooh wazee!! Tena kwenye kiblog chake alikuwa anamtumia dogo mmoja mwandishi mwenye akili za kipunga kuiponda Simba. Anaitwa Baraka Mbolembole, yaani yeye anatoa makala siku Simba ikifungwa tu.Acha atolewe upepo na wivu wake wa kike.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchambuzi gani wa kuikatisha tamaa Simba kila kukicha ? Kilasiku kilasiku Simba mbovu Simba vibonde.
Atoe basi hata pongezi kwa kuifikia hiyo hatua. Mchambuzi akitoa maoni, anatoa na mbinu ya kuweza kuuondoa huo ubovu anaouona kama wenzake wanavyofanya.
Aseme basi ubovu wa Simba uko wapi na urekebishwe vipi. Na sio kila kukicha ukiona anaizungumzia Simba basi kauli ni mbovu mbovu mbovu, vibonde,vibonde vibonde kila siku za uchambuzi.
Huu ni uchambuzi au udhalilishaji ?
Huu ni ukatishanaji tamaa. Aseme basi anataka Simba ijitoe ktk hayo mashindano au vipi ?
Mbona maneno ya kejeri kila kukicha ?
Huu sio uchambuzi ni ubabaishaji wenye nia ovu ya kuikatisha tamaa timu.
Wachambuzi ni akina Ally Mayai na Mwalimu kashasha.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakuunga mkono shafii ni bogas Amuige mwenzie Edo Kumwembe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dauda si mchambuzi mzuri nina shaka na vyanzo vyake vya habari anatulisha sana matango poli kwa upande wa manara naona anaifanyia vizur tu taasisi yake tatizo watu wanachukua mambo binafsi kuliko ya kazi yake ninyi ndio mtakuwa mnashindana nae insta kule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali kama mchambuzi kwanini unachambua kwa upendeleo yanga huyu bwana hajawahi kuiponda lakin simba anaiita underdog huuu niujinga wa kupindukia

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani akiita underdog ni tatizo! Au ni tusi? Ni vema wakiiona hivyo ili wasijiandae vya kutosha baadae wanapokutana Simba iwaonyeshe kazi kuliko kuonekana mabingwa na jamaa wakaingia kwa nguvu zote ikawa aibu nyumbani na Ugenini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtazamo wangu, Haji kuitetea simba ni haki yake. Tatizo kwa Dauda, yeye ni mtangazaji na inatakiwa asionyeshe ushabiki wake umeegemea wapi wakati anachambua mambo ya vilabu.

Binafsi huwa simsikilizi Dauda maana huwa anajenga hoja za kukosoa tu na kuponda hata pale panapohitaji pongezi. Mbaya zaidi anatumia hisia za ushabiki wake binafsi na sio facts za kiuchambuzi.

Mfano uchambuzi wake wa juzi baada ya simba kuitoa khana, jamaa kakomalia kuhusu mafanikio ya yanga badala walau kuipongeza simba.

Pia ukimsikiliza hata kwa timu za ulaya, ni mnazi anaeipinga Man United waziwazi kwa hisia zake na sio facts.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tuache ushabiki tuje kweny ukweli japo huwa mchungu uliyosema ni kweli 100%√√√ manara anatuponza sana Simba na hana tofaut na Masau bwile nae anaiponza timu yake ukiongea maneno mbovumbovu ya kujiamini sana kuwa lazima nitamfunga mshindani wangu nae anajipanga ili kuficha aibu na. Kutaka kukata kauli zako hata kama hana faida na matokeo ushindi ktk ule mchezo ila kwa matusi yako na namna ulivojigamba aanaamua kukuzia kwani ni uongo mara ngap tunaona simba tunacheza na vitimu vya kawaida na vinatukamia na mwisho wa siku tunaaibika kwa kichapo kama sio suhuru nk... Manara ajitathimini kwa mwendo wake huo hatufai abadilike la sivo apige chini anajisifu sana acha majisifu fanya v oh vizur watu wakusifie sio ujisifu wewe no narudia tena kama manara hatabadilika na akaachwa aendelee kuwa msemaji wa simba tutakuwa na wakat mgumu sana kuwahi kutokea.. Pamoja na kuwa na hera pia na kikosi kizuri yangu ni hayo tu.. Nampenda msemaji wa yanga au azam akihojiwa anavojibu hadi raha lakini huyu. Mwite wetu ni shida ki2 kidogo tu mijisifa kibao mpaka anaharibu kama sio kuboa.. Ni kweli ktk michuano hiyo ya club bingwa afrka sisi simba ni underdog kwan kuna ubishi hapo ila tu mpira unadunda na mwamzi ni dakika 90 ila ukweli lazima usemwe kama ulivo.. Otherwise time will tell.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
Huyo Haji ana tatizo zaidi ya hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…