Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani

Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani

Nazidi kuamini maneno ya jamaa mmoja kuhusu hawa watoto waliozaliwa miaka ya 2000. Hawa watoto ni changamoto mno! Hawana adabu wala akili, wao kila wanachofanyia gizani wanataka tusiokuwepo pia tuyafahamu.
Yani waliona ni sifa kabisa kufanyiana mitihani na wangesifiwa kabisa!
 
Issue hapo ni ushahid mzee kumbka hapo ni radio station unaweza kujitapa unakaa masaki na unamiliki range wakati ulikwenda hapo na boda boda toka gongo la mboto
Si wamekiri wenyewe kwa vinywa vyao hahahaha sasa ushahidi gani tena?
 
Wanaweza kusema hiyo kauli waliyotoa ilikuwa ni kuchangamasha tu mahojiano kwenye media waliyokuwepo. Ni ngumu kwa chuo kuthibitisha kuwa mmoja alimfanyia mitihani pacha wake.
 
Hakuna hatua yoyote inayoweza kuchukuliwa.

Ingekuwa sheria za nchi zipo hivyo basi jeshi la polisi lingekamata wanaotoa ushuhuda makanisani.
Sure. Hata watuumiwa wanapokuwa wamekamatwa na kutakiwa kuandika maelezo yao hatimaye uyakana mahakamani na kudai waliyaandika kutokana na undue influence/coercion/intimidation kutoka kwa waliokuwa wakiwachukua maelezo.
 
Hivi kwa kizazi cha sasa mtu aliemaliza Chuo mwaka 2021 kwa sasa atakua na umri gani?! Najaribu kufikiria labda bado ni watoto coz kwa mtu mzima kabsa huwezi kuongea issue kama hii kwenye media hata kama hizo degree hawana kazi nazo. Wanachafua sector ya Elimu na hata wao wenyewe, kwa uropokaji huo ni ngumu kuaminiwa kwenye sensitive issues
 
If you have found guilty or misconduct, even decades after graduating, academic institutions have the right to revoke your degree.

A college can revoke a degree if a student is discovered to have earned it illegitimately, be it by plagiarism or any other form of academic misconduct.

Kwa msaada wa mtandao.
Degree ni mali ya Chuo na wana mamlaka ya kukunyang'anya muda wowote pale ambapo watagundua kuna walakini.
 
Kuna mwaka kijana mmoja kutoka Ujerumani alifichua kuwa waziri mmoja aliiba tasnifu yake ya master's degree. Yule kijana alimkomalia waziri mpaka waziri akajiuzulu.

Nataka kusema kwamba. Kwa nchi zilizoendelea, mtu akifanya udanganyifu kwenye elimu anajitahidi kuuficha asibainike kwa sababu anajua madhara yake, lakini kwa Tanzania kwa sasa mtu anaona fahari kutrend kwa kuibua kioja bila kujali madhara yake huko mbeleni. Kwa sasa teknolojia inahifadhi, hao wanafunzi watakuja kuumbuka huko mbeleni!
 
Tumekuwa tukisikia hapa Duniani hasa Tanzania kuwa huwa kuna degree za bure na wengine wamekuwa wakisema kuna degree za chupi!

Lakini sijawai kusikia au kuona watuhumiwa wakikiri kufanya uhalifu kabisa hadharani!

Chuo cha Ardhi ni chuo kizuri lakini ikifika hatua ya watu kisa tuu mapacha wanaweza kufanyiana mitihani na wana kiri hadharani kuwa walifanyiana mitihani tena ya supplimentary basi ujue hii ni hatua kubwa na dharau kubwa sana kwa taasisi hasa ya Elimu ya juu na inayo aminika!

Hawa mabinti wanasema waliweza kufanyiana mitihani na walimaliza chuo kikuu Ardhi(ARU) mwaka 2021 hakuna aliyegundua na sasa wanakwenda hadharani kusema kuwa waliweza kufanya hivyo ni wazi dharau sana kwa taasisi hii ya Elimu na inathibitisha kuwa taasisi hii haiko makini na kuna walakini kwenye hutoaji wa Elimu!

Watu wana hangaika sana kupata elimu halafu watu wanaidhalilisha elimu kiasi hiki …hii ni aibu kwa chuo cha Ardhi na Wizara ya Elimu pia!

Watu wengi wamekuwa wakitilia mashaka sana Elimu zetu hasa utoaji wake na sasa ni wazi wahalifu wameanza kutoa ushahidi wa mashaka kwenye hizi degree zilizojaa mtaani!

Ni matuamaini yangu taasisi itachukua hatua kali dhidi ya uhalifu huu wa kielemu uliofanywa na hawa mapacha na kwenda kukiri hadharani kwenye chombo cha habari Wasafi FM!

Source: Wasafi FM

View attachment 2926553
Kumbe ndio maana miji yetu haipangiki kwa kuwa wapanga miji na watu wa mazingira wanafanyia mitihani!Tuna shida kubwa!
 
Kuna mwaka kijana mmoja kutoka Ujerumani alifichua kuwa waziri mmoja aliiba tasnifu yake ya master's degree. Yule kijana alimkomalia waziri mpaka waziri akajiuzulu.

Nataka kusema kwamba. Kwa nchi zilizoendelea, mtu akifanya udanganyifu kwenye elimu anajitahidi kuuficha asibainike kwa sababu anajua madhara yake, lakini kwa Tanzania kwa sasa mtu anaona fahari kutrend kwa kuibua kioja bila kujali madhara yake huko mbeleni. Kwa sasa teknolojia inahifadhi, hao wanafunzi watakuja kuumbuka huko mbeleni!
Ni aibu sana!
 
Back
Top Bottom