Don Clericuzio
JF-Expert Member
- Dec 8, 2017
- 16,930
- 40,556
Baba yangu sisi wabongo ni wajuaji kinyamaa alafu wabishi dunia nzima!
Nilitegemea kukuta ubishi wa hivyo yani mtu hata hajasikiliza Radio labda mara ya mwisho amesikiliza miezi minne nyuma lakini anabisha tu hahahahaha kudadaaadeki😂😂
Nilijua naeleweshwa na mtu mwenye busara.
Ha ha ha ha! acha kusumbua wenzako.Amani itawale baina yenu .. msimpe nafasi shetani akafanikiwa kuwa gombanisha
Kipindi Cha michezo cha asubuhi kumbukumbu zangu zinaniambia mwasisi Ni RFA. Kilikuwa kinaanza saa 1:30 asubuhi hadi saa 1:50 asubuhi.Hatimaye Clouds FM moja kati ya redio kubwa Tanzania imeanzisha kipindi cha michezo asubuhi kiitwacho Hili Game.
Ikumbukwe Efm ndio mwasisi wa kipindi cha michezo asubuhi kitwacho Sports HQ.
Zamani ili kuwa nadra sana Clouds ku-adapt mifumo ya vipindi vya redio zingine hakika katika hili ni mapinduzi Efm wameleta katika tasnia ya media.
Hawajaishiwa mzee, issue ni kuwahabarisha wateja wao ..kuhakikisha msikilizaj abanduk redionClouds imeishiwa kitambo tu, hawana jipya hata kidogo. Wasafi nao ni wachovu sana kwa vipindi vya redio.
Naaaam, RFA ndiyo waasisi wa vipindi vya michezo asubuhi.vipindi vya michezo asubuhi vilianzishwa na Radio free africa, walianza na kipindi chao mwaka 2006 kuanzia saa 1:20 asubuhi
🏃😁Ha ha ha ha! acha kusumbua wenzako.
Yes, baada ya matukio. Enzi hizo inabamba sana, kisha baada ya michezo yanafuatia matangazo hadi saa mbili kamili, muhtasari wa habari kisha anaingia Fredwaa na sindano tano za moto. Inafuata RFA bonanza hadi saa sita mchana kisha mapishi na salamu, taarifa ya habari saa 6 na nusu. Saa saba ni DW. Saa nane ni Showtime hadi saa 10 jioni. Kisha mambomambo na RFA hadi 12 kamili, DW kwa nusu saa inafuata BBC. Ilikuwa bandika bandua. Sijui kwnn wamepoa sana siku hizi.Naaaam, RFA ndiyo waasisi wa vipindi vya michezo asubuhi.
Mkuu inaonekana ulikuwa mfuatiliaji mzuri sn wa RFA kipindi hicho.Yes, baada ya matukio. Enzi hizo inabamba sana, kisha baada ya michezo yanafuatia matangazo hadi saa mbili kamili, muhtasari wa habari kisha anaingia Fredwaa na sindano tano za moto. Inafuata RFA bonanza hadi saa sita mchana kisha mapishi na salamu, taarifa ya habari saa 6 na nusu. Saa saba ni DW. Saa nane ni Showtime hadi saa 10 jioni. Kisha mambomambo na RFA hadi 12 kamili, DW kwa nusu saa inafuata BBC. Ilikuwa bandika bandua. Sijui kwnn wamepoa sana siku hizi.
Acha kabisa mkuu. Enzi hizo nilikuwa nachelewa hata kwenda shule sababu ya mpangilio wa vipindi. Kuna muda ilinilazimu kukwepa masomo ili nisikilize redio. Ukija wikend ndio ilikuwa balaa lenyewe. Kuna kipindi kiliitwa Hindu style kama sikosei, ilikuwa inaelezewa movie ya kihindi na unaimagine kama unaona live kabisa. Zilikuwa zikipigwa nach za kutosha usiku wa kipindi. Rest in peace RFA ya enzi hizo. Sound engineers walikuwa makini na sauti ilikuwa haiumizi masikio. Siku hizi sijui wameajiri watu gani, sauti haivutii na kuna muda inakuwa kama inaparaza speaker.Mkuu inaonekana ulikuwa mfuatiliaji mzuri sn wa RFA kipindi hicho.
Ukweli ni kuwa RFA ilikuwa redio bora sana siku za nyuma lkn nadhani Management imewaangusha mpaka watangazaji wote wazuri wakakimbia!
Ukifatilia vizuri utagundua karibu nusu ya watangazaji maarufu wa redio na tv nchini ni zao la RFA.
Mwambie huyo boya sio kutafuta kosa kwa sababu humpendi basi kila baya unampaHili game ni session ndani ya PB, na ipo muda mrefu sana.
Maulidi Baraka Kitenge ni mmoja kati ya watangazaji waliokuwa wanasauti za kimichezo tangu zamani. Jezi nambari 9 mgongoni. Jamaa anajua sana aisee.Radio One ilikuwa nzuri kwa kipindi cha michezo enzi hizo. Key mtangazaji? Maulid Kitenge.
Ikaja EFM ikawasha moto. Key anchor? Maulid Kitenge.
Kwa sasa inavuma Wasafi na Sports Arena/ Sports Court. Key anchor? Kitenge once again.
In two or tree years kunaweza kutokea Radio nyingine. Sina shaka nahodha wa kipindi cha michezo atakuwa nani.
Upo Kama mimi Jumbe BrownIla hawa SPORTS ARENA...
Really nilikuwa sikosi kuwasikiliza kina Jeff Lea na wenzake wa mawingu...
Toka waje akina G.Ambangile na crew yake pale WASAFI FM daah SIWABUNDUKI...huniachia siku mojamoja kwenda kuwasikiliza sports court hapo mawinguni...
Ameshatafuta ndio amepata ndio mana amkeuja hapa kama wewe ulivokua, kiherehere kuja hapa kwa kua tayari una mapesa ya kutoshaKatafute pesa mkuu achana na yasokuhusu.
Issue ni kwamba binadamu tunapenda sana matunda ya mafanikio au kuwaona watu ni mashujaa kwa kuwa wanakuwa "nyuso" za firm husika.Ndo biashara na maisha yalivyo
Anakuja mtu unamdharau ana take over
Hadi unalazimika kujifunza kwake..
Industry ambayo unafikiri wewe ndo pioneer
Na hakuna anaeijua kama wewe
Wanaibuka chipukizi wanaitawala Hadi unaondolewa kabisa au kujifunza kuwa copy
FM radio ya Kwanza ni redio one
Leo iko wapi??
Gazeti la michezo la kwanza ni dimba
Leo liko wapi??
Huku kwetu Bara kuna Redio kabisa ya michezo ya Abdallah Majura kwa hiyo ni Redio nyingi tu zinaanza na Michezo asubuhi.Baba yangu sisi wabongo ni wajuaji kinyamaa alafu wabishi dunia nzima!
Nilitegemea kukuta ubishi wa hivyo yani mtu hata hajasikiliza Radio labda mara ya mwisho amesikiliza miezi minne nyuma lakini anabisha tu hahahahaha kudadaaadeki😂😂