Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

on second a thought, binafsi nashawishika kuamini kuwa kufungiwa kwa Clouds Media kuna mkono wa MATAGA nyuma yake?

why nasema hivi?

karibia wiki ya 2 sasa Clouds wamekuwa wakimpa promo kubwa Lady Jaydee katika maandalizi take kuelekea kwenye concert yake kubwa ya tarehe 4 September ambapo atakuwa anaadhimisha 20th anniversary tangu alipojikita kwenye tasnia ya muziki.

sasa... tunajua Lady Jaydee ni "shangazi" fulani hivi kwenye misimamo yake, na MATAGA na "mashangazi" huwaga hawapikiki chungu kimoja kabisa.
am pretty sure you guys now know where am heading to, right? hahahahahaaa!

so, this Clouds Media ban is an indirect sabotage vs Lady Jaydee's preparations ahead of her grand concert next week.

this could be the most feasible explanation ya hii ban ya sasa. I can't put my finger on any other reason kwani Clouds na MATAGA have been sleeping in the same bed for 5 years now na Clouds kufungiwa kwa jambo linalowasaidia MATAGA simply doesn't add up!

udhahidi huu hapa... kama Klauz wamefungiwa, why not gazeti la Uhuru?

IMG_20200827_184732.jpg
 
Wakurungezi waliokuwa wanawatangaza wabunge wa CCM na kuwathibitisha kwa hati kuwa ni wabunge wamepita bila kupingwa wameachwa wanafungiwa wale waliotangaza kile kilichotangazwa na wakurugenzi ambao ndio tume yenyewe.
Nadhani hapa ametafutwa wa kuangushiwa jumba bovu..
 
Hawa wanaofungia vyombo vya habari wangetafakari kwanza wanapoteza ajira za watanzania wangapi? Au hao walishatengeneza ajira ngapi? Au hao hawaoni hii changamoto ya ajira?

Wakati mwingine watanzania tunakatishana tamaa wenyewe, hili suala la kutangaza matokeo kabla ya tume ni suala la kupewa onyo tu ingetosha kuliko kutukosesha habari wiki nzima.

Wajue pia kuna vipindi vya kuwasaidia watu kama njia panda, je wanajua kua wameharibia watu kusaidiwa?

..tuna kiongozi mkuu MKATILI.

..hivyo kilichotokea ni trickle-down effect.

..wa chini yake nao wanaiga ukatili wake ktk maeneo yao.
 
Na hii kushinda bila wananchi kupiga kura Ni ushenzi mkubwa Karne hii, Sasa mtu kujaza fomu kwanini tume isiwarekebishe hzo fomu watu waingie kwenye uchaguzi na wapigiwe kura, nchi hii tumerudi nyuma Sana kudemocracy, eti mtu anafurahia kupita bila kupigiwa kura

Halafu wao wenyewe ndio waluosema awe darasa la 7. Sasa NEC waichukuwe ile fomu waipeleke kwa mtoto wa darasa la 7 aijaze. Wakitowa jawabu kuwa wana option ya kujaziwa na Wanasheria mimi nitawauliza huko Bungeni mbona haviweki viti viwili kimoja kikiwa cha msaidizi wake awe anamsaidia kuwakilisha mada pia!
 
Mbona TCRA imemwacha Millard Ayo maana yeye ndio alitangaza wagombea kupita nakuwa wabunge ikiwemo Kasimu Majaliwa, na wale Morogoro
Huyo wakwao wanamtumia bado naye akichokwa mtamsikia...
 
Source: simulizi na sauti.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imeifungia Clouds TV na Clouds FM Radio kwa siku 7 kuanzia Agosti 28 hadi Septemba 3, 2020 kufuatia kukiuka kanuni za utangazaji ikiwemo kanuni ndogo za utangazaji wa uchaguzi.

TCRA imesema kosa walilolifanya ni kutangaza takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na vituo hivyo vimetakiwa kuomba Radhi S
 
 
Haya mambo ya kufungiana huwezi kuyasikia kabisa kwa east africa radio. Wale jamaa wako makini sana duh
 
Kwani TCRA Wameamua Kimabavu Ama Wamesimamia SHERIA....SHERIA ya takwimu........?!!!

Ni kweli, ila ni sheria zenye nia ovu. Hata huko Afrika kusini enzi za makaburu kulikuwa na sheria zenye nia ovu kama hizi hizi. Clouds walikuwa na tabia ya kujipendekeza sana kaa serikali, acha wajue kuwa waliokuwa wakijipendekeza kwao sio watu wazuri. Cha ajabu wakurugenzi waliotangaza wagombea waliopita bila kupingwa bado wako ofisini.
 
Take it from me, Clouds watafunguliwa na mkuu atatamka mwenyewewe jukwaani kwamba nimewasamehe endeleeni kutoa burudani na hii itafanyika kutafuta Milage. Hawana siku 3 au 4 kabla hawajafunguliwa na itaandikwa Barua kabisa ya kutoa msamaha.
 
Tangu jasiri muongoza njia aondoke Mawingu imekuwa ya hovyo
Ilikuwa hovyo hata kabla. Imekuwa hovyo zaidi na sioni kama uongozi wa sasa una nia au uwezo wa kutoka kwenye kifungo walichojiingiza. Wangebaki kama chombo cha burudani tu.
 
Back
Top Bottom