Clouds media wanavuna walichopanda wasitafute mchawi

Clouds media wanavuna walichopanda wasitafute mchawi

Yule Dada Ni shupavu tu Angekuwa mwingine angeshajikatia tamaa sababu ya fitina hizi za clouds
NAONGEZEA
Komando Jide alikua na kashow kake nao clouds bila hiyana wakaweka show ya Mwana FA siku hiyohiyo.
Komando Jide alitamani kulia aisee.
 
Hawa mabwenyenye wa media Tanzania kwa muda mrefu sana walizoea kuishi kwa mazoea, waliishi kwa kujipendekeza kwa serikali ya ccm na ndivyo wanavyoishi mpaka Leo

Mara nyingi hawa mabwenyenye hawafuti ethics za kazi yao hujiona bora kuliko media nyinginezo

Tunajua clouds media ilipaa sana Kipindi cha kikwete, walipiga sana pesa walipata fursa nyingi sana tunajua mzee kikwete Ni mtu simple alikuwa anapiga interview pale kila Mara


Nakumbuka kina kibonde walikuwa wanawanyea sana wapinzani na kuipigia makofi ccm

Yaan Kipindi cha kikwete mpinzan kusikiliza clouds ilikuwa kama unakalia kaa la moto wenyewe muda wote ilikuwa kuukashifu upinzani

Hawakujua hawakujua kuwa unafki una mwisho, hawakujua uongo una mwisho hawakujua dhuluma Ina mwisho
Hawakujua kuwa kila zama Zina mtume wake walifikiri mzee jk atadumu milele

Angalia Sasa pamoja na kujipendekeza kote awamu hii bado hawapati kile walichozoea kukipata
Kila wanachogusa wanapuyanga. Kama wangekuwa werevu wangekaa chini wakajiuliza

Nimesikia kuwa hawakukubaliwa kufanya onesho pale leaders ila wenyewe wakajiamini kwa kuwa walijua wao Ni makaada wa ccm

Mbona EFM waliomba pale walanyimwa na walipewa sababu

MI binafsi sifurahi kunyimwa kwa tamasha lenu kufanyika ila matatizo ya Leo mliyatengeneza wenyewe siku nyingi

Badilikeni...mbona huwa mnasema uyo ruge Ni usalama wa Taifa ameshindwa kutumia kofia yake kushawishi mamlaka?

Kuna media huwa zinanyanyaswa na mamlaka ila huwezi kuta wanalalamika hadharani nyie mmebanwa kende kidogo tu mshaanza kulia Lia,,, alahhh
Ninaheshimu maoni yako lakini hujawatendea haki Clouds, ujue media kama hiyo ina wasikilizaji wengi na wenye interest tofauti, kwa bahati mbaya umetofautiana nayo,hiyo haitoshi kuwahukumu hivyo kwa sababu wasikilizaji wa clouds radio na media zao zingine bado ni wengi tu. kwa mfano mimi nilikuwa sisikilizi kabisa clouds hasa kipindi kile ulichokitaja,lakini leo nawasikiliza sana hasa PB ndio nina muda, kiukweli wanafanya vizuri.Wanaelimisha, wanatoa fursa kwa watu kwenda kujitangaza hasa waandishi wa vitabu, akina Dr.Isaac wameelimisha sana kuhusu afya, KP ni msema kweli tu hajui kujikombakomba,na wala sijaona kama wako political oriented. waache wachape kazi TZ inahitaji sana media huru kuchangia maendeleo ya nchi hii. JARIBU TU KUTAFUTA NGUVU UFUNGUE RADIO/TV/GAZETI na vitu kama hivyo halafu utatuona mwitikio wetu. ISSUE C CHAMA/SERIKALI isuue ni kuvuta wasikilizaji wangapi ili ufanye biashara. WABEJA NG'WANA MAYU!!!
 
Acha uongo.
Mbona hakuna kilicho mpata Gwajima
Ndo kwanza nGwaj yupo mjengoni, yule bingwa aliangukia pua, siku hizi mpanda bodaboda Kama sisi tu hakuna Cha lst aliyokuwa anaziponda Wala Nini.
 
Back
Top Bottom