COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu

COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu

Moja ya sababu inayofanya watu kuamini kuwa kuna mungu ni uwepo wa huu ulimwengu,na ukitafakari kuhusu huu ulimwengu inazidisha kuamini kuwepo kwa mungu.

Kwa nini uwepo wa ulimwengu ukufanye uamini uwepo wa mungu?

Kuna uhusiano gani kati ya kuwepo kwa ulimwengu na kuwepo kwa mungu?

Uhusiano huo unaoneshaje kwamba ulimwengu huu unawezekana kuwepo tu ikiwa mungu yupo na hauwezi kuwepo vinginevyo?

Mbona hujanijibu swali langu ambalo limetokana na kuona kwangu kwamba uwepo wa ulimwengu huu ni moja ya sababu inayonifanya nisiamini uwepo wa mungu?

Imekuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kama huu? Hususan kama alikuwa na kila uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Je, ulimwengu huu kuwapo kunatuonesha ushahidi kwamba mungu yupo au kwamba mungu hayupo?
 
Ni kwasababu ana upendo kwa maana ya kutotaka kukulazimisha kukupa kile ambacho hujakitaka,hivyo ndivyo Mungu alivyo,kama unahitaji chochote kutoka kwa Mungu we mwambie tu na atakupa

Mungu hawezi kufanya jambo ambalo hajaombwa kwasababu halazimishi bali watu wanamwendea bila shuruti!

mkuu eiyer nakubaliana na yote uliyoandika..kumbuka Mungu atupi tunachotaka bali utupa tunachostahili maana Mungu atujua zaidi tunavyojijua wenyewe!!
 
Mkuu unataka watu waamini kibubusa?


Mkuu hivi yale maonesho ya mazingaombwe ambayo tunaona kabisa mtu akikatwa kichwa je,wewe unakubali kwamba ni kweli mtu anakatwa kichwa?

Hakuna kitu, mazingaombwe ni tricks tu
 
Kwa nini uwepo wa ulimwengu ukufanye uamini uwepo wa mungu?

Kuna uhusiano gani kati ya kuwepo kwa ulimwengu na kuwepo kwa mungu?

Uhusiano huo unaoneshaje kwamba ulimwengu huu unawezekana kuwepo tu ikiwa mungu yupo na hauwezi kuwepo vinginevyo?

Mbona hujanijibu swali langu ambalo limetokana na kuona kwangu kwamba uwepo wa ulimwengu huu ni moja ya sababu inayonifanya nisiamini uwepo wa mungu?

Imekuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kama huu? Hususan kama alikuwa na kila uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Je, ulimwengu huu kuwapo kunatuonesha ushahidi kwamba mungu yupo au kwamba mungu hayupo?

Uwepo wa ulimwengu unanifanya niamini kuwa mungu yupo ni kwa sababu kinyume na hivyo maana yake ni kwamba huu ulimwengu umetokea tu wenyewe.

Ni vigumu kusema kwamba huu ulimwengu umetokea tu wenyewe na mambo yakawa yanajiendesha yenyewe,kwa hivyo lazima kutakuwa na mwenyewe huu ulimwengu na ndiye mwenye kuhusika na yanayoenda humu ulimwenguni(kuchomaza jua na kuzama,mvua n.k). Mungu ndiye mwenye kusema(ktk vitabu) kuwa yeye ndiye aliyeumba huu ulimwengu.

Kuwepo vinginevyo kwa huu ulimwengu inamaana ya huu ulimwengu umetokea tu wenyewe,na kama nilivyosema inakuwa ngumu kuamini hivyo.


Tushaeleza sana kwamba ameumba hivi kwa sababu, na yote anaonesha uwezo wake,maana angetaka kufanya huu ulimwengu kutokuwa na maovu angefanya.
 
Uwepo wa ulimwengu unanifanya niamini kuwa mungu yupo ni kwa sababu kinyume na hivyo maana yake ni kwamba huu ulimwengu umetokea tu wenyewe.

Ni vigumu kusema kwamba huu ulimwengu umetokea tu wenyewe na mambo yakawa yanajiendesha yenyewe,kwa hivyo lazima kutakuwa na mwenyewe huu ulimwengu na ndiye mwenye kuhusika na yanayoenda humu ulimwenguni(kuchomaza jua na kuzama,mvua n.k). Mungu ndiye mwenye kusema(ktk vitabu) kuwa yeye ndiye aliyeumba huu ulimwengu.

Kuwepo vinginevyo kwa huu ulimwengu inamaana ya huu ulimwengu umetokea tu wenyewe,na kama nilivyosema inakuwa ngumu kuamini hivyo.


Tushaeleza sana kwamba ameumba hivi kwa sababu, na yote anaonesha uwezo wake,maana angetaka kufanya huu ulimwengu kutokuwa na maovu angefanya.

Umejiridhishaje kwamba fafanuzi zilizopo ni ulimwengu kuumbwa na mungu au kutokea wenyewe tu?

Unajuaje kwamba wewe fikra zako za kwamba ama ulimwengu umeumbwa na mungu ama kutokea wenyewe si fikra za kufuata kitu kama line ya reli inayoweza kwenda mbele na nyuma tu bila kujua kwamba kuna juu na chini?

Unajuaje kwamba hakuna fafanuzi nyingine zaidi, fafanuzi ambazo labda hata hatujapata elimu ya kuzielewa kwa sasa?

Na kama ulimwengu huu kwa jinsi ulivyo, in terms of order/intelligence, ni lazima uwe umeumbwa na mungu, then hilo linatueleza kwamba order/intelligence huwa haitikei tu, ni lazima ipangwe/iumbwe.

Kama ni hivyo, mungu aliyeumba ulimwengu yeye ana order/intelligence zaidi ya ulimwengu aliouumba.

Kama ni hivyo, ufafanuzi wako unazalisha swali lingine, ikiwa intelligence/order ninlazima oumbwe na haiwezi kutokea yenyewe (ndiyo maana unasema ulimwengu ni lazima uwe umeumbwa na mungu, na hauwezi kiwa umetokea wenyewe tu) je huyo mungu aliyeumba ulimwengu na mwenye intelligence na order kuliko ukimwengu naye kaumbwa na nani?

Maana kwa mujibu wa kanuni yako inayosema kwamba hakuna order/inyelligence inayoweza kutokea yenyewe tu, ni lazima iwe na muumba, hata mungu wako atahitaji muumba, na muumba wake atahitaji muumba, na muumba wake atahitaji muumba, ad infinitum, ad absurdum.

Unajikuta umemfanya mungu wako kuwa si mungu at all, bali ni a small cog in an infinite machine.

Unaona habari zako zinavyojichanganya na kujipinga zenyewe sasa?

Kwa jusema ulimwengu hauwezi kutokea wenyewr bula kuumbwa na mungu, undirectly umesema hakuna mungu.

Kwa maana mungu utakayemsema kauumba ulimwengu naye atahitaji mungu, na mungu wake atahitaji mungu, ad infinitum, ad absurdum, kama nilivyotaja hapo juu.

Habari ya mungu inajikanganya kwa mara nyingine tena.

Pia unasema ameuumba ulimwengu hivi kwa sababu, na angetaka kuuumba ukimwengu bula maovu angeumba.

Kusema hivi hakujibu swali langu.

Swali langu halikusema kwamba kaumba ilimwengu inaoruhusu maovu bila sababu, limeuliza kwa sababu gani?

Hujajibu swali.

Hujanipa sababu iliyomfanya mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwebgu ambao inaruhusu maovu yasiyosemeja wakati alokuwa na uwezo wote wa kuumba ulimwengu ambao maovu hayawezekani.

Hujalijibu swali hili.

Nikikuuliza, kwa nini unatembea hivyo? Ukinijibu "kwa sababu", unakuwa hujajibu swali kimantiki.

Kwa sababu hujanipa sababu inayokufanya utembee hivyo.

Ndicho ulichofanya hapa.

Badala ya kunipa sababu iliyomfanya mungu aumbe ulimwengu unaoruhusu uovu, unaniambia kaumba ulimwengu hivyo jwa sababu.

Umekimbia swali, hujajibu swali,
 
mkuu eiyer nakubaliana na yote uliyoandika..kumbuka Mungu atupi tunachotaka bali utupa tunachostahili maana Mungu atujua zaidi tunavyojijua wenyewe!!

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote, upendo wote ambaye alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengi ambao mabaya hayawezekani hakuumba ulimwengu huo na kaumba huu ambao mabaya yanawezekana?

Sijaona jibu la kimantiki la swali hili.
 
if their is evil and wrong doings then an equal and greater opposite exists and that is God
 
Sio kila ukweli ni kwa ajili ya kila mmoja ......!!
 
Hujaelewa nini?

Hufahamu maana ya tofauti?

Kitu gani kinakutofautisha wewe unayeamua kuamini mungu yupo na yule anayeamua kuamini mungu hayupo?

Wote mko sawa au mna tofauti?

Tofauti yake ni kama maiti na aliehai.
 
Sio kila ukweli ni kwa ajili ya kila mmoja ......!!

Kwa hiyo hata kama mungu hayupo na huo ni ukweli si sawa kumwambia ukweli huo kila mmoja?

Ndicho unachosema hapa?
 
Kwa hiyo hata kama mungu hayupo na huo ni ukweli si sawa kumwambia ukweli huo kila mmoja?

Ndicho unachosema hapa?

Ukweli hauna "kudhani",ukishasema "kama" tayari huna uhakika na maelezo yako na kwasababu hiyo huo sio ukweli!
 
Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote, upendo wote ambaye alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengi ambao mabaya hayawezekani hakuumba ulimwengu huo na kaumba huu ambao mabaya yanawezekana?

Sijaona jibu la kimantiki la swali hili.


Uwezo wako wa kumpima Mungu unaishia kwenye taswila ya maovu unayoyaona na hutaki kujilazimisha kuona mazuri yake.

mabaya yanayokupata ni kutokana na kukosa maarifa ya Mungu.

Mungu hajaumba baya kwa watu wema bali baya kwa wabaya.na kwa watu wema baya kwao ni changamoto/mtihani ambao anauweza kuufuzu.na Mungu hampi mtihani mwanaadamu unaomzidi ila kwa mtu kama wewe unauita ni ubaya.Nae Mwenyezimungu anakuelekeza/anakugeuzia kwenye SHIDA na HOFU ya ubaya unaounadi.
 
Uwezo wako wa kumpima Mungu unaishia kwenye taswila ya maovu unayoyaona na hutaki kujilazimisha kuona mazuri yake.

mabaya yanayokupata ni kutokana na kukosa maarifa ya Mungu.

Mungu hajaumba baya kwa watu wema bali baya kwa wabaya.na kwa watu wema baya kwao ni changamoto/mtihani ambao anauweza kuufuzu.na Mungu hampi mtihani mwanaadamu unaomzidi ila kwa mtu kama wewe unauita ni ubaya.Nae Mwenyezimungu anakuelekeza/anakugeuzia kwenye SHIDA na HOFU ya ubaya unaounadi.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao unaruhusu mabaya wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya?

Hujajibu hili swali.

Unasema mungu kaumba mabaya kwa wabaya.

Kwa nini karuhusu ulimwengu ambao mabaya yanaweza kuwezekana at alll wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Hujajibu swali hili.
 
Kwa context ipi?

Yoyote ile.

Umesema ukweli hauna kudhani, ukishasema "kama" tayari umedhani na huna uhakika.

Wewe unajua ukweli gani kwa uhakika ambao haujanajisiwa na kudhani?
 
Yoyote ile.

Umesema ukweli hauna kudhani, ukishasema "kama" tayari umedhani na huna uhakika.

Wewe unajua ukweli gani kwa uhakika ambao haujanajisiwa na kudhani?

Kwa context ya ukweli nina uhakika na uwepo wangu ....!!
 
Kwa context ya ukweli nina uhakika na uwepo wangu ....!!

Na hakika hiyo umeipata bila kudhani? Kumbuka suala si hakika tu, bali hakika iliyopatikana bila kudhani.

Kwa maana umeshakubeza kudhani kwa kusema kwamba anayedhani hana hakika na hivyo hana ukweli.
 
Back
Top Bottom